Waamuzi 13
1 Waisraeli wakafanya maovu tena mbele za Mwenyezi Mungu. Hivyo Mwenyezi Mungu akawatia mikononi mwa Wafilisti kwa muda wa miaka arobaini.
2 Palikuwa na mtu mmoja wa Sora, aliyeitwa Manoa, wa ukoo wa Wadani, naye alikuwa na mke aliyekuwa tasa, asiyeweza kuzaa watoto.
3 Malaika wa Mwenyezi Mungu akamtokea huyo mwanamke na kumwambia, “Wewe ni tasa na huna mtoto, lakini utachukua mimba na utamzaa mtoto wa kiume.
4 Lakini ujihadhari sana usinywe divai wala kileo kingine chochote, wala usile kitu chochote kilicho najisi,
5 kwa kuwa utachukua mimba na utamzaa mtoto wa kiume. Wembe usipite kwenye kichwa chake, kwa kuwa huyo mwana atakuwa Mnadhiri aliyetengwa kwa Mungu tangu tumboni mwa mama yake. Naye atawaongoza na kuwaokoa Waisraeli kutoka mikononi mwa Wafilisti.”
6 Ndipo huyo mwanamke akamwendea mumewe na kumwambia, “Mtu wa Mungu alinijia. Alionekana kama malaika wa Mungu, wa kutisha sana. Sikumuuliza alikotoka wala hakuniambia jina lake.
7 Lakini aliniambia, ‘Utachukua mimba na utazaa mtoto wa kiume. Basi sasa, usinywe divai wala kileo kingine chochote, wala usile kitu kilicho najisi, kwa kuwa huyo mtoto atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yake hadi kufa kwake.’ ”
8 Ndipo Manoa akamwomba Mwenyezi Mungu, akasema: “Ee Bwana, nakusihi huyo mtu wa Mungu uliyemtuma kwetu aje tena, ili atufundishe jinsi ya kumlea huyo mwana atakayezaliwa.”
9 Mungu akamsikia Manoa, naye malaika wa Mungu akamjia tena huyo mwanamke alipokuwa shambani; lakini mumewe Manoa hakuwa naye.
10 Basi yule mwanamke akaenda haraka na kumwambia mumewe, “Tazama mtu yule aliyenitokea siku ile yupo hapa!”
11 Manoa akainuka akaandamana na mkewe. Alipomfikia yule mtu akamuuliza, “Je, wewe ndiwe ulisema na mke wangu?” Akasema, “Ni mimi.”
12 Basi Manoa akamuuliza, “Maneno yako yatakapotimia, je, masharti ya maisha ya mtoto huyu yatakuwa ni yapi, na kazi yake itakuwa ni ipi?”
13 Malaika wa Mwenyezi Mungu akamjibu, “Mke wako hana budi kufanya yale yote niliyomwambia.
14 Kamwe asile kitu chochote kitakachotoka katika mzabibu, wala asinywe divai yoyote wala kileo chochote, wala asile kitu chochote kilicho najisi. Hana budi kufanya kila kitu nilichomwagiza.”
15 Manoa akamjibu yule malaika wa Mwenyezi Mungu, “Twakuomba usubiri kwanza ili tuweze kuandaa mwana-mbuzi kwa ajili yako.”
16 Malaika wa Mwenyezi Mungu akamjibu, “Hata kama utanizuia, sitakula chochote kwako. Lakini ukitaka kuandaa sadaka ya kuteketezwa, mtolee Mwenyezi Mungu.” (Manoa hakumtambua kuwa huyu alikuwa malaika wa Mwenyezi Mungu.)
17 Kisha Manoa akamuuliza yule malaika wa Mwenyezi Mungu, “Jina lako ni nani, ili tuweze kukupa heshima wakati maneno uliyonena yatakapotimia?”
18 Malaika wa Mwenyezi Mungu akamjibu, “Kwa nini unauliza jina langu? Ni jina la ajabu.”
19 Ndipo Manoa akamchukua mwana-mbuzi, pamoja na sadaka ya unga, naye akamtolea Mwenyezi Mungu dhabihu hapo juu ya mwamba. Naye yule malaika wa Mwenyezi Mungu akafanya jambo la ajabu wakati Manoa na mkewe wakiwa wanaangalia:
20 Mwali wa moto kutoka hapo madhabahuni ulipowaka kuelekea mbinguni, malaika wa Mwenyezi Mungu akapaa ndani ya huo mwali. Manoa na mkewe, kwa kuona jambo hili, wakaanguka kifudifudi.
21 Malaika wa Mwenyezi Mungu hakumtokea tena Manoa na mkewe. Ndipo Manoa akatambua kuwa huyo alikuwa malaika wa Mwenyezi Mungu.
22 Manoa akamwambia mkewe, “Hakika tutakufa, kwa kuwa tumemwona Mungu.”
23 Lakini mkewe akamwambia, “Ikiwa Mwenyezi Mungu alikuwa amekusudia kutuua, hangepokea sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya unga kutoka mikononi mwetu, wala hangetuonesha mambo haya yote wala kututangazia mambo haya wakati huu.”
24 Yule mwanamke akazaa mtoto wa kiume, akamwita jina Samsoni. Kijana akakua, naye Mwenyezi Mungu akambariki.
25 Roho wa Mwenyezi Mungu akaanza kumpa msukumo alipokuwa huko Mahane-Dani, kati ya Sora na Eshtaoli.
Cross-references
114
- 11Sa 12:9, Jdg 6:1, Rom 2:6, Jdg 3:7, Jdg 2:11, Jdg 4:1, Jdg 10:6, Jer 13:23
- 2Jos 19:41, Jos 15:33, Luk 1:7, Gen 25:21, Gen 16:1, 1Sa 1:2–6
- 3Luk 1:13, Gen 18:10, Luk 1:11, 2Ki 4:16, Jdg 2:1, Jdg 6:11–12, Jdg 13:8, 1Sa 1:20
- 4Luk 1:15, Jdg 13:14, Num 6:2–3, Jdg 13:7, Lev 11:27, Act 10:14, Lev 11:47
- 5Num 6:5, 1Sa 1:11, Num 6:2–3, 1Ch 18:1, 1Sa 7:13, 2Sa 8:1
- 6Jdg 13:17–18, Mat 28:3–4, Rev 1:17, 1Sa 9:6, Luk 9:29, Dan 8:17, Luk 1:19, Dan 10:11
- 7Jdg 13:4
- 8Act 9:6, Job 34:32, Pro 3:5–6
- 9Psa 65:2, Mat 7:7–11
- 10Jhn 4:28–29, Jhn 1:41–42
- 12Eph 6:4, Pro 22:6, Gen 18:19, Pro 4:4
- 14Jhn 2:5, Deu 12:32, Jhn 15:14, Jdg 13:4, 2Th 3:4, Jdg 13:7, Num 6:4, Mat 28:20
- 15Gen 18:3–5, Jdg 13:3, Jdg 6:18–19
- 16Jdg 13:23, Jdg 6:20, Jdg 6:26
- 17Gen 32:29
- 18Gen 32:29, Isa 9:6, Jdg 13:6
- 19Jdg 6:19–21, 1Ki 18:30–38
- 20Lev 9:24, 1Ch 21:16, 2Ki 2:11, Ezk 1:28, Mat 17:6, Heb 1:3, 1Ch 21:26, Gen 17:3
- 21Jdg 6:22, Jdg 13:16, Hos 12:4–5
- 22Gen 32:30, Deu 5:26, Jhn 1:18, Exo 33:20, Jhn 5:37, Isa 6:5, Deu 4:38, Jdg 6:22
- 231Co 12:21, Psa 25:14, Psa 86:17, Jhn 14:20, Jhn 15:15, Pro 3:32, Ecc 4:9–10, Gen 4:4–5
- 24Luk 1:80, 1Sa 3:19, Heb 11:32, Luk 2:52
- 25Jdg 3:10, Jhn 3:34, Jos 15:33, Jdg 6:34, Jdg 11:29, Jdg 18:11–12, 1Sa 11:6, Mat 4:1