1 Samweli 13
1 Sauli alikuwa na umri wa miaka thelathini, alipokuwa mfalme, akatawala Israeli miaka arobaini na mbili.
2 Sauli alichagua watu elfu tatu kutoka Israeli; miongoni mwa hao, watu elfu mbili walikuwa naye huko Mikmashi na katika nchi ya vilima ya Betheli; nao watu elfu moja walikuwa na Yonathani huko Gibea ya Benyamini. Watu waliosalia aliwarudisha nyumbani mwao.
3 Yonathani akashambulia ngome ya Wafilisti huko Geba, nao Wafilisti wakapata habari hizo. Kisha Sauli akaamuru tarumbeta ipigwe nchi yote na kusema, “Waebrania na wasikie!”
4 Hivyo Israeli wote wakasikia habari kwamba: “Sauli ameshambulia ngome ya Wafilisti, na sasa Israeli wamekuwa harufu mbaya kwa Wafilisti.” Basi watu waliitwa kuungana na Sauli huko Gilgali.
5 Wafilisti wakakusanyika ili kupigana na Israeli, wakiwa na magari ya vita elfu tatu, waendesha magari ya vita elfu sita, na askari wa miguu wengi kama mchanga wa ufuoni mwa bahari. Walipanda na kupiga kambi huko Mikmashi, mashariki mwa Beth-Aveni.
6 Waisraeli walipoona kuwa hali yao ni ya hatari na kuwa jeshi lao limesongwa sana, wakajificha katika mapango na katika vichaka, katika miamba, kwenye mashimo na kwenye mahandaki.
7 Hata baadhi ya Waebrania wakavuka Yordani hadi nchi ya Gadi na Gileadi. Sauli akabaki huko Gilgali, navyo vikosi vyote vilivyokuwa pamoja naye vilikuwa vikitetemeka kwa hofu.
8 Akangoja kwa siku saba, muda uliowekwa na Samweli; lakini Samweli hakuja Gilgali, nao watu wa Sauli wakaanza kutawanyika.
9 Basi akasema, “Nileteeni hapa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani.” Naye Sauli akatoa sadaka ya kuteketezwa.
10 Mara alipomaliza kutoa hiyo sadaka, Samweli akatokea, naye Sauli akaondoka kwenda kumlaki.
11 Samweli akamuuliza, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanatawanyika, na kwamba hukuja wakati uliopangwa na kwamba Wafilisti walikuwa wakikusanyika huko Mikmashi,
12 nikawaza, ‘Sasa Wafilisti watateremka dhidi yangu huko Gilgali nami sijaomba kibali kwa Mwenyezi Mungu.’ Hivyo nikalazimika kutoa sadaka ya kuteketezwa.”
13 Samweli akamwambia Sauli, “Umetenda kwa upumbavu. Hukuyashika maagizo ya Mwenyezi Mungu, Mungu wako, aliyokupa. Kama ungetii, angeudumisha ufalme wako juu ya Israeli kwa wakati wote.
14 Lakini sasa ufalme wako hautadumu; Mwenyezi Mungu amemtafuta mtu aupendezaye moyo wake, na amemchagua awe kiongozi wa watu wake, kwa sababu hukuyatii maagizo ya Mwenyezi Mungu.”
15 Kisha Samweli akaondoka Gilgali, akapanda Gibea ya Benyamini, naye Sauli akawahesabu watu aliokuwa nao. Jumla yao walikuwa watu mia sita.
16 Sauli, mwanawe Yonathani na watu waliokuwa pamoja nao walikuwa wakiishi huko Gibea ya Benyamini, wakati Wafilisti wakiwa wamepiga kambi huko Mikmashi.
17 Makundi ya wavamiaji walikuja kutoka kambi ya Wafilisti katika vikosi vitatu. Kikosi kimoja kilielekea Ofra karibu na Shuali,
18 kikosi kingine kilielekea Beth-Horoni, nacho kikosi cha tatu kilielekea kwenye nchi ya mpakani ielekeayo Bonde la Seboimu linalotazamana na jangwa.
19 Hapakuwa na mhunzi ambaye angeweza kupatikana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walikuwa wamesema, “Waebrania wasije wakatengeneza panga au mikuki!”
20 Hivyo Waisraeli wote waliteremka kwa Wafilisti ili kila mtu kunoa plau yake, jembe lake, shoka lake, au mundu wake.
21 Bei ilikuwa fedha theluthi mbili za shekeli kunoa majembe ya plau na majembe ya mkono, na theluthi moja ya shekeli kunoa uma, na shoka, na mchokoo.
22 Kwa hiyo siku ya vita hakuna askari yeyote kambini na Sauli na Yonathani aliyekuwa na upanga wala mkuki mkononi mwake; Sauli na mwanawe Yonathani tu ndio walikuwa navyo.
23 Basi kikosi cha Wafilisti kilikuwa kimetoka kuelekea njia iendayo Mikmashi.
Cross-references
122
- 1Mic 6:6, Exo 12:5
- 21Sa 10:26, 1Sa 14:31, 1Sa 13:5, 1Sa 13:23, Isa 10:28–29, 1Sa 8:11, 1Sa 14:52, Jdg 19:12
- 31Sa 10:5, Jdg 3:27, Jdg 6:34, Zec 14:10, 1Sa 14:1–6, Jos 21:17, Isa 10:29, 1Sa 13:16
- 4Gen 34:30, Exo 5:21, 1Sa 11:14–15, Zec 11:8, 1Sa 10:8, Jos 5:9, Gen 46:34
- 5Jos 11:4, 1Sa 14:23, Jos 18:12, Hos 4:15, Hos 10:5, 2Ch 1:9, Isa 48:19, Hos 5:8
- 6Jdg 6:2, Heb 11:38, 1Sa 14:11, Jdg 20:41, Isa 42:22, Jdg 10:9, Jos 8:20, Exo 14:10–12
- 7Num 32:33–42, Deu 20:8, Jos 13:24–31, Num 32:1–5, Deu 3:12, Jdg 7:3, Lev 26:17, Hos 11:10–11
- 81Sa 10:8
- 91Ki 3:4, Pro 21:27, Pro 15:8, Pro 21:3, 1Sa 13:12–13, 2Sa 24:25, 1Sa 15:21–22, 1Sa 14:18
- 101Sa 15:13, Psa 129:8, Rut 2:4
- 111Sa 13:23, 1Sa 13:5, 1Sa 13:2, 1Sa 13:16, Gen 3:13, 2Ki 5:25, Gen 4:10, 2Sa 3:24
- 121Ki 12:26–27, Amo 8:5, 2Co 9:7, Psa 66:3, 1Sa 21:7
- 131Sa 15:22, 2Ch 16:9, 1Sa 15:28, 1Sa 15:11, 2Ch 25:15–16, 1Ki 18:18, 1Ki 21:20, Psa 50:8–15
- 14Act 13:22, 1Sa 15:28, Psa 89:19–37, Psa 78:70, 1Sa 16:1, Act 7:46, 1Sa 16:12, 1Sa 2:30
- 151Sa 13:2, 1Sa 14:2, 1Sa 13:6–7
- 161Sa 13:3
- 17Jos 18:23, 1Sa 14:15, Jos 19:3, 1Sa 11:11
- 18Neh 11:34, Jos 18:13–14, Jos 16:3, 2Ch 8:5, 1Ch 6:68, Gen 14:2, Hos 11:8, Jos 16:5
- 192Ki 24:14, Jer 24:1, Jdg 5:8, Isa 54:16
- 22Jdg 5:8, 1Co 1:27–29, 1Sa 17:47, Zec 4:6, 1Sa 17:50, 2Co 4:7
- 23Isa 10:28, 1Sa 14:4–5, 1Sa 14:1, 1Sa 13:5, 2Sa 23:14, 1Sa 13:2–3
Topics in this chapter
40
Agriculture, Armies, Ax, Beth-Aven, Beth-El, Beth-Horon, Canaan, Cavalry, Cave, Chariot, Church and State, Confidence, Cowardice, David, Disobedience to God, File, Fork, Garrison, Geba, Gilgal, Goad, Israel, Jonathan, Mattock, Michmash, Minister, Christian, Ophrah, Philistines, Plow, Presumption, Quotations and Allusions, Righteous, Samuel, Saul, Seven, Shual, Smith, Trumpet, Usurpation, Zeboim