Yoshua 1
1 Baada ya kifo cha Musa mtumishi wa Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu akamwambia Yoshua mwana wa Nuni, msaidizi wa Musa:
2 “Mtumishi wangu Musa amekufa. Sasa basi, wewe na watu wote hawa jiandaeni kuvuka Mto Yordani kuingia nchi nitakayowapa Waisraeli karibuni.
3 Kila mahali nyayo za miguu yenu zitakapokanyaga nimewapa, kama vile nilivyomwahidi Musa.
4 Nchi yenu itaenea kuanzia jangwa hili hadi Lebanoni, tena kuanzia mto mkubwa wa Frati, yaani nchi yote ya Wahiti, hadi Bahari ile Kubwa iliyo upande wa magharibi.
5 Hakuna mtu yeyote atakayeweza kushindana na wewe siku zote za maisha yako. Kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe, sitakuacha wala sitakupungukia.
6 “Uwe hodari na shujaa, kwa sababu wewe ndiwe utawaongoza watu hawa kuirithi nchi niliyowaapia baba zao kuwapa.
7 Uwe hodari na uwe na ushujaa mwingi. Uwe na bidii kutii sheria yote aliyokupa Musa mtumishi wangu; usiiache kwa kugeuka kuelekea kuume au kushoto, ili upate kufanikiwa popote utakapoenda.
8 Usiache Kitabu hiki cha Torati kiondoke kinywani mwako; yatafakari maneno yake usiku na mchana, ili upate kuwa mwangalifu kufanya kila kitu sawasawa na yote yaliyoandikwa ndani yake. Ndipo utakapofanikiwa na kisha utastawi.
9 Je, si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na shujaa. Usihofu wala usivunjike moyo, kwa kuwa Mwenyezi Mungu, Mungu wako, atakuwa pamoja nawe popote utakapoenda.”
10 Ndipo Yoshua akawaagiza maafisa wa watu akisema,
11 “Pitieni katika kambi yote mkawaambie watu, ‘Tayarisheni vyakula vyenu. Siku tatu kuanzia sasa mtavuka Yordani ili kuingia na kuimiliki nchi ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapa iwe yenu.’ ”
12 Lakini kwa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase, Yoshua akasema,
13 “Kumbukeni agizo lile Musa mtumishi wa Mwenyezi Mungu alilowapa: ‘Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapa ninyi utulivu kwa kuwapa nchi hii.’
14 Wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu watakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa mashariki mwa Yordani, lakini wapiganaji wenu wote, wakiwa wamejiandaa kwa vita, lazima wavuke mbele ya ndugu zenu. Imewapasa kuwasaidia ndugu zenu,
15 hadi Mwenyezi Mungu awape nao utulivu, kama alivyowatendea ninyi, hadi wao pia watakapokuwa wamemiliki nchi ile Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anayowapa. Baada ya hilo, mwaweza kurudi na kuimiliki nchi yenu wenyewe, ambayo Musa mtumishi wa Mwenyezi Mungu aliwapa mashariki mwa Yordani kuelekea linakochomoza jua.”
16 Ndipo wakamjibu Yoshua, “Chochote ambacho umetuagiza tutafanya na popote utakapotutuma tutaenda.
17 Kama vile tulivyomtii Musa kikamilifu, ndivyo tutakavyokutii wewe. Mwenyezi Mungu, Mungu wako, na awe pamoja nawe tu kama vile alivyokuwa pamoja na Musa.
18 Yeyote atakayeasi neno lako na kuacha kuyatii maneno yako, au chochote utakachowaamuru, atauawa. Uwe imara na hodari tu!”
Cross-references
109
- 1Deu 34:9, Deu 31:23, Deu 1:38, Deu 31:3, Exo 24:13, Deu 34:5, 2Ki 5:25–27, Jos 12:6
- 2Deu 3:28, Deu 31:7, Num 27:16–21, Jos 1:11, Jos 1:1, Heb 7:23–24, Heb 3:5–6, Isa 42:1
- 3Deu 11:24, Jos 14:9, Tit 1:2
- 4Exo 23:31, Gen 15:18–21, Num 34:2–18, Deu 3:25, Deu 11:24, Deu 1:7, 1Ch 5:9, 1Ch 18:3
- 5Rom 8:31, Deu 31:6–8, Mat 28:20, Isa 41:10–14, Jos 1:9, Act 18:9–10, Deu 20:4, 2Ti 4:17
- 6Dan 10:19, Eph 6:10, Jos 1:9, Jos 1:7, 1Ch 22:13, 1Co 16:13, 1Ch 28:10, 2Ti 2:1
- 71Ch 22:13, Deu 5:32, Jos 1:8, Pro 4:27, Jos 11:15, Deu 12:32, Deu 29:9, Deu 28:14
- 8Psa 119:15, Psa 19:14, Col 3:16, Pro 3:1, Deu 29:9, Jhn 14:21, Luk 11:28, Deu 6:6–9
- 9Gen 28:15, Jer 1:7–8, Psa 27:1–2, Jos 1:6–7, Deu 20:1, Psa 46:7, Deu 31:7–8, Isa 43:1
- 11Deu 9:1, 2Ki 20:5, Hos 6:2, Jos 3:2, Deu 11:31, Exo 19:11
- 12Num 32:20–22
- 13Num 32:20–28, Deu 3:18–20, Jos 22:1–4
- 14Exo 13:18, Deu 20:8, Rev 17:4
- 15Php 2:4, Num 32:17–22, Jos 22:4–9, 1Co 13:5, Gal 5:13, 1Co 12:26, Php 1:21–26, Gal 6:2
- 16Tit 3:1, 1Pe 2:13–15, Deu 5:27, Rom 13:1–5, Num 32:25
- 17Jos 1:5, 1Ki 1:37, Jos 1:9, Psa 20:4, 1Ch 28:20, Psa 20:1, Psa 118:25–26, 1Sa 20:13
- 18Eph 6:10, Jos 1:9, 1Co 16:13, Ezr 10:4, Heb 12:25, Heb 10:28–29, 1Sa 11:12, Luk 19:27