Kumbukumbu La Torati 31
1 Kisha Musa akaenda akasema maneno haya kwa Waisraeli wote:
2 “Sasa nina miaka mia moja na ishirini nami siwezi tena kuwaongoza. Mwenyezi Mungu ameniambia, ‘Hutavuka Yordani.’
3 Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, yeye mwenyewe atavuka mbele yenu. Ataangamiza mataifa haya mbele yenu, nanyi mtaimiliki nchi yao. Pia Yoshua atavuka mbele yenu, kama Mwenyezi Mungu alivyosema.
4 Naye Mwenyezi Mungu atawafanyia watu hao kile alichowafanyia Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, ambao aliwaangamiza pamoja na nchi yao.
5 Mwenyezi Mungu atawakabidhi kwenu, nanyi lazima mkawatendee yale yote niliyowaamuru.
6 Kuweni imara na moyo wa ushujaa. Msiogope wala msifadhaike kwa sababu yao, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anaenda pamoja nanyi; kamwe hatawaacha wala hatawatupa ninyi.”
7 Kisha Musa akamwita Yoshua na akamwambia mbele ya Israeli wote, “Uwe imara na moyo wa ushujaa, kwa kuwa ni lazima uende na watu hawa katika nchi ile Mwenyezi Mungu aliyowaapia baba zao kuwapa, nawe ni lazima uwagawie kama urithi wao.
8 Mwenyezi Mungu mwenyewe atakutangulia naye atakuwa pamoja nawe; kamwe hatakuacha wala hatakutupa. Usiogope, wala usifadhaike.”
9 Kwa hiyo Musa akaandika sheria hii na kuwapa makuhani, wana wa Lawi, waliochukua Sanduku la Agano la Mwenyezi Mungu na wazee wote wa Israeli.
10 Kisha Musa akawaamuru, akasema: “Mwishoni mwa kila miaka saba, katika mwaka wa kufuta madeni, wakati wa Sikukuu ya Vibanda,
11 Waisraeli wote wanapokuja mbele za Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, mahali atakapopachagua, utasoma sheria hii mbele yao masikioni mwao.
12 Kusanya watu wote, wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, ili waweze kusikia na kujifunza kumcha Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, na kuzingatia maneno yote ya sheria hii.
13 Watoto wao, ambao hawaijui sheria hii, lazima waisikie na kujifunza kumcha Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, kwa muda mtakaoishi katika nchi mnayovuka Yordani kuimiliki.”
14 Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Sasa siku ya kifo chako imekaribia. Mwite Yoshua, mkajihudhurishe katika Hema la Kukutania, mahali nitakapompa maagizo ya kazi.” Kwa hiyo Musa na Yoshua wakaja na kujihudhurisha kwenye Hema la Kukutania.
15 Kisha Mwenyezi Mungu akatokea katika Hema katika nguzo ya wingu, nalo wingu likasimama juu ya ingilio la Hema.
16 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa: “Unaenda kupumzika na baba zako, nao watu hawa hivi karibuni watazini na miungu migeni ya nchi wanayoingia. Wataniacha na kuvunja agano nililofanya nao.
17 Siku hiyo nitawakasirikia na kuwaacha; nitawaficha uso wangu, nao wataangamizwa. Maafa mengi na shida nyingi zitakuja juu yao, nao siku hiyo watauliza, ‘Je, maafa haya hayakuja juu yetu kwa sababu Mungu wetu hayuko pamoja nasi?’
18 Nami hakika nitauficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya maovu yao yote kwa kugeukia miungu mingine.
19 “Sasa ujiandikie wimbo huu, uwafundishe Waisraeli na uwaamuru wauimbe, ili upate kuwa ushahidi wangu dhidi yao.
20 Nitakapokwisha kuwaingiza katika nchi inayotiririka maziwa na asali, nchi niliyowaahidi baba zao kwa kiapo, nao watakapokula wakashiba na kufanikiwa, watageukia miungu mingine na kuiabudu, wakinikataa mimi na kuvunja agano langu.
21 Maafa na shida zitakapokuja juu yao, wimbo huu utashuhudia dhidi yao, kwa sababu hautasahauliwa na wazao wao. Ninajua lile wanaloandaa kufanya, hata kabla sijawaingiza katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo.”
22 Hivyo Musa akaandika wimbo huu siku ile na akawafundisha Waisraeli.
23 Mwenyezi Mungu akampa Yoshua mwana wa Nuni agizo hili: “Uwe hodari na shujaa, kwa kuwa utawaleta Waisraeli katika nchi niliyowaahidi kwa kiapo, nami mwenyewe nitakuwa pamoja nawe.”
24 Baada ya Musa kumaliza kuandika kwenye kitabu maneno ya sheria hii kutoka mwanzo hadi mwisho,
25 akawapa Walawi wale waliolibeba Sanduku la Agano la Mwenyezi Mungu agizo hili, akawaambia:
26 “Chukueni Kitabu hiki cha Torati mkakiweke kando ya Sanduku la Agano la Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Hapo ndipo kitakapokaa kama shahidi dhidi yenu.
27 Kwa kuwa ninajua jinsi mlivyo waasi na mlivyo na shingo ngumu. Kama mmekuwa mkiasi dhidi ya Mwenyezi Mungu nikiwa bado niko hai na nikiwa pamoja nanyi, mtaasi mara ngapi baada ya kufa kwangu!
28 Kusanyeni mbele yangu wazee wote wa makabila yenu na maafisa wenu wote, ili nipate kusema maneno haya masikioni mwao na kuziita mbingu na nchi ili kushuhudia dhidi yao.
29 Kwa kuwa ninajua, baada ya kifo changu hakika mtakuwa waovu kabisa na kugeuka kutoka njia niliyowaamuru ninyi. Katika siku zijazo, maafa yatawapata, kwa sababu mtafanya maovu mbele za macho ya Mwenyezi Mungu, na kuchochea hasira yake kwa kazi za mikono yenu.”
30 Musa akayasoma maneno ya wimbo huu kutoka mwanzo hadi mwisho katika masikio ya kusanyiko lote la Israeli:
Cross-references
184
- 2Deu 34:7, Num 27:17, 1Ki 3:7, Num 20:12, Exo 7:7, Deu 3:26–27, Jos 14:10–11, 2Sa 21:17
- 3Deu 9:3, Deu 31:23, Deu 3:28, Jos 4:14, Deu 31:7–8, Num 27:18–21, Gen 48:21, Deu 31:14
- 4Deu 3:3–11, Deu 2:33, Deu 3:21, Exo 23:28–31, Num 21:24–35, Deu 7:16, Deu 7:2
- 5Deu 7:2, Deu 20:16–17, Exo 23:32–33, Num 33:52–56, Deu 7:18, Exo 34:12–16, Deu 7:23–25
- 6Jos 1:9, Eph 6:10, Psa 27:14, 1Ch 28:20, Isa 41:10, Luk 12:32, 2Ti 2:1, Psa 27:1
- 7Deu 3:28, Deu 31:6, Deu 1:38, Eph 6:10, Jos 1:6, Deu 31:23, Dan 10:19, Deu 31:3
- 8Exo 33:14, Deu 31:6, Jos 1:9, Rom 8:31, Jos 1:5, Isa 43:1–2, Exo 13:21–22, 1Ch 28:20
- 9Num 4:15, Jos 3:3, Jhn 1:17, Dan 9:13, Jhn 5:46, Deu 31:22–26, Deu 17:18, Jos 3:14–17
- 10Deu 15:1–2, Lev 23:34–43
- 112Ki 23:2, Jos 8:34–35, Deu 16:16–17, Deu 12:5, Exo 34:24, Neh 8:1–8, Exo 23:16–17, Neh 9:3
- 12Deu 4:10, Deu 6:6–7, Psa 19:7–11, Psa 34:11–14, Ezr 10:1, 2Ti 3:15–17, Deu 29:29, Jhn 5:39
- 13Deu 11:2, Deu 6:7, Pro 22:6, Psa 78:4–8, Eph 6:4
- 14Num 27:13, Deu 31:23, Jud 1:24, Ecc 9:5, 2Ti 4:1–4, 1Sa 10:19, Job 2:1, Deu 31:2
- 15Exo 33:9–10, Psa 99:7, Exo 40:38
- 16Jdg 10:6, Jdg 10:13, Jdg 2:12, Exo 34:15, Ezk 16:15, Rev 19:2, Deu 32:15, Jer 2:11–13
- 17Psa 104:29, 2Ch 15:2, Isa 8:17, Jdg 6:13, Num 14:42, Deu 29:24–27, Psa 30:7, 1Ch 28:9
- 18Deu 31:16–17
- 19Deu 6:7, Deu 31:21–22, Deu 31:26, Deu 4:9–10, Jhn 12:48, Deu 11:19, 2Sa 14:3, Deu 31:30–32:45
- 20Hos 13:6, Deu 6:10–12, Neh 9:25–26, Exo 3:8, Ezk 34:16, Ezk 34:20, Jer 5:28, Neh 9:35
- 21Hos 5:3, Gen 6:5, Jhn 2:24–25, Psa 139:2, Amo 5:25–26, Gen 8:21, Hos 13:5–6, Isa 46:10
- 22Deu 31:19, Deu 31:9
- 23Deu 31:7–8, Deu 31:14, Act 7:45, Deu 3:28, Jos 1:5–9, Deu 31:3
- 24Deu 31:9, Deu 17:18
- 25Deu 31:9
- 26Deu 31:19, 2Ch 34:14–15, 2Ki 22:13–19, 2Ki 22:8–11, 1Ki 8:9, Gal 2:19, Rom 3:19–20
- 27Deu 32:20, Deu 9:24, 2Ch 30:8, Exo 32:8–9, Isa 48:4, Act 7:51, Deu 9:6–7, Psa 78:8
- 28Deu 4:26, Deu 32:1, Deu 30:19, Luk 19:40, Deu 29:10, Gen 49:1–2, Num 11:16–17, Isa 1:2
- 29Jdg 2:19, Deu 32:5, Luk 19:42–44, Luk 21:24, Hos 9:9, Isa 1:4, Deu 4:30, Gen 49:1
- 30Jhn 12:49, Heb 3:2, Deu 4:5, Heb 3:5, Act 20:27
Topics in this chapter
46
Afflictions and Adversities, Ark, Backsliders, Call, Canaanites, Children, Cloud, Courage, Death, Faith, Fear, Fellowship, God, Government, Heart, Holy Spirit, Idolatry, Ingratitude, Instruction, Israel, Joshua, Law, Longevity, Minister, Christian, Moab, Moses, Og, Priest, Prosperity, Quotations and Allusions, Reprobacy, Reproof, Riches, Sabbatic Year, School, Secret, Self-Will, Sin, Tabernacle, Tabernacles, Feast of, War, Whoredom, Wicked (People), Women, Word of God, Worship