Kumbukumbu La Torati 11
1 Mpende Mwenyezi Mungu, Mungu wako, na kushika masharti yake, amri zake, sheria zake na maagizo yake siku zote.
2 Kumbuka hivi leo kwamba sio watoto wako walioona na kujua adhabu ya Mwenyezi Mungu, Mungu wako: utukufu wake, mkono wake wenye nguvu, mkono wake ulionyooshwa;
3 ishara alizozifanya na mambo aliyoyafanya katikati ya Misri, kwa Farao mfalme wa Misri na kwa nchi yake yote;
4 lile alilolifanyia jeshi la Wamisri, farasi na magari yake ya vita, jinsi alivyowafurikisha na maji ya Bahari ya Shamu walipokuwa wakiwafuatilia ninyi, na jinsi Mwenyezi Mungu alivyowaletea angamizi la kudumu juu yao.
5 Sio watoto wenu walioyaona yale Mungu aliyowafanyia huko jangwani hadi mkafika mahali hapa,
6 wala lile Mungu alilowafanyia Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu wa kabila la Reubeni, wakati ardhi ilipofungua kinywa chake katikati ya Israeli yote, ikawameza pamoja na walio nyumbani mwao, mahema yao na kila kitu hai kilichokuwa mali yao.
7 Bali ni macho yenu wenyewe yaliyoyaona mambo haya yote makuu Mwenyezi Mungu aliyoyatenda.
8 Kwa hiyo fuateni maagizo yote ninayowapa leo, ili mpate kuwa na nguvu za kuingia na kuiteka nchi ambayo mnavuka Yordani kuimiliki,
9 ili mpate kuishi siku nyingi katika nchi ambayo Mwenyezi Mungu aliapa kuwapa baba zenu na wazao wao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
10 Nchi mnayoiingia kuimiliki haifanani na nchi ya Misri mlikotoka, ambako mlipanda mbegu zenu na kunyunyizia maji kwa miguu kama bustani ya mboga.
11 Lakini nchi mnayovuka Yordani kuimiliki ni nchi ya milima na mabonde inayokunywa maji ya mvua ya mbinguni.
12 Ni nchi ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anaitunza; macho ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, yanaitazama daima kutoka mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka.
13 Hivyo mkiyatii maagizo yangu ninayowapa leo kwa uaminifu, yaani kwa kumpenda Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na kumtumikia kwa moyo wako wote na kwa roho yenu yote,
14 ndipo atawanyeshea mvua katika nchi yenu kwa majira yake, mvua ya masika na ya vuli, ili mpate kuvuna nafaka zenu, divai mpya na mafuta.
15 Nitawapa majani katika malisho yako kwa ajili ya ng’ombe wenu, nanyi mtakula na kushiba.
16 Jihadharini, la sivyo mtashawishika kugeuka na kuabudu miungu mingine na kuisujudia.
17 Ndipo hasira ya Mwenyezi Mungu itawaka dhidi yenu, naye atafunga mbingu ili mvua isinyeshe nayo ardhi haitatoa mazao, nanyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo Mwenyezi Mungu anawapa.
18 Yawekeni haya maneno yangu katika mioyo yenu na akili zenu, yafungeni kama alama juu ya mikono yenu na kwenye paji za nyuso zenu.
19 Wafundisheni watoto wenu, yazungumzeni mnapoketi nyumbani na mnapotembea njiani, mnapolala na mnapoamka.
20 Yaandikeni juu ya miimo ya nyumba zenu na juu ya malango yenu,
21 ili siku zenu na siku za watoto wenu zipate kuwa nyingi katika nchi ile Mwenyezi Mungu aliyoapa kuwapa baba zenu, kama zilivyo nyingi siku za mbingu juu ya nchi.
22 Mkizingatia kwa makini maagizo haya yote ninayowapa kuyafuata, ya kumpenda Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kuenenda katika njia zake zote na kushikamana naye kwa uthabiti,
23 ndipo Mwenyezi Mungu atawafukuza mataifa haya yote mbele yako, nawe utawafukuza mataifa yaliyo makubwa na yenye nguvu kuliko wewe.
24 Kila mahali mtakapoweka mguu wenu patakuwa penu: Nchi yenu itaenea kutoka jangwa la Lebanoni, na kutoka Mto Frati hadi bahari ya magharibi.
25 Hapatakuwa na mtu atakayeweza kusimama dhidi yenu. Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kama alivyoahidi, ataweka juu ya nchi yote utisho na hofu kwa ajili yenu popote mtaenda.
26 Tazama, leo ninaweka mbele yenu baraka na laana:
27 baraka kama mtatii maagizo ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ninayowapa leo;
28 laana kama hamtatii maagizo ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na kuacha njia ninayowaamuru leo kwa kufuata miungu mingine, ambayo hamkuijua.
29 Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakapokuwa amewaleta katika nchi mnayoiingia kuimiliki, mtatangaza baraka kutoka Mlima Gerizimu, na kutangaza laana kutoka Mlima Ebali.
30 Kama mnavyofahamu, milima hii ipo ng’ambo ya Yordani, magharibi mwa barabara, kuelekea machweo ya jua, karibu na mialoni ya More, katika nchi ya wale Wakanaani wanaoishi Araba, jirani na Gilgali.
31 Karibu mvuke ng’ambo ya Yordani kuingia na kuimiliki nchi ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapa. Mtakapokuwa mmeimiliki na mnaishi humo,
32 hakikisheni kwamba mnatii amri na sheria zote ninazoziweka mbele yenu leo.
Cross-references
200
- 1Deu 6:5, Luk 1:74–75, Deu 10:12, Deu 30:16–20, Deu 6:1, Deu 4:40, Zec 3:7, Lev 8:35
- 2Deu 5:24, Act 26:22, Deu 8:19, Pro 22:19, Deu 29:10, Deu 4:34, Deu 9:26, Deu 8:2–5
- 3Deu 7:19, Psa 135:9, Deu 4:34, Psa 105:27–45, Jer 32:20–21, Psa 78:12–13
- 4Psa 106:11, Exo 15:9–10, Exo 14:23–31, Exo 15:19, Heb 11:29, Exo 15:4
- 5Psa 106:12–48, Psa 105:39–41, Psa 77:20, Psa 78:14–72
- 6Num 26:9–10, Psa 106:17, Num 16:1–35, Num 27:3
- 7Psa 145:12, Psa 150:2, Psa 145:4–6, Psa 106:2, Deu 7:19, Deu 5:3
- 8Jos 1:6–7, Eph 6:10, Php 4:13, Eph 3:16, Deu 31:23, 2Co 12:9–10, Psa 138:3, Deu 8:10–11
- 9Exo 3:8, Deu 4:40, Ezk 20:6, Deu 6:2, Deu 9:5, Deu 5:16, Pro 3:2, Deu 6:18
- 10Zec 14:18
- 11Heb 6:7, Deu 8:7–9, Psa 65:12–13, Gen 27:28, Psa 104:10–13, Isa 28:1, Jer 2:7
- 12Jer 24:6, Psa 33:18, 1Ki 9:3, Psa 34:15, Ezr 5:5
- 13Deu 10:12, Deu 4:29, Deu 6:17, Deu 11:8, Deu 6:5–6, Psa 119:4, Deu 11:22
- 14Jas 5:7, Lev 26:4, Ezk 34:26, Deu 28:12, Jol 2:22–23, Jer 14:22, Psa 65:9–13, Job 5:10–11
- 15Deu 6:11, Psa 104:14, Jol 2:19, Mal 3:10–11, Jol 2:22, Deu 8:10, Hag 1:6, Jol 1:18
- 16Heb 3:12, Job 31:27, Heb 2:1, Deu 29:18, Jas 1:26, Deu 4:23, Deu 8:19, Isa 44:20
- 171Ki 8:35, Amo 4:7, Deu 6:15, 2Ch 6:26, 1Ki 17:1, Deu 4:26, Deu 30:17–18, Deu 8:19–20
- 18Col 3:16, Deu 6:6–9, Pro 3:1, 2Pe 3:1–2, Psa 119:11, Pro 6:20–23, Exo 13:9, 2Pe 1:12
- 19Deu 6:7, Psa 34:11, Isa 38:19, Deu 4:9–10, Pro 2:1, Pro 4:1–27, Psa 78:5–6
- 20Deu 6:9
- 21Pro 3:2, Pro 4:10, Pro 9:11, Deu 4:40, Psa 72:5, Psa 89:28–29, Isa 65:20, Rev 20:6
- 22Deu 6:17, Deu 11:13, Deu 10:20, 2Co 11:2–3, Act 11:23, Deu 30:20, Gen 2:24, 2Ti 4:8
- 23Deu 4:38, Deu 9:1, Exo 34:11, Deu 9:5, Exo 23:27–30, Deu 7:22–23, Deu 7:1–2
- 24Jos 14:9, Exo 23:31, Gen 15:18–21, 1Ki 4:21, 2Ch 9:26, 1Ki 4:24, Jos 1:3–4, Num 34:3–15
- 25Deu 7:24, Jos 1:5, Exo 23:27, Deu 2:25, Jos 5:1, Jos 2:9
- 26Deu 30:15–20, Deu 30:1, Gal 3:10, Gal 3:13–14
- 27Isa 1:19, Deu 28:1–14, Isa 3:10, Luk 11:28, Lev 26:3–13, Jhn 13:17, Jhn 14:21–23, Psa 19:11
- 28Deu 28:15–68, Gal 3:10, Rom 2:8–9, Lev 26:14–32, Isa 3:11, Deu 29:19–28, Isa 1:20, Mat 25:41
- 29Jos 8:30–35, Deu 27:12–26
- 30Gen 12:6, Jdg 7:1, Jos 4:19, Jos 5:9
- 31Jos 1:11, Deu 9:1, Jos 3:13–17
- 32Deu 12:32, Mat 28:20, Deu 5:32–33, Luk 1:6, Mat 7:21–27, Jhn 15:14, 1Th 4:1–2, Psa 119:6
Topics in this chapter
48
Abiram, Arm, Benedictions, Blessing, Canaan, Champaign, Chastisement, Children, Commandments, Contingencies, Dathan, Diligence, Door, Duty, Ebal, Egypt, Eliab, Euphrates, Family, Frontlets, Gerizim, God, Heart, Idolatry, Instruction, Irrigation, Israel, Korah, Law, Lebanon, Legends (Inscriptions), Love, Mediterranean Sea, Miracles, Moreh, Obedience, Obligation, Parents, Phylactery, Prayer, Rain, Reading, Red Sea, Reward, School, Watchfulness, Wicked (People), Word of God