Kutoka 23
1 “Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.
2 “Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu,
3 nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake.
4 “Ukikutana na maksai au punda wa adui yako anapotea, hakikisha umemrudisha kwake.
5 Ukiona punda wa mtu anayekuchukia ameanguka na mzigo wake, usimwache hapo alipoangukia; hakikisha kuwa umemsaidia.
6 “Usiwanyime haki watu wako walio maskini katika mashtaka yao.
7 Ujiepushe na mashtaka ya uongo, wala usimuue mtu asiye na hatia au mtu mwaminifu, kwa maana sitamhesabia hana hatia yeye aliye na hatia.
8 “Usipokee rushwa, kwa kuwa rushwa hupofusha wale waonao, na kupinda maneno ya wenye haki.
9 “Usimdhulumu mgeni; ninyi wenyewe mnajua jinsi mgeni anavyojisikia, kwa sababu mlikuwa wageni Misri.
10 “Kwa muda wa miaka sita mtapanda mashamba yenu na kuvuna mazao,
11 lakini katika mwaka wa saba usiilime ardhi wala kuitumia, ili watu walio maskini miongoni mwenu waweze kupata chakula kwenye hayo mashamba, nao wanyama pori wapate chakula kwa yale mabaki watakayobakiza. Utafanya hivyo katika shamba lako la mizabibu na la mizeituni.
12 “Kwa siku sita fanya kazi zako, lakini siku ya saba usifanye kazi, ili maksai wako na punda wako wapate kupumzika, naye mtumwa aliyezaliwa nyumbani mwako, pamoja na mgeni, wapate kuburudishwa.
13 “Uzingatie kutenda kila kitu nilichokuambia. Usiombe kwa majina ya miungu mingine, wala usiyaruhusu kusikika kinywani mwako.
14 “Mara tatu kwa mwaka utanifanyia sikukuu.
15 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu; kwa siku saba utakula mikate isiyotiwa chachu kama nilivyokuagiza. Fanya jambo hili kwa wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu, kwa sababu katika mwezi huo ulitoka Misri. “Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
16 “Utaadhimisha Sikukuu ya Mavuno kwa malimbuko ya mazao yako uliyopanda katika shamba lako. “Utaadhimisha Sikukuu ya Kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka, unapokusanya mavuno yako toka shambani.
17 “Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakuja mbele za Bwana Mungu Mwenyezi.
18 “Msitoe damu ya dhabihu kwangu pamoja na kitu chochote kilicho na chachu. “Mafuta ya mnyama wa sadaka ya sikukuu yangu yasibakizwe hadi asubuhi.
19 “Utaleta malimbuko bora ya ardhi yako katika nyumba ya Mwenyezi Mungu, Mungu wako. “Usimchemshe mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
20 “Tazama, ninamtuma malaika akutangulie mbele yako akulinde njiani na kukuleta mahali nilipoandaa.
21 Mtamtii na kusikiliza kile anachokisema. Usiasi dhidi yake; hatakusamehe uasi wako, kwa maana Jina langu limo ndani yake.
22 Ukizingatia atakachosema na kufanya yote ninayosema, nitakuwa adui wa adui zako, na nitawapinga wale wakupingao.
23 Malaika wangu atatangulia mbele yako na kukuleta katika nchi ya Waamori, Wahiti, Waperizi, Wakanaani, Wahivi na Wayebusi, nami nitawafutilia mbali.
24 Usiisujudie miungu yao, au kuiabudu, wala kufuata desturi yao. Utayabomoa kabisa na kuvunjavunja mawe yao ya ibada vipande vipande.
25 Utamwabudu Mwenyezi Mungu, Mungu wako, na baraka zake zitakuwa juu ya vyakula vyako na maji yako. Nami nitaondoa maradhi miongoni mwako,
26 na hakuna atakayeharibu mimba wala atakayekuwa tasa katika nchi yako. Nami nitakupa maisha makamilifu.
27 “Nitapeleka utisho wangu mbele yako na kufadhaisha kila taifa utakalolifikia. Nitafanya adui zako wote wakupe kisogo na kukimbia.
28 Nitatanguliza nyigu mbele yako kuwafukuza Wahivi, Wakanaani na Wahiti waondoke njiani mwako.
29 Lakini sitawafukuza kwa mara moja, kwa sababu nchi itabaki ukiwa na wanyama pori watakuwa wengi mno kwako.
30 Nitawafukuza kidogo kidogo mbele yako, hadi uwe umeongezeka kiasi cha kutosha kuimiliki nchi.
31 “Nitaweka mipaka ya nchi yako kuanzia Bahari ya Shamu hadi Bahari ya Wafilisti, na kuanzia jangwani hadi Mto. Nitawatia watu wanaoishi katika nchi hizo mikononi mwako, nawe utawafukuza watoke mbele yako.
32 Usifanye agano lolote nao wala na miungu yao.
33 Usiwaache waishi katika nchi yako, la sivyo watakusababisha utende dhambi dhidi yangu, kwa sababu ibada ya miungu yao hakika itakuwa mtego kwako.”
Cross-references
219
- 1Psa 101:5, Pro 19:5, Deu 19:16–21, Exo 20:16, Mat 26:59–61, Rom 3:8, Psa 35:11, Lev 19:16
- 2Pro 1:10–11, Pro 1:15, Luk 23:23–24, Job 31:34, Mat 27:24–26, 1Ki 19:10, Deu 1:17, Exo 23:6–7
- 3Jas 3:17, Lev 19:15, Psa 82:2–3, Deu 1:17
- 4Deu 22:1–4, 1Th 5:15, Mat 5:44, Rom 12:17–21, Pro 25:21, Luk 6:27–28, Pro 24:17–18, Job 31:29–30
- 5Deu 22:4
- 6Mal 3:5, Jas 2:5–6, Isa 10:1–2, Ecc 5:8, Jer 5:28, Lev 19:15, Deu 27:19, Exo 23:2–3
- 7Eph 4:25, Deu 27:25, Exo 23:1, Exo 34:7, Rom 1:18, 1Th 5:22, Lev 19:11, Deu 19:16–21
- 8Deu 16:19, Pro 17:23, Isa 5:23, Pro 15:27, 1Sa 8:3, Ecc 7:7, Deu 10:17, Psa 26:10
- 9Exo 22:21, Deu 27:19, Mat 18:33, Deu 24:14–18, Exo 21:21, Psa 94:6, Heb 2:17–18, Deu 10:19
- 10Lev 25:3–4
- 11Lev 25:2–7, Lev 26:34–35, Lev 25:11–12, Lev 25:20, Lev 25:22
- 12Luk 13:14, Exo 35:3, Exo 34:21, Exo 31:15–16, Exo 20:8–11, Deu 5:13–15, Isa 58:3
- 13Jos 23:7, Zec 13:2, Deu 4:9, Hos 2:17, 1Ti 4:16, Deu 12:3, Psa 16:4, Jer 10:11
- 14Deu 16:16, Exo 23:17, Lev 23:5, Lev 23:34, Lev 23:16, Exo 34:22–24
- 15Exo 34:20, Luk 22:7, Deu 16:16, Num 28:16–25, Pro 3:9–10, Deu 16:1–8, Lev 23:5–8, 2Ki 23:21–23
- 16Exo 34:22, Lev 23:9–21, Deu 16:9–15, Exo 22:29, Lev 23:34–44, Jhn 7:2, Zec 14:16–19, Act 2:1
- 17Deu 16:16, Exo 34:23, Exo 23:14, Deu 31:11, Deu 12:5, Luk 2:42, Psa 84:7
- 18Lev 2:11, Exo 34:25, Deu 16:4, Exo 12:10, Exo 12:8, Lev 7:15, Exo 12:15, Lev 7:12
- 19Exo 34:26, Deu 14:21, Deu 26:10, Neh 10:35, Exo 22:29, Deu 26:2, Num 18:12–13, Jer 10:3
- 20Exo 33:14, Psa 91:11, Exo 32:34, Exo 14:19, Exo 33:2, Isa 63:9, Jhn 14:3, Mat 25:34
- 21Psa 78:56, Psa 78:40, Heb 12:25, Jhn 10:38, Jhn 10:30, Eph 4:30, Deu 18:19, Heb 10:26–29
- 22Gen 12:3, Deu 30:7, Zec 2:8, Jer 30:20, Num 24:9, Act 9:4–5
- 23Exo 23:20, Isa 5:13, Gen 34:2, Gen 15:19–21, Exo 32:2, Exo 3:17, Jos 24:8–11
- 24Exo 20:5, Num 33:52, Deu 12:30–31, Deu 12:3, Deu 7:5, 2Ch 33:9, Exo 32:20, Lev 18:3
- 25Deu 7:15, Exo 15:26, Jos 22:5, Isa 33:24, Psa 103:3, Deu 7:13, Deu 10:12, Deu 6:13
- 26Deu 7:14, Deu 28:4, Job 5:26, Job 21:10, Isa 65:20, Psa 107:38, Psa 144:13, Mal 3:10–11
- 27Deu 2:25, Gen 35:5, Deu 11:25, Deu 7:23, Exo 15:14–16, Psa 18:40, 1Sa 14:15, 2Ch 14:14
- 28Deu 7:20, Jos 24:11–12
- 29Deu 7:22, Jdg 3:1–4, Jos 17:12–13, Jos 15:63, Jos 16:10
- 31Gen 15:18, Deu 11:24, Jos 21:44, Jos 1:4, Num 34:3–15, 1Ki 4:24, Jos 24:18, Jdg 1:4
- 32Deu 7:2, Exo 34:12, Exo 34:15, Deu 7:16, Psa 106:35, Num 25:1–2, 2Co 6:15, Jos 9:14–23
- 33Psa 106:36, Deu 7:16, Jdg 2:3, Exo 34:12, Jos 23:13, Deu 12:30, 1Ki 14:16, 1Sa 18:21
Topics in this chapter
77
Abib, Accusation, False, Agriculture, Aliens, Alliances, Amorites, Angel (A Spirit), Animals, Ass (Donkey), Blessing, Bribery, Bullock, Canaan, Canaanites, Church, Company, Conspiracy, Court, Disease, Enemy, Euphrates, Evidence, Falsehood, False Teachers, Fat, Feasts, Fellowship, First Fruits, Forgiveness, Goat, God, Hivites, Hornet, Hospitality, Iconoclasm, Idolatry, Industry, Injustice, Israel, Jebusites, Jesus, the Christ, Justice, Labor, Lamb, Land, Leaven (Yeast), Liberality, Mediterranean Sea, Milk, Month, Neighbor, Oath, Obedience, Offerings, Olive, Passover, Pentecost, Perizzites, Philistines, Poor, Popular Sins, Red Sea, Rest, Revelation, Righteous, Rulers, Sabbath, Sabbatic Year, Servant, Slander, Strangers, Stray, Tabernacle, Tabernacles, Feast of, War, Watchfulness, Worship