1 Samweli 31
1 Basi Wafilisti wakapigana na Israeli. Waisraeli wakawakimbia, na wengi wakauawa katika Mlima Gilboa.
2 Wafilisti wakawafuatilia Sauli na wanawe kwa karibu, na wakawaua Yonathani, Abinadabu, na Malki-Shua.
3 Mapigano yakawa makali sana dhidi ya Sauli, nao wapiga upinde wakampata na kumjeruhi vibaya.
4 Sauli akamwambia mbeba silaha wake, “Futa upanga wako unichome nao, la sivyo hawa watu wasiotahiriwa watakuja wanichome na kunidhalilisha.” Lakini mbeba silaha wake akaogopa sana wala hakuweza kufanya hivyo. Kwa hiyo Sauli akachukua upanga wake mwenyewe, akauangukia.
5 Mbeba silaha wake alipoona Sauli amekufa, pia akaangukia upanga wake, akafa pamoja naye.
6 Basi Sauli, wanawe watatu, mbeba silaha wake na watu wake wote wakafa pamoja siku ile ile.
7 Waisraeli waliokuwa kando ya bonde na wale waliokuwa ng’ambo ya Yordani walipoona kuwa jeshi la Waisraeli limekimbia na kwamba Sauli na wanawe wamekufa, wakaacha miji yao na kukimbia. Nao Wafilisti wakaenda na kukaa humo.
8 Kesho yake Wafilisti walipokuja kuwavua maiti silaha, walimkuta Sauli na wanawe watatu wameanguka katika Mlima Gilboa.
9 Wakamkata Sauli kichwa na kumvua silaha zake, nao wakatuma wajumbe katika nchi yote ya Wafilisti kutangaza habari katika hekalu la sanamu zao na miongoni mwa watu wao.
10 Wakaweka silaha zake katika hekalu la Maashtorethi, na kukifunga kiwiliwili chake katika ukuta wa Beth-Shani.
11 Watu wa Yabesh-Gileadi waliposikia yale Wafilisti waliyomfanyia Sauli,
12 mashujaa wao wote wakaenda usiku hadi Beth-Shani. Wakauchukua mwili wa Sauli na miili ya wanawe kutoka ukuta wa Beth-Shani na kurudi hadi Yabeshi, ambapo waliiteketeza miili kwa moto.
13 Kisha wakachukua mifupa yao na kuizika chini ya mti wa mkwaju huko Yabeshi, nao wakafunga kwa siku saba.
Cross-references
68
- 11Ch 10:1–12, 1Sa 28:4, 2Sa 1:21, 1Sa 29:1, 1Sa 28:15, 1Sa 12:25, 1Sa 28:1
- 21Ch 8:33, 1Sa 14:49, 1Sa 23:17, Exo 20:5, 1Sa 18:1–4, 1Sa 13:16, 2Sa 1:6, 1Sa 13:2
- 32Sa 1:6, Gen 49:23, 1Ki 22:34, 2Sa 1:4, Amo 2:14
- 42Sa 1:6, Jdg 9:54, 2Sa 1:9–10, 2Sa 1:20, 2Sa 17:23, 2Sa 1:14, 1Ki 16:27, Jdg 14:3
- 51Ch 10:5
- 61Sa 4:10–11, 1Sa 11:15, Hos 13:10–11, 1Ch 10:6, 1Sa 12:17, 1Sa 28:19, 1Sa 12:25, Ecc 9:1–2
- 7Jdg 6:2, 1Sa 13:6, Lev 26:36, Deu 28:33, Lev 26:32
- 81Ch 10:8, 2Ch 20:25
- 92Sa 1:20, Jdg 16:23–24, 1Sa 17:51, 1Sa 17:54, 1Sa 31:4, 1Ch 10:9–10
- 10Jos 17:11, Jdg 2:13, 1Sa 21:9, Jdg 1:27, 2Sa 21:12–14, 1Sa 7:3
- 112Sa 2:4, 1Sa 11:1–11
- 122Ch 16:14, Jer 34:5, 2Sa 2:4–7, Amo 6:10
- 13Gen 50:10, 2Sa 21:12–14, 2Sa 1:12, 1Sa 22:6, Gen 35:8, 2Sa 2:4–5