Yoshua 24
1 Ndipo Yoshua akaita pamoja makabila yote ya Israeli huko Shekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na maafisa wa Israeli, nao wakaja mbele za Mungu.
2 Yoshua akawaambia watu wote, “Hili ndilo Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Hapo zamani baba zenu, pamoja na Tera baba yake Ibrahimu na Nahori, waliishi ng’ambo ya Mto, nao waliiabudu miungu mingine.
3 Lakini nilimwondoa baba yenu Ibrahimu kutoka nchi hiyo ng’ambo ya Mto, nami nikamwongoza katika nchi yote ya Kanaani, nikampa wazao wengi. Nikampa Isaka,
4 naye Isaka nikampa Yakobo na Esau. Esau nikampa nchi ya vilima ya Seiri, lakini Yakobo pamoja na wanawe wakashuka Misri.
5 “ ‘Kisha nikawatuma Musa na Haruni, nami nikawapiga Wamisri kwa kile nilichokitenda huko, tena nikawatoa ninyi huko.
6 Nilipowatoa baba zenu Misri, mlifika kwenye bahari, nao Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari ya vita na wapanda farasi hadi Bahari ya Shamu.
7 Lakini wakamlilia Mwenyezi Mungu wakitaka msaada, naye akaweka giza kati yenu na Wamisri, akaileta bahari juu yao ikawafunika. Ninyi mliona kwa macho yenu wenyewe kile nilichowatendea Wamisri. Kisha mliishi jangwani kwa muda mrefu.
8 “ ‘Nikawaleta katika nchi ya Waamori ambao waliishi mashariki mwa Yordani. Wakapigana nanyi, lakini nikawatia mikononi mwenu. Nikawaangamiza mbele yenu nanyi mkaimiliki nchi yao.
9 Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu, alipojiandaa kupigana dhidi ya Israeli, alimwita Balaamu mwana wa Beori apate kuwalaani.
10 Lakini sikumkubali Balaamu, kwa hiyo aliwabariki tena na tena, nami niliwaokoa toka mkononi mwake.
11 “ ‘Ndipo mlipovuka Yordani mkafika Yeriko. Raia wa Yeriko wakapigana nanyi, kama walivyofanya Waamori, Waperizi, Wakanaani, Wahiti, Wagirgashi, Wahivi na Wayebusi, lakini niliwatia mikononi mwenu.
12 Nikatuma nyigu mbele yenu, ambao pia waliwafukuza mbele yenu, hao wafalme wawili wa Waamori. Siyo upanga au upinde wenu wenyewe vilivyowapatia ushindi.
13 Hivyo nikawapa ninyi nchi ambayo hamkuitaabikia, na miji ambayo hamkuijenga, na mnaishi ndani yake, na kula kutoka mashamba ya mizabibu na mizeituni msiyoipanda.’
14 “Sasa basi mcheni Mwenyezi Mungu na kumtumikia kwa uaminifu wote. Itupeni mbali miungu ambayo baba zenu waliiabudu huko ng’ambo ya Mto na huko Misri, nanyi mtumikieni Mwenyezi Mungu.
15 Lakini msipoona vyema kumtumikia Mwenyezi Mungu, chagueni hivi leo mtakayemtumikia, kama ni miungu ile baba zenu waliitumikia ng’ambo ya Frati, au miungu ya Waamori, ambao mnakaa katika nchi yao. Lakini mimi na nyumba yangu, tutamtumikia Mwenyezi Mungu.”
16 Ndipo hao watu wakajibu, “Hili jambo liwe mbali nasi la kumsahau Mwenyezi Mungu na kuitumikia miungu mingine!
17 Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, mwenyewe ndiye alitutoa sisi na baba zetu akatupandisha kutoka Misri, kutoka nchi ile ya utumwa, na kutenda zile ishara kubwa mbele ya macho yetu. Ndiye aliyetulinda katika safari yetu yote na kutokana na mataifa yote ambayo tulipita katikati yao.
18 Mwenyezi Mungu akayafukuza mbele yetu mataifa yote pamoja na Waamori, walioishi katika nchi hii. Hivyo sisi nasi tutamtumikia Mwenyezi Mungu kwa kuwa yeye ndiye Mungu wetu.”
19 Yoshua akawaambia watu, “Hamwezi kumtumikia Mwenyezi Mungu. Yeye ni Mungu Mtakatifu, ni Mungu mwenye wivu. Hatasamehe uasi wenu na dhambi zenu.
20 Ikiwa mkimwacha Mwenyezi Mungu na kuitumikia miungu migeni, atageuka na kuwaleteeni maafa na kuwaangamiza, baada ya kuwa mwema kwenu.”
21 Lakini watu wakamwambia Yoshua, “Sivyo! Sisi tutamtumikia Mwenyezi Mungu.”
22 Ndipo Yoshua akawaambia, “Ninyi mmekuwa mashahidi juu yenu wenyewe kuwa mmechagua kumtumikia Mwenyezi Mungu.” Nao wakajibu, “Ndiyo, tu mashahidi.”
23 Yoshua akawaambia, “Sasa basi, itupeni mbali hiyo miungu migeni mliyo nayo, nanyi mtoleeni Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, mioyo yenu.”
24 Nao watu wakamwambia Yoshua, “Tutamtumikia Mwenyezi Mungu, Mungu wetu, na kumtii yeye.”
25 Siku ile Yoshua akafanya agano kwa ajili ya watu na hapo Shekemu ndipo alipowaandikia amri na sheria.
26 Naye Yoshua akayaandika mambo haya katika Kitabu cha Torati ya Mungu. Ndipo akalitwaa jiwe kubwa, akalisimamisha huko chini ya mwaloni, karibu na mahali patakatifu pa Mwenyezi Mungu.
27 Yoshua akawaambia watu wote, “Tazameni! Jiwe hili litakuwa shahidi juu yetu. Limesikia maneno yote Mwenyezi Mungu aliyotuambia. Litakuwa shahidi juu yenu kama mtakuwa waongo kwa Mungu wenu.”
28 Basi Yoshua akawatuma watu kila mmoja aende katika urithi wake mwenyewe.
29 Baada ya mambo haya, Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Mwenyezi Mungu akafa akiwa na umri wa miaka mia moja na kumi.
30 Nao wakamzika katika nchi ya urithi wake, huko Timnath-Sera katika nchi ya vilima ya Efraimu, kaskazini mwa Mlima Gaashi.
31 Israeli wakamtumikia Mwenyezi Mungu siku zote za maisha ya Yoshua, na za hao wazee walioishi baada ya Yoshua kufa, ambao waliona kila kitu Mwenyezi Mungu alichowatendea Israeli.
32 Nayo ile mifupa ya Yusufu, ambayo Waisraeli waliipandisha kutoka huko Misri, wakaizika huko Shekemu kwenye eneo ambalo Yakobo alilinunua kwa wana wa Hamori baba yake Shekemu, kwa vipande mia vya fedha. Eneo hili likawa ni urithi wa uzao wa Yusufu.
33 Naye Eleazari mwana wa Haruni akafariki, akazikwa huko Gibea, mlima aliokuwa amepewa mtoto wake Finehasi, kwenye nchi ya vilima ya Efraimu.
Cross-references
217
- 1Jos 23:2, 1Sa 10:19, Gen 12:6, Act 10:33, Gen 33:18–19, Exo 18:25–26, Jdg 9:1–3, 1Ki 12:1
- 2Jos 24:15, Gen 31:30, Ezk 16:3, Deu 26:5, Gen 31:19, Isa 51:2, Gen 31:53, Gen 31:32
- 3Gen 12:1–4, Gen 21:2–3, Act 7:2–3, Gen 15:5, Neh 9:7–8, Psa 127:3
- 4Deu 2:5, Gen 36:8, Act 7:15, Gen 25:24–26, Gen 46:1–7, Psa 105:23, Gen 32:3
- 5Exo 3:10, Exo 7:1–12, Psa 135:8–9, Psa 105:26–36, Psa 136:10, Psa 78:43–51, Exo 12:37, Exo 12:51
- 6Heb 11:29, Act 7:36, Neh 9:11, Psa 77:15–20, Psa 136:13–15, Mic 6:4, Isa 63:12–13, Exo 12:37
- 7Deu 4:34, Exo 14:20, Exo 14:10, Psa 95:9–10, Exo 14:27–28, Exo 14:31, Neh 9:12–21, Deu 29:2
- 8Num 21:21–35, Jos 13:10, Neh 9:22, Deu 2:32–3:7, Psa 135:10–11, Psa 136:17–22
- 9Jdg 11:25, Mic 6:5, Num 22:2, Deu 23:4–5, Num 22:5–21
- 10Deu 23:5, Isa 54:17, Num 24:5–10, Num 22:35, Num 23:3–12, Num 22:11–12, Num 23:15–26, Num 22:18–20
- 11Jos 3:14–17, Jos 4:10–12, Exo 23:23, Deu 7:1, Act 7:45, Act 13:19, Neh 9:24–25, Jos 4:23
- 12Exo 23:28, Deu 7:20, Psa 44:3–6
- 13Deu 6:10–12, Deu 8:7, Jos 21:45, Pro 13:22, Jos 11:13
- 141Sa 12:24, Deu 10:12, Gen 35:2, Jos 24:23, 2Co 1:12, Psa 119:1, Jhn 4:23–24, Ezk 20:18
- 151Ki 18:21, Jhn 6:67–68, Rut 1:15–16, Deu 29:18, Ezk 20:39, Act 11:23, Exo 23:32–33, Jdg 6:10
- 16Heb 10:38–39, 1Sa 12:23, Rom 3:6, Rom 6:2
- 17Exo 19:4, Isa 63:7–14, Deu 32:11–12, Jos 24:5–14, Isa 46:4, Amo 2:9–10
- 18Exo 10:2, Mic 4:2, Psa 116:16, Luk 1:73–75, Zec 8:23, Exo 15:2
- 19Exo 23:21, Isa 5:16, Psa 99:9, Psa 99:5, Lev 19:2, Exo 20:5, 1Sa 6:20, Isa 6:3–5
- 20Heb 10:26–27, 1Ch 28:9, Act 7:42, Jer 17:13, Ezk 18:24, Isa 1:28, Isa 63:10, Isa 65:11–12
- 21Exo 20:19, Exo 19:8, Isa 44:5, Deu 5:27–28, Exo 24:7, Exo 24:3
- 22Psa 119:173, Psa 119:11, Luk 10:42, Job 15:6, Deu 26:17, Luk 19:22
- 23Jos 24:14, 2Co 6:16–18, 1Sa 7:3–4, Gen 35:2–4, Pro 2:2, Jdg 10:15–16, Heb 12:28–29, 1Ki 8:58
- 24Exo 24:7, Exo 24:3, Deu 5:27–29
- 252Ch 23:16, Exo 15:25, Neh 9:38, 2Ki 11:17, Jos 24:1, 2Ch 15:15, Deu 29:10–15, Deu 5:2–3
- 26Jdg 9:6, Gen 35:4, Deu 31:24–26, Jos 4:20–24, Gen 28:18–22, Gen 35:8, Exo 24:4, Jos 4:3–9
- 27Luk 19:40, Jos 22:34, Mat 10:33, Deu 31:26, Jos 22:27–28, Isa 1:2, Deu 32:1, 1Sa 7:12
- 28Jdg 2:6
- 29Jdg 2:8, Deu 34:5, Gen 50:22, Rev 14:13, Psa 115:17, 2Ti 4:7–8, Gen 50:26
- 30Jos 19:50, Jdg 2:9, 2Sa 23:30
- 31Jdg 2:7, Deu 31:13, Deu 11:2, Deu 31:29, Act 20:29, 2Ch 24:2, 2Ch 24:17–18, Deu 11:7
- 32Gen 50:25, Gen 33:19, Exo 13:19, Act 7:16, Gen 48:22, Jhn 4:5, Heb 11:22
- 33Jos 22:13, Exo 6:25, Zec 1:5, Job 30:23, Psa 49:10, Heb 9:26–27, Num 3:32, Exo 6:23
Topics in this chapter
51
Aaron, Abraham, Amorites, Animals, Backsliders, Balaam, Balak, Burial, Choice, Contingencies, Covenant, Decision, Eleazar (Eleazer), Family, Fear, Gaash, Girgashites, God, Good and Evil, Government, Grape, Hamor, Haran, Hittites, Hivites, Hornet, Isaac, Israel, Jacob, Jebusites, Jericho, Joseph, Joshua, Longevity, Moabites, Nahor, Obedience, Phinehas, Pillar, Polytheism, Prayer, Red Sea, Shechem, Sincerity, Stones, Terah, Time, Timnath-Serah, Truth, Zeal, Religious, Zippor