Kumbukumbu La Torati 14
1 Ninyi ni watoto wa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
2 kwa kuwa ninyi ni taifa takatifu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Mwenyezi Mungu amewachagua ninyi kuwa taifa lake la pekee kutoka mataifa yote duniani.
3 Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
4 Hawa ndio wanyama mtakaokula: ng’ombe, kondoo, mbuzi,
5 kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
7 Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu.
8 Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
9 Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
10 Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
11 Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
12 Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
13 kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
14 kunguru wa aina yoyote,
15 mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
16 bundi, mumbi, bundi mkubwa,
17 mwari, nderi, mnandi,
18 korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
19 Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
20 Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
21 Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
22 Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
23 Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ng’ombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili mpate kujifunza kumheshimu Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, daima.
24 Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Mwenyezi Mungu atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
25 basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, atakapopachagua.
26 Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ng’ombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na watu wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na kufurahi.
27 Msiache kuwajali Walawi wanaoishi katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
28 Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
29 ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.
Cross-references
95
- 1Rom 9:8, Lev 21:5, Gal 3:26, Rom 9:26, Hos 1:10, Rom 8:16, Heb 2:10, Jer 41:5
- 2Deu 7:6, Lev 20:26, Exo 19:5–6, 1Pe 2:9, Deu 26:18–19, Lev 19:2, Tit 2:14, Deu 28:9
- 3Ezk 4:14, Lev 20:25, Lev 11:43, Rom 14:14, 1Co 10:28, Act 10:12–14, Tit 1:15, Isa 65:4
- 41Ki 4:23, Lev 11:2–45, Act 10:14
- 6Pro 18:1, 2Co 6:17, Psa 1:1–2
- 72Pe 2:18–22, Mat 7:26, Mat 7:22–23, 2Ti 3:5, Tit 1:16, Lev 11:5
- 8Lev 11:26–27, Isa 66:3, Isa 66:17, Isa 65:4, Luk 15:15–16, 2Pe 2:22
- 9Lev 11:9–12
- 12Lev 11:13–19
- 15Job 30:29
- 19Lev 11:20–23, Php 3:19
- 21Exo 23:19, Exo 34:26, Lev 22:8, Rom 12:2, Deu 14:2, Dan 12:7, Lev 19:33–34, Act 15:20
- 22Deu 12:6, Neh 10:37, Num 18:21, Deu 26:12–15, Deu 12:17, Lev 27:30–33
- 23Deu 12:5–7, Deu 12:17–18, Deu 4:10, Deu 15:19–20
- 24Deu 12:21, Deu 12:5, Deu 11:24, Exo 23:31
- 26Ecc 9:7, Deu 12:20–21, Deu 26:11, Mat 21:12, 1Co 6:12–13, Psa 106:14, Deu 12:7, Deu 12:15
- 27Deu 14:29, Num 18:20, Deu 12:12, 1Ti 5:17, Deu 18:1–2, Deu 12:18–19, Gal 6:6
- 28Deu 14:22, Deu 26:12–15, Amo 4:4
- 29Deu 15:10, Deu 14:27, Pro 19:17, Deu 24:19–21, Deu 16:11, Mal 3:10–11, Psa 41:1, Deu 16:14
Topics in this chapter
61
Adoption, Aliens, Alms, Animals, Baldness, Bat, Birds, Chamois, Character, Children, Coney, Cooking, Cormorant, Creeping Things, Cuckoo, Cud, Cutting, Deer, Eagle, Falcon, Family, Fear, Fish, Glede, Goat, God, Hare, Hawk, Heron, Holiness, Hoof, Idolatry, Insects, Kite, Lapwing, Levites, Liberality, Milk, Minister, Christian, Money, Mourning, Night Hawk, Orphan, Osprey, Ossifrage, Ostriches, Owl, Pelican, Poor, Priest, Pygarg, Raven, Sanitation, Strangers, Swan, Swine, Tithes, Unclean, Vulture, Widow, Wine