Kutoka 10
1 Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Nenda kwa Farao, kwa kuwa nimeufanya moyo wake kuwa mgumu na mioyo ya maafisa wake ili nipate kutenda ishara hizi zangu za ajabu miongoni mwao,
2 ili upate kuwaeleza watoto wako na wajukuu wako jinsi nilivyowatendea Wamisri kwa ukali, na jinsi nilivyofanya ishara zangu miongoni mwao, nanyi mpate kujua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu.”
3 Kwa hiyo Musa na Haruni wakaenda kwa Farao na kumwambia, “Hili ndilo Mwenyezi Mungu, Mungu wa Waebrania, asemalo: ‘Utaendelea hata lini kukataa kunyenyekea mbele yangu? Waachie watu wangu waende, ili waniabudu.
4 Ukikataa kuwaachia waende, kesho nitaleta nzige katika nchi yako.
5 Nao watafunika uso wa ardhi hata usionekane. Watatafuna mabaki machache yaliyobakizwa baada ya ile mvua ya mawe, yaani pamoja na kila mti unaoota katika mashamba yenu.
6 Nzige hao watajaza nyumba zako, za maafisa wako wote na za Wamisri wote. Jambo ambalo baba zenu wala babu zenu hawajapata kuona tangu siku ile walipoanza kuishi katika nchi hii hadi leo.’ ” Ndipo Musa akageuka na kumwacha Farao.
7 Maafisa wa Farao wakamwambia, “Hadi lini huyu mtu atakuwa tanzi kwetu? Waachie hao watu waende zao, ili wapate kumwabudu Mwenyezi Mungu, Mungu wao. Je, bado hutambui kuwa Misri imeangamia?”
8 Ndipo Musa na Haruni wakaletwa kwa Farao. Farao akawaambia, “Nendeni, mkamwabudu Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Lakini ni nani hasa watakaoenda?”
9 Musa akajibu, “Tutaenda na vijana wetu na wazee, pamoja na wana wetu na binti zetu, pia pamoja na mbuzi, kondoo, na ng’ombe wetu kwa sababu tutaadhimisha sikukuu kwa Mwenyezi Mungu.”
10 Farao akasema, “Kama kweli nitawaruhusu mwondoke pamoja na wanawake wenu na watoto wenu, Mwenyezi Mungu awe pamoja nanyi! Ni wazi kwamba mna makusudi mabaya.
11 La hasha! Wanaume peke yao na waende, wakamwabudu Mwenyezi Mungu, kwa kuwa hilo ndilo mmekuwa mkiomba.” Kwa hiyo Musa na Haruni wakaondolewa mbele ya Farao.
12 Basi Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Nyoosha mkono wako juu ya Misri, ili kundi la nzige liweze kuvamia nchi na kutafuna kila kitu kinachoota katika mashamba na kila kitu kilichosazwa na ile mvua ya mawe.”
13 Kwa hiyo Musa akanyoosha fimbo yake juu ya Misri, Mwenyezi Mungu akauleta upepo wa mashariki ukavuma katika nchi yote mchana wote na usiku kucha, kufikia asubuhi upepo ukawa umeleta nzige.
14 Wakaivamia Misri yote na kukaa katika kila eneo la nchi kwa wingi. Kamwe halijapata kutokea pigo la nzige kama hilo, wala halitakuwa tena.
15 Wakafunika ardhi yote hata ardhi ikawa nyeusi. Wakatafuna kila kilichokuwa kimebakizwa na ile mvua ya mawe: kila kitu kilichoota shambani, pamoja na matunda kwenye miti. Hakuna kitu chochote cha kijani kilichosalia katika miti au mmea katika nchi yote ya Misri.
16 Farao akawaita Musa na Haruni kwa haraka na kuwaambia, “Nimetenda dhambi dhidi ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na dhidi yenu pia.
17 Sasa unisamehe dhambi yangu mara moja tena na umwombe Mwenyezi Mungu, Mungu wako, aondoe pigo hili baya kwangu.”
18 Kisha Musa akaondoka kwa Farao akamwomba Mwenyezi Mungu.
19 Naye Mwenyezi Mungu akaugeuza upepo kuwa upepo mkali sana kutoka magharibi, ambao uliwaondoa wale nzige na kuwapeleka kwenye Bahari ya Shamu. Hakuna nzige hata mmoja aliyebaki popote katika nchi ya Misri.
20 Lakini Mwenyezi Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, wala hakuwaachia Waisraeli waondoke.
21 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Nyoosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.”
22 Kwa hiyo Musa akaunyoosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu.
23 Hakuna mtu yeyote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo waliyokuwa wanaishi.
24 Ndipo Farao akamwita Musa na kusema, “Nendeni, mkamwabudu Mwenyezi Mungu. Hata wanawake na watoto wenu mwaweza kwenda nao pia, lakini kondoo, mbuzi na ng’ombe wenu waacheni.”
25 Lakini Musa akasema, “Huna budi kuturuhusu tuwe na dhabihu, na sadaka za kuteketezwa za kutoa mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wetu.
26 Sisi ni lazima tuondoke na mifugo yetu pia, wala hakuna ukwato utakaoachwa nyuma. Inatupasa kutumia baadhi ya hiyo mifugo katika kumwabudu Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, kwa kuwa hadi tutakapofika huko, hatutakuwa tumefahamu ni nini tutakachotumia katika kumwabudu Mwenyezi Mungu.”
27 Lakini Mwenyezi Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, hakuwa radhi kuwaachia waondoke.
28 Farao akamwambia Musa, “Ondoka mbele yangu! Hakikisha kuwa hutakuja mbele yangu tena! Siku ile utakapouona uso wangu utakufa.”
29 Musa akamjibu, “Iwe kama ulivyosema! Kamwe sitauona uso wako tena.”
Cross-references
180
- 1Exo 4:21, Exo 7:13–14, Exo 3:20, Rom 9:17, Jos 2:9–10, Exo 15:14–15, Psa 7:11, Exo 9:34–35
- 2Jol 1:3, Deu 4:9, Deu 6:20–22, Exo 13:14, Psa 78:5–6, Exo 7:17, Psa 44:1, Eph 6:4
- 31Pe 5:6, Jas 4:10, 1Ki 21:29, Jer 13:18, Rom 2:4, Heb 12:25, Num 14:27, Jer 13:10
- 4Rev 9:3, Jol 2:25, Exo 9:18, Pro 30:27, Exo 11:4–5, Jol 2:2–11, Exo 9:5, Exo 8:10
- 5Jol 1:4, Exo 9:32, Jol 2:25
- 6Exo 8:21, Exo 8:3, Heb 11:27, Exo 11:8, Exo 10:11, Exo 10:14–15, Exo 9:24, Exo 11:6
- 71Sa 18:21, Ecc 7:26, Exo 23:33, Jos 23:13, Isa 14:20, Exo 8:19, Jer 48:4, Zep 1:18
- 8Exo 10:24, Exo 10:16, Exo 8:8, Exo 12:31
- 9Deu 31:12–13, 1Co 5:7–8, Exo 5:1, Exo 3:18, Exo 8:25–28, Ecc 12:1, Eph 6:4, Gen 50:8
- 10Exo 13:21, 2Ch 32:15, Exo 12:30–31, Lam 3:37
- 11Exo 10:28, Psa 119:69, Psa 52:3–4, Exo 5:4
- 12Exo 7:19, Exo 10:4–5
- 13Psa 148:8, Gen 41:6, Psa 107:25–28, Jon 4:8, Psa 105:34, Mat 8:27, Jon 1:4, Psa 78:26
- 14Psa 78:46, Jol 2:1–11, Rev 9:3–7, Jol 1:2–4, Exo 10:5–6, Deu 28:42, Exo 11:6, Psa 105:34–35
- 15Exo 10:5, Psa 105:34–35, Jol 1:6–7, Psa 78:46, Jol 2:1–11, Jol 2:25
- 16Exo 9:27, 2Sa 19:20, Num 21:7, Pro 28:13, Num 22:34, 1Sa 26:21, Mat 27:4, Job 34:31–32
- 17Exo 8:8, Exo 9:28, 1Ki 13:6, 1Sa 15:25, Isa 26:16, Act 8:24, 2Ki 4:40, 2Co 1:10
- 18Exo 8:9, Exo 8:28–30, Mat 5:44, Luk 6:28
- 19Jol 2:20, Heb 11:29, Exo 15:4, Exo 13:18
- 20Exo 4:21, Exo 11:10, Deu 2:30, Isa 6:9–10, Jhn 12:39–40, Exo 7:13–14, Rom 9:18, Exo 9:12
- 21Jud 1:6, Rev 16:10–11, Luk 23:44, 2Pe 2:17, 2Pe 2:4, Deu 28:29, Psa 105:28, Mrk 15:33
- 22Psa 105:28, Rev 16:10, Jol 2:2, Deu 4:11, Amo 4:13, Jol 2:31, Exo 20:21, Deu 5:22
- 23Exo 8:22, Exo 9:4, Isa 42:16, 1Pe 2:9, Jos 24:7, Col 1:13, Isa 65:13–14, Exo 14:20
- 24Exo 8:28, Exo 10:8–10, Exo 9:28, Gen 34:23
- 25Lev 16:9, Exo 29:1–46, Lev 9:22, Exo 36:1–38
- 26Hos 5:6, Act 2:44–45, Isa 60:5–10, Pro 3:9, Isa 23:18, Heb 11:8, Exo 12:32, Zec 14:20
- 27Exo 10:20, Exo 4:21, Exo 14:8, Exo 14:4, Rev 9:20, Rev 16:10–11, Exo 10:1
- 28Amo 7:13, 2Ch 16:10, 2Ch 25:16
- 29Heb 11:27, Exo 12:30–31, Exo 11:4–8
Topics in this chapter
29
Afflictions and Adversities, Anger, Animals, Conviction, Darkness, Disobedience to God, Egyptians, Falsehood, God, Government, Hypocrisy, Impenitence, Instability, Instruction, Intercession, Israel, Locust, Meteorology and Celestial Phenomena, Miracles, Moses, Parents, Plague, Red Sea, Repentance, Reproof, Rulers, Sin, Sun, Wind