1 Petro 5
1 Kwa wazee walio miongoni mwenu, nawasihi mimi nikiwa mzee mwenzenu, shahidi wa mateso ya Al-Masihi, na mshiriki katika utukufu utakaofunuliwa:
2 lichungeni kundi la Mungu mlilokabidhiwa, mkitumika kama waangalizi, si kwa kulazimishwa bali kwa hiari, kama Mungu anavyowataka mwe; si kwa tamaa ya fedha, bali mlio na bidii katika kutumika.
3 Msijifanye mabwana juu ya wale walio chini ya uangalizi wenu, bali kuweni vielelezo kwa hilo kundi.
4 Naye Mchungaji Mkuu atakapodhihirishwa, mtapokea taji la utukufu lisiloharibika.
5 Vivyo hivyo, ninyi mlio vijana watiini wazee. Nanyi nyote jivikeni unyenyekevu kila mtu kwa mwenzake, kwa kuwa, “Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”
6 Basi, nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake.
7 Mtwikeni yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye anajishughulisha sana na mambo yenu.
8 Mwe na kiasi na kukesha, maana adui yenu ibilisi huzungukazunguka kama simba angurumaye akitafuta mtu ili apate kummeza.
9 Mpingeni, mkiwa thabiti katika imani, mkijua kwamba mateso kama hayo yanawapata ndugu zenu pote duniani.
10 Nanyi baada ya kuteswa kwa kitambo kidogo, Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele ndani ya Al-Masihi, yeye mwenyewe atawarejesha na kuwatia nguvu, akiwaimarisha na kuwathibitisha.
11 Uweza una yeye milele na milele. Amen.
12 Kwa msaada wa Silvano, ninayemhesabu kuwa ndugu mwaminifu, nimewaandikia waraka huu mfupi ili kuwatia moyo, na kushuhudia kwamba hii ni neema halisi ya Mungu. Simameni imara katika neema hiyo.
13 Kundi la waumini lililoko Babeli, lililochaguliwa pamoja nanyi, wanawasalimu; vivyo hivyo mwanangu Marko anawasalimu.
14 Salimianeni kwa busu la upendo. Amani iwe nanyi nyote mlio katika Al-Masihi.
Cross-references
106
- 1Luk 24:48, Col 3:3–4, Rom 8:17–18, 2Jn 1:1–15, Psa 73:24–25, Rev 1:9, 1Pe 5:4, 1Jn 3:2
- 2Tit 1:7, 1Ti 3:8, Tit 3:1, Act 20:26–28, 1Ti 3:3, 1Co 9:7, Ezk 34:2–3, Mal 1:10
- 32Th 3:9, Ezk 34:4, Php 3:17, Mat 20:25–26, 2Co 1:24, 1Ti 4:12, Tit 2:7, Mrk 10:42–45
- 4Jas 1:12, 1Co 9:25, Isa 40:11, 2Ti 4:8, 1Jn 3:2, Psa 23:1, Rev 2:10, Rev 3:11
- 5Jas 4:6, Pro 3:34, Eph 5:21, Rom 12:10, Php 2:3, Col 3:12, Isa 66:2, Rom 13:14
- 6Jas 4:10, Luk 14:11, Pro 29:23, Mat 23:12, Luk 18:14, Luk 1:52, 2Ch 32:26, 2Ch 12:12
- 7Psa 55:22, Php 4:6, Psa 37:5, Psa 56:3–4, Mat 6:25–26, Mat 6:33–34, Heb 13:5–6, Psa 34:15
- 8Eph 6:11, Jas 4:7, Eph 4:27, Job 2:2, 1Pe 1:13, 1Pe 4:7, 1Jn 3:8–10, 1Th 5:6–8
- 9Jas 4:7, Act 14:22, Eph 6:11–13, 1Pe 2:21, 1Co 10:13, Eph 6:16, 1Ti 6:12, 2Ti 3:12
- 102Co 4:17, 2Th 3:3, 1Pe 1:6–7, Jud 1:24, Psa 138:7, 1Ti 6:12, 2Th 2:17, Rom 8:28–30
- 111Pe 4:11, Rom 11:36, Rev 1:6, Rev 5:13
- 12Heb 13:22, Act 11:23, 2Co 1:19, 1Co 15:1, Act 20:24, 1Th 1:1, 2Th 1:1, Rom 5:2
- 13Act 12:12, Act 12:25, Rev 18:2, Psa 87:4, Rev 17:5, 2Jn 1:13
- 14Rom 16:16, Eph 6:23, Rom 8:1, 1Co 16:20, Rom 1:7, 1Th 5:26, 2Co 13:12, Jhn 14:27
Topics in this chapter
42
Afflictions and Adversities, Babylon, Benedictions, Call, Care, Character, Church, Commandments, Covetousness, Crown, Decision, Elder, Election, Example, Glory, God, Gospel, Grace of God, Humility, Intercession, Jesus, the Christ, Kiss, Lion, Mark, Minister, Christian, Perfection, Perseverance, Praise, Pride, Quotations and Allusions, Righteous, Sacrilege, Satan, Shepherd, Silas, Sobriety, Suffering, Temptation, Testimony, Trouble, War, Watchfulness