1 Samweli 11
1 Nahashi Mwamoni akakwea kuuzingira mji wa Yabesh-Gileadi kwa jeshi. Wanaume wote wa Yabeshi wakamwambia, “Fanya mkataba nasi, na tutakutumikia.”
2 Lakini Nahashi yule Mwamoni akajibu, “Nitafanya mkataba na ninyi tu kwa sharti kwamba nitang’oa jicho la kulia la kila mmoja wenu, na hivyo kuleta aibu juu ya Israeli yote.”
3 Viongozi wa Yabeshi wakamwambia, “Tupe siku saba ili tuweze kutuma wajumbe katika Israeli yote. Ikies hakuna hata mmoja atayekuja kutuokoa, tutajisalimisha kwako.”
4 Wajumbe walipofika Gibea ya Sauli na kutoa taarifa kuhusu masharti haya kwa watu, wote walilia kwa sauti kubwa.
5 Wakati huo huo Sauli alikuwa anarudi kutoka mashambani, akiwa nyuma ya maksai wake, naye akauliza, “Watu wana nini? Mbona wanalia?” Ndipo wakamweleza vile wanaume wa Yabeshi walivyokuwa wamesema.
6 Sauli aliposikia maneno yao, Roho wa Mungu akaja juu yake kwa nguvu, naye akawaka hasira.
7 Akachukua maksai wawili na kuwakata vipande vipande, naye kuvituma hivyo vipande kupitia wajumbe katika Israeli yote, wakitangaza, “Hivi ndivyo itakavyofanyika kwa maksai wa kila mmoja ambaye hatamfuata Sauli na Samweli.” Kisha kicho cha Mwenyezi Mungu kikawaangukia watu, nao wakatoka kama mtu mmoja.
8 Sauli alipowakusanya huko Bezeki, wanaume wa Israeli walikuwa elfu mia tatu, na wanaume wa Yuda elfu thelathini.
9 Wakawaambia wale wajumbe waliokuwa wamekuja, “Waambieni wanaume wa Yabesh-Gileadi, ‘Kesho kabla jua halijawa kali, mtaokolewa.’ ” Wajumbe walipoenda na kutoa taarifa hii kwa wanaume wa Yabeshi, wakafurahi.
10 Wakawaambia Waamoni, “Kesho tutajisalimisha kwenu, nanyi mtaweza kututendea chochote mnachoona chema kwenu.”
11 Kesho yake Sauli alitenganisha watu wake katika vikosi vitatu; wakati wa zamu ya mwisho ya usiku wakaingia katika kambi ya Waamoni na kuwachinja hadi mchana. Wale walionusurika wakatawanyika, hivi kwamba hawakusalia watu wawili pamoja.
12 Kisha watu wakamwambia Samweli, “Ni nani yule aliyeuliza, ‘Je, Sauli atatutawala?’ Tuletee hawa watu, nasi tutawaua.”
13 Lakini Sauli akasema, “Hakuna hata mmoja atakayeuawa leo, kwa kuwa siku hii Mwenyezi Mungu ameokoa Israeli.”
14 Ndipo Samweli akawaambia watu, “Njooni, twendeni Gilgali na huko tuthibitishe ufalme.”
15 Kwa hiyo watu wote wakaenda Gilgali na kumthibitisha Sauli kuwa mfalme mbele za Mwenyezi Mungu. Huko wakatoa dhabihu za sadaka za amani mbele za Mwenyezi Mungu, naye Sauli na Waisraeli wote wakafanya karamu kubwa.
Cross-references
84
- 11Sa 12:12, Ezk 17:13, 1Ki 20:34, Gen 26:28, Jdg 21:8, Job 41:4, Exo 23:32, Isa 36:16
- 21Sa 17:26, Gen 34:14, Num 16:14, Jdg 16:21, Exo 3:6, 2Ki 18:31, Jer 39:7, Pro 12:10
- 41Sa 10:26, Jdg 2:4, 1Sa 15:34, Jdg 21:2, 1Sa 30:4, Gal 6:2, Heb 13:3, 1Sa 14:2
- 51Ki 19:19, Gen 21:17, Isa 22:1, 1Sa 9:1, Jdg 18:23, Psa 78:71
- 61Sa 10:10, 1Sa 16:13, Jdg 6:34, Jdg 14:6, Jdg 3:10, Jdg 13:25, Jdg 11:29, Exo 32:19
- 7Jdg 19:29, Jdg 20:1, Gen 35:5, 2Ch 14:14, 2Ch 17:10, Jdg 21:5–11
- 82Sa 24:9, Jdg 1:4–5, Jdg 20:2, 1Sa 13:15, 1Sa 15:4, 2Ch 17:12–19
- 9Psa 18:17
- 101Sa 11:2–3
- 11Jdg 7:16, Exo 14:24, Jas 2:13, Gen 22:14, Mat 7:2, 1Sa 30:17–18, Jdg 4:16, 1Sa 11:2
- 121Sa 10:27, Luk 19:27, Psa 21:8
- 13Exo 14:13, 1Sa 19:5, 2Sa 19:22, 1Sa 14:45, Exo 14:30, Psa 44:4–8, Isa 59:16, 1Co 15:10
- 141Sa 10:8, 1Sa 7:16, 1Sa 10:24–25, 1Ch 12:38–39, 1Sa 5:3
- 151Sa 10:8, 1Sa 10:17, 1Ch 29:21–24, Exo 24:5, Hos 13:10–11, Jas 4:16, 1Sa 12:13–15, 1Sa 12:17