Waamuzi 8
1 Basi Waefraimu wakamuuliza Gideoni, “Mbona umetutenda hivi? Kwa nini hukutuita ulipoenda kupigana na Wamidiani?” Wakamlaumu kwa ukali sana.
2 Gideoni akawajibu, “Nilichofanya mimi ni nini kulinganisha na kile ninyi mlichofanya? Je, kuokoa masazo ya zabibu za Efraimu si bora kuliko mavuno kamili ya zabibu ya Abiezeri?
3 Mungu amewatia Orebu na Zeebu, hao viongozi wa Wamidiani, mikononi mwenu. Je, mimi niliweza kufanya nini kulinganisha na mlichofanya ninyi?” Aliposema hili, hasira yao dhidi yake ikatulia.
4 Gideoni pamoja na watu wake mia tatu, wakiwa wamechoka sana lakini bado wakiwafuatia, wakafika Yordani na kuuvuka.
5 Akawaambia wanaume wa Sukothi, “Tafadhali lipatieni jeshi langu mikate, kwa maana wamechoka, nami ningali ninawafuatia Zeba na Salmuna, wafalme wa Midiani.”
6 Lakini viongozi wa Sukothi wakasema, “Je, tayari umewakamata Zeba na Salmuna ili tulipatie jeshi lako mikate?”
7 Gideoni akajibu, “Kwa ajili ya hilo tu, Mwenyezi Mungu atakapowatia Zeba na Salmuna mkononi mwangu, nitaichana nyama ya miili yenu kwenye miiba ya nyikani na kwenye michongoma.”
8 Kutoka hapo alikwea hadi Penieli na kutoa ombi lile lile, lakini nao wanaume wa Penieli wakamjibu kama wanaume wa Sukothi walivyokuwa wamemjibu.
9 Hivyo akawaambia wanaume wa Penieli, “Nitakaporudi kwa ushindi, nitaubomoa mnara huu.”
10 Wakati huu Zeba na Salmuna walikuwa Karkori, wakiwa na jeshi la watu wapatao elfu kumi na tano waliokuwa wamesalia wa mataifa ya mashariki, kwa kuwa watu wapatao elfu mia moja na ishirini wenye panga walikuwa wameuawa.
11 Basi Gideoni akakwea kwa njia ya wafugaji wahamaji mashariki mwa Noba na Yogbeha, na kulishambulia jeshi ambalo halikushuku lolote.
12 Zeba na Salmuna, hao wafalme wawili wa Midiani, wakakimbia lakini yeye Gideoni akawafuata na kuwakamata, akalishinda hilo jeshi lao lote kabisa.
13 Gideoni mwana wa Yoashi akarudi kutoka vitani kupitia Mwinuko wa Heresi.
14 Akamkamata kijana mmoja wa Sukothi na kumuuliza maswali, naye yule kijana akamwandikia majina ya viongozi sabini na saba wa Sukothi, ambao ni wazee wa mji.
15 Ndipo Gideoni akaja na kuwaambia wanaume wa Sukothi, “Tazameni Zeba na Salmuna mlionisimanga kwa ajili yao mkisema, ‘Je, tayari umewakamata Zeba na Salmuna ili tulipatie jeshi lako mikate?’ ”
16 Akawachukua hao wazee wa mji, na kuwaadhibu wanaume wa Sukothi kwa kuwachapa kwa miiba na michongoma ya nyikani.
17 Pia akaubomoa mnara wa Penieli na kuwaua wanaume wa huo mji.
18 Kisha akawauliza Zeba na Salmuna, “Ni wanaume wa aina gani mliowaua huko Tabori?” Wakajibu, “Ni wanaume kama wewe, kila mmoja wao akiwa anafanana na mwana wa mfalme.”
19 Gideoni akajibu, “Hao walikuwa ndugu zangu, wana wa mama yangu hasa. Hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo, kama mngekuwa mmewaacha hai, mimi nisingewaua ninyi.”
20 Akamgeukia Yetheri, mwanawe mzaliwa wa kwanza, akasema, “Waue hawa!” Lakini Yetheri hakuufuta upanga wake, kwa sababu aliogopa, kwa kuwa alikuwa bado kijana mdogo tu.
21 Zeba na Salmuna wakasema, “Njoo ufanye hivyo wewe mwenyewe. ‘Alivyo mwanaume, ndivyo zilivyo nguvu zake.’ ” Hivyo, Gideoni akajitokeza na kuwaua, naye akayaondoa mapambo kwenye shingo za ngamia wao.
22 Waisraeli wakamwambia Gideoni, “Ututawale, wewe, mwanao, na mjukuu wako, kwa kuwa umetuokoa kutoka mikononi mwa Wamidiani.”
23 Lakini Gideoni akawaambia, “Mimi sitawatawala ninyi, wala mwanangu hatawatawala. Mwenyezi Mungu ndiye atakayewatawala ninyi.”
24 Naye akasema, “Ninalo ombi moja, kwamba kila mmoja wenu anipatie kipuli kutoka fungu lake la nyara.” (Ilikuwa desturi ya Waishmaeli kuvaa vipuli vya dhahabu.)
25 Wakajibu, “Tutafurahi kuvitoa.” Hivyo wakatanda vazi chini na kila mwanaume akatupia juu yake pete kutoka fungu lake la nyara.
26 Uzito wa pete za dhahabu alizoomba ulikuwa shekeli elfu moja na mia saba, bila kuhesabu mapambo mengine, vidani, na mavazi ya zambarau yaliyovaliwa na wafalme wa Midiani, au mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia wao.
27 Gideoni akatengeneza kizibau kwa kutumia ile dhahabu, ambacho alikiweka katika mji wake, yaani Ofra. Waisraeli wote wakafanya uasherati kwa kukiabudu huko, nacho kikawa mtego kwa Gideoni na jamaa yake.
28 Hivyo Midiani wakashindwa mbele ya Waisraeli, nao hawakuinua vichwa vyao tena. Wakati wa siku za uhai wa Gideoni, nchi ikafurahia amani miaka arobaini.
29 Yerub-Baali mwana wa Yoashi akarudi kwenda kuishi katika nyumba yake.
30 Alikuwa na wana sabini wa kwake mwenyewe, kwa kuwa alikuwa na wake wengi.
31 Suria wake, aliyekuwa anaishi huko Shekemu, pia alimzalia mwana, akamwita jina Abimeleki.
32 Gideoni mwana wa Yoashi akafa akiwa na umri mzuri wa uzee, akazikwa katika kaburi la Yoashi baba yake huko Ofra ya Waabiezeri.
33 Mara tu alipofariki Gideoni, Waisraeli wakarudia hali ya uovu na kufanya uasherati kwa kuabudu Mabaali. Wakamsimamisha Baal-Berithi kuwa mungu wao na
34 wala hawakumkumbuka Mwenyezi Mungu, Mungu wao, aliyewaokoa kutoka mikononi mwa adui zao wote kutoka kila upande.
35 Pia wakashindwa kuitendea mema jamaa ya Yerub-Baali (yaani Gideoni) kwa ajili ya mambo yote mema aliyokuwa amefanyia Israeli.
Cross-references
180
- 1Job 5:2, 2Sa 19:41, Jdg 12:1–6, Jas 4:5–6, Ecc 4:4
- 2Jas 1:19–20, Php 2:2–3, 1Co 13:4–7, Jas 3:13–18, Gal 5:14–15, Jdg 6:11, Jdg 6:34
- 3Pro 15:1, Jdg 7:24–25, Jhn 4:37, Psa 44:3, Pro 25:11, Pro 16:32, Rom 12:6, Psa 115:1
- 4Gal 6:9, 2Co 4:16, Heb 12:1–4, 1Sa 30:10, 1Sa 14:28–29, 2Co 4:8–9, Jdg 7:25, 1Sa 14:31–32
- 5Gen 33:17, Psa 60:6, 1Sa 25:18, 3Jn 1:6–8, Deu 23:4, 2Sa 17:28–29, Gen 14:18
- 61Ki 20:11, Php 2:21, Jdg 5:23, Pro 18:23, Gen 37:28, Jdg 8:15, 1Sa 25:10–11, Gen 37:25
- 7Jdg 7:15
- 8Gen 32:30–31, 1Ki 12:25
- 91Ki 22:27–28, Jdg 8:17
- 10Jdg 7:12, Jdg 20:25, Isa 9:4, Jdg 20:15, Jdg 20:2, 2Ki 3:26, Jdg 20:17, Jdg 20:35
- 11Num 32:35, Num 32:42, Jdg 18:27, 1Th 5:3, 1Sa 30:16, 1Sa 15:32
- 12Psa 83:11, Rev 6:15–16, Jos 10:22–25, Jos 10:16–18, Amo 2:14, Rev 19:19–21, Job 12:16–21, Job 34:19
- 14Jdg 1:24–25, 1Sa 30:11–15
- 15Jdg 8:6–7
- 16Pro 19:29, Pro 10:13, Jdg 8:7, Mic 7:4, Ezr 2:6
- 17Jdg 8:9, 1Ki 12:25
- 18Jdg 4:6, Jud 1:16, Psa 89:12, Psa 12:2
- 20Psa 149:9, Jos 10:24, 1Sa 15:33
- 21Psa 83:11, Jdg 8:26, Isa 3:18, 1Sa 31:5, Psa 83:1, Rev 9:6, Jdg 9:54, 1Sa 31:3
- 22Jhn 6:15, Jdg 9:8–15, 1Sa 12:12, 1Sa 8:5
- 23Isa 33:22, 1Sa 12:12, 1Sa 10:19, 2Co 1:24, Jdg 11:9–11, Jdg 10:18, Jdg 2:18, 1Pe 5:3
- 24Gen 25:13, Gen 37:28, 1Pe 3:3–5, Gen 37:25, 1Ki 20:11, 1Sa 25:11, Gen 24:22, Exo 32:3
- 26Jer 10:9, Rev 18:12, Rev 18:16, Est 8:15, Jhn 19:2, Jhn 19:5, Ezk 27:7, Rev 17:4
- 27Psa 106:39, Jdg 17:5, Deu 7:16, Jdg 18:14, Jdg 18:17, Jdg 6:24, Exo 23:33, Psa 73:27
- 28Jdg 5:31, Jdg 3:11, Jdg 3:30, Isa 10:26, Psa 83:9–12, Isa 9:4
- 291Sa 12:11, Jdg 6:32, Jdg 7:1, Neh 5:14–15
- 30Jdg 9:2, Jdg 9:5, 1Ki 11:3, Deu 17:17, 2Sa 3:2–5, Jdg 12:9, Gen 46:26, Jdg 10:4
- 31Gen 20:2, Jdg 9:1–5, Jdg 9:18, Gen 22:24, Gen 16:15
- 32Gen 25:8, Gen 15:15, Jdg 6:24, Job 42:17, Job 5:26, Jos 24:29–30, Jdg 8:27
- 33Jdg 9:4, Jdg 2:19, Jdg 9:46, Jdg 8:27, Jdg 2:17, Exo 34:15–16, 2Ch 24:17–18, Jer 3:9
- 34Psa 78:42, Psa 106:21, Psa 78:11, Psa 106:18, Jdg 3:7, Ecc 12:1, Deu 4:9, Jer 2:32
- 35Ecc 9:14–15, Jdg 9:16–19, Jdg 9:5
Topics in this chapter
49
Abiezer, Abimelech, Anger, Baal-Berith, Camel, Captive, Chains, Colors, Concubinage, Ephod, Ephraim, Flattery, Forgetting God, Forty, Gideon, Gleaning, God, Government, Ingratitude, Ishmaelites, Israel, Jealousy, Jether, Joash, Jogbehah, Jordan, Judge, Karkor, Meekness, Midianites, Ophrah, Oppression, Oreb, Patriotism, Penuel, Polygamy, Retaliation, Shechem, Shekel, Succoth, Tabor, Tact, Temptation, Theocracy, Tower, Unselfishness, Zalmunna, Zebah, Zeeb