Isaya 12
1 Katika siku ile utasema: “Nitakusifu wewe, Ee Mwenyezi Mungu. Ingawa ulinikasirikia, hasira yako imegeukia mbali nawe umenifariji.
2 Hakika Mungu ni wokovu wangu; nitamtumaini wala sitaogopa. Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu, ni nguvu zangu na wimbo wangu; amekuwa wokovu wangu.”
3 Kwa furaha mtachota maji kutoka visima vya wokovu.
4 Katika siku hiyo mtasema: “Mshukuruni Mwenyezi Mungu, mliitie jina lake; julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya, tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5 Mwimbieni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ametenda mambo makuu, hili na lijulikane duniani kote.
6 Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni, kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
Cross-references
48
- 1Psa 30:5, Isa 25:1, Isa 54:8, Zec 14:9, Isa 40:1–2, Hos 6:1, Isa 27:1–3, Isa 35:10
- 2Exo 15:2, Psa 118:14, Psa 27:1, Rev 7:10, Isa 26:3–4, Jon 2:9, Isa 45:17, Mat 1:21–23
- 3Rev 22:1, Rev 22:17, Jer 2:13, Jhn 4:10–14, Rev 7:17, Isa 55:1–3, Jhn 7:37–39, Isa 49:10
- 4Psa 105:1, Psa 145:4–6, 1Ch 29:11, Jhn 17:26, Psa 117:1–2, Php 2:9–11, Jer 51:9–10, Exo 33:19
- 5Exo 15:1, Psa 98:1, Hab 2:14, Exo 15:21, Rev 15:3, Rev 19:1–3, Isa 40:9, Psa 105:2
- 6Zec 2:5, Zec 2:10–11, Zep 3:14–17, Psa 9:11, Isa 41:14, Luk 19:37–40, Ezk 48:35, Isa 54:1