Waamuzi 5
1 Siku hiyo Debora na Baraka mwana wa Abinoamu wakaimba wimbo huu:
2 “Wakuu katika Israeli wanapoongoza, wakati watu wanapojitoa kwa hiari yao wenyewe: mhimidini Mwenyezi Mungu!
3 “Sikieni hili, enyi wafalme! Sikilizeni, enyi watawala! Nitamwimbia Mwenyezi Mungu, nitaimba; kwa wimbo nitamhimidi Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli.
4 “Ee Mwenyezi Mungu, ulipotoka katika Seiri, ulipopita katika mashamba ya Edomu, nchi ilitetemeka, mbingu nazo zikamwaga, naam, mawingu yakamwaga maji.
5 Milima ilitetemeka mbele za Mwenyezi Mungu, Yule wa Sinai, mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli.
6 “Katika siku za Shamgari mwana wa Anathi, katika siku za Yaeli, barabara kuu hazikuwa na watu; wasafiri walipita njia za kando.
7 Mashujaa walikoma katika Israeli, walikoma hadi mimi, Debora, nilipoinuka, nilipoinuka kama mama katika Israeli.
8 Mungu alichagua viongozi wapya vita vilipokuja malangoni ya mji; lakini hapakuonekana ngao wala mkuki miongoni mwa watu elfu arobaini katika Israeli.
9 Moyo wangu u pamoja na wakuu wa Israeli, u pamoja na wale wanaojitoa kwa hiari yao miongoni mwa watu. Mhimidini Mwenyezi Mungu!
10 “Ninyi mpandao punda weupe, mkiketi juu ya matandiko ya thamani, nanyi mnaotembea barabarani, fikirini
11 kuhusu sauti za waimbaji mahali pa kunyweshea maji. Wanasimulia matendo ya haki ya Mwenyezi Mungu, matendo ya haki ya mashujaa wake katika Israeli. “Ndipo watu wa Mwenyezi Mungu walipoteremka malangoni pa mji.
12 ‘Amka, amka! Debora! Amka, amka, uimbe! Ee Baraka! Inuka, chukua mateka wako uliowateka, ee mwana wa Abinoamu.’
13 “Ndipo mabaki ya watu wakashuka dhidi ya wakuu, watu wa Mwenyezi Mungu wakashuka kwangu dhidi ya wenye nguvu.
14 Baadhi yao walitoka Efraimu, ambao chimbuko lao ni Amaleki; Benyamini alikuwa miongoni mwa watu waliokufuata. Kutoka Makiri wakashuka viongozi, na kutoka Zabuloni wale washikao fimbo ya jemadari.
15 Wakuu wa Isakari walikuwa pamoja na Debora; naam, Isakari alikuwa pamoja na Baraka, wakija nyuma yake kwa mbio wakielekea bondeni. Katika jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
16 Kwa nini ulikaa katikati ya mazizi ya kondoo kusikiliza sauti ya filimbi zinazoita makundi? Kwa jamaa za Reubeni, palikuwa na kujihoji kukubwa moyoni.
17 Gileadi alikaa ng’ambo ya Yordani. Naye Dani, kwa nini alikaa kwenye merikebu siku nyingi? Asheri alikaa kwa utulivu ufuoni mwa bahari, akikaa kwenye ghuba zake ndogo.
18 Watu wa Zabuloni walihatarisha maisha yao, vilevile nao watu wa Naftali.
19 “Wafalme walikuja na kufanya vita; wafalme wa Kanaani walipigana huko Taanaki, karibu na maji ya Megido, lakini hawakuchukua nyara za fedha.
20 Kutoka mbinguni nyota zilipigana, nyota kutoka njia zake zilipigana na Sisera.
21 Mto wa Kishoni uliwasomba, ule mto wa zamani, mto wa Kishoni. Songa mbele, ee nafsi yangu, kwa ujasiri!
22 Ndipo kwato za farasi zikafanya mshindo: farasi wake wenye nguvu huenda mbio kwa kurukaruka.
23 Malaika wa Mwenyezi Mungu akasema, ‘Laani Merozi. Laani watu wake kwa uchungu, kwa kuwa hawakuja kumsaidia Mwenyezi Mungu, kumsaidia Mwenyezi Mungu dhidi ya hao wenye nguvu.’
24 “Yaeli abarikiwe kuliko wanawake wote, mkewe Heberi, Mkeni, abarikiwe kuliko wanawake wote wanaoishi kwenye mahema.
25 Sisera alimwomba maji, naye akampa maziwa; kwenye bakuli la heshima akamletea maziwa mgando.
26 Akanyoosha mkono wake akashika kigingi cha hema, mkono wake wa kuume ukashika nyundo ya fundi. Akampiga Sisera kwa nyundo, akamponda kichwa chake, akamvunjavunja na kumtoboa paji lake la uso.
27 Aliinama miguuni pa Yaeli, akaanguka; akalala hapo. Alipoinama miguuni pake, alianguka; pale alipoinamia, ndipo alipoanguka, akiwa amekufa.
28 “Kupitia dirishani mamaye Sisera alichungulia; nyuma ya dirisha alilia, akasema, ‘Mbona gari lake la vita linachelewa kufika? Mbona vishindo vya magari yake ya vita vimechelewa?’
29 Wajakazi wale wenye busara kuliko wengine wote wanamjibu; naam, naye anasema moyoni mwake,
30 ‘Je, hawapati na kugawanya nyara: msichana mmoja au wawili kwa kila mtu, mavazi ya rangi mbalimbali kwa Sisera kuwa nyara, mavazi ya rangi mbalimbali yaliyotariziwa, mavazi yaliyotariziwa vizuri kwa ajili ya shingo yangu: haya yote yakiwa nyara?’
31 “Adui zako wote na waangamie hivyo, Ee Mwenyezi Mungu! Bali wote wanaokupenda na wawe kama jua linavyochomoza kwa nguvu zake.” Hivyo nchi ikawa na amani kwa miaka arobaini.
Cross-references
194
- 1Exo 15:1, Rev 19:1–3, Isa 12:1–6, Psa 18:1, Rev 15:3–4, 1Sa 2:1, Exo 15:21, Luk 1:67–68
- 2Jdg 5:9, 2Ch 17:16, Psa 110:3, Php 2:13, Psa 136:15, Rev 19:2, Neh 11:2, 2Co 8:12
- 3Psa 138:4–5, Psa 2:10–12, Psa 49:1–2, Psa 119:46, Ezr 7:21, Gen 9:9, 1Ki 19:10, Lev 26:28
- 4Deu 33:2, Psa 77:17, Psa 68:7–8, Job 9:6, Psa 18:7–15, 2Sa 22:8, Hab 3:3–6
- 5Exo 19:18, Psa 97:5, Nam 1:5, Isa 64:1–3, Hab 3:10, Psa 68:8, Heb 12:18, Deu 4:11–12
- 6Isa 33:8, Jdg 3:31, Lev 26:22, Lam 1:4, Mic 3:12, Lam 4:18, 2Ch 15:5, Jdg 4:17–18
- 72Sa 20:19, Isa 49:23, Est 9:19, Jdg 4:4–6, Rom 16:13
- 8Deu 32:16–17, Jdg 2:12, Jdg 2:17, Jdg 4:3, 1Sa 13:19–22
- 9Jdg 5:2, 2Co 9:5, 2Co 8:3–4, 2Co 8:17, 2Co 8:12, 1Ch 29:9
- 10Jdg 12:14, Jdg 10:4, Psa 105:2, Isa 28:6, Psa 145:11, Psa 145:5, Psa 107:32, Jol 3:12
- 11Mic 6:5, Jdg 5:8, 1Sa 12:7, Deu 22:24, Lam 5:4, Jer 7:2, Lam 5:9, Isa 12:3
- 12Eph 4:8, Psa 68:18, Psa 57:8, 2Ti 2:26, Eph 5:14, 1Co 15:34, Psa 108:2, Isa 60:1
- 13Rev 2:26–27, Isa 41:15–16, Rom 8:37, Psa 75:7, Rev 3:9, Ezk 17:24, Dan 7:18–27, Psa 49:14
- 14Jdg 3:13, Jdg 12:15, Jdg 3:27, Num 32:39–40, Jdg 4:14, Jdg 4:10, Jdg 4:5–6, Exo 17:8–16
- 15Jdg 4:14, Jdg 4:10, 2Co 11:2, 1Ch 12:32, Jdg 4:6, Pro 22:13, Act 15:39, Act 20:13
- 16Num 32:24, Num 32:1–5, Jdg 5:15, Php 2:21, Psa 77:6, Php 3:19, Lam 3:40–41, Psa 4:4
- 17Jos 13:25, Jos 19:24–31, Jos 13:31
- 18Jdg 4:10, Jdg 4:6, Rev 12:11, Est 4:16, 1Jn 3:16, Jdg 4:14, Act 20:24
- 19Jdg 5:30, Jdg 1:27, 1Ki 4:12, Jos 10:22–27, Gen 4:16, Psa 48:4–6, Jos 11:1–15, Psa 44:12
- 20Jos 10:11, Psa 77:17–18, 1Sa 7:10, Jdg 4:15
- 21Jdg 4:7, Mic 7:10, Psa 44:5, Isa 25:10, Jdg 4:13, Gen 49:18, 1Ki 18:40, Psa 83:9–10
- 22Isa 5:28, Psa 33:17, Psa 20:7, Jer 47:4, Mic 4:13, Psa 147:10–11
- 23Jer 48:10, 1Co 16:22, 1Co 3:9, Jdg 21:9–10, 1Sa 26:19, Rom 15:18, Jdg 2:1, 1Sa 17:47
- 24Luk 1:42, Luk 1:28, Jdg 4:17, Gen 14:19, Pro 31:31
- 25Jdg 4:19–21
- 261Sa 17:49–51, Jdg 4:21, 2Sa 20:22
- 27Psa 52:7, Jas 2:13, Mat 7:2
- 28Jas 5:7, Sng 2:9, Sng 8:14, 2Ki 1:2, Pro 7:6, Jdg 4:15
- 30Exo 15:9, Psa 45:14, 2Sa 13:18, Gen 37:3, Job 20:5
- 31Psa 37:6, 2Sa 23:4, 1Co 8:3, 1Pe 1:8, Psa 19:4–5, Jas 1:12, Psa 91:14, Jas 2:5
Topics in this chapter
54
Archery, Armies, Art, Asher, Ass (Donkey), Barak, Benjamin, Butter, Captivity, Chiding, Country, Curse, Dan, Deborah, Embroidery, Epic, Forty, God, Heber, House, Intercession, Israel, Issachar, Jael, Joy, Judge, Kishon, Lukewarmness, Megiddo, Meroz, Meteorology and Celestial Phenomena, Milk, Money, Mountain, Music, Naphtali, Patriotism, Pen, Poetry, Praise, Psalms, Reubenites, Righteous, Servant, Shamgar, Sisera, Song, Sun, Taanach, Thankfulness, Victories, Volcanoes, Women, Zebulun