Kutoka 24
1 Kisha Mungu akamwambia Musa, “Njooni huku juu kwa Mwenyezi Mungu, wewe na Haruni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli. Mniabudu kwa mbali,
2 lakini Musa peke yake ndiye atakayemkaribia Mwenyezi Mungu; wengine wasije karibu. Nao watu wasije wakapanda pamoja naye.”
3 Musa alipoenda na kuwaambia watu maneno yote na sheria zote za Mwenyezi Mungu, wakaitikia kwa sauti moja, “Kila kitu alichosema Mwenyezi Mungu tutakifanya.”
4 Ndipo Musa akaandika kila kitu Mwenyezi Mungu alichokuwa amesema. Akaamka kesho yake asubuhi na mapema na kujenga madhabahu chini ya mlima na kusimamisha nguzo kumi na mbili za mawe kuwakilisha makabila kumi na mawili ya Israeli.
5 Kisha akawatuma vijana wanaume Waisraeli, nao wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu za mafahali wachanga kuwa sadaka za amani kwa Mwenyezi Mungu.
6 Musa akachukua nusu ya damu ya wale wanyama na kuiweka kwenye mabakuli, na nusu nyingine akainyunyiza juu ya madhabahu.
7 Kisha akachukua kile Kitabu cha Agano na kuwasomea watu. Nao wakajibu, “Tutafanya kila kitu alichosema Mwenyezi Mungu, nasi tutatii.”
8 Ndipo Musa akachukua ile damu, akawanyunyizia wale watu, akasema, “Hii ni damu ya agano ambalo Mwenyezi Mungu amelifanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.”
9 Musa na Haruni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli wakapanda mlimani,
10 nao wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa na kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, iliyo safi kama anga angavu.
11 Lakini Mungu hakuinua mkono wake dhidi ya hawa viongozi wa Waisraeli; walimwona Mungu, nao wakala na kunywa.
12 Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Panda uje kwangu huku mlimani na ukae hapa, nami nitakupa vibao vya mawe, vyenye sheria na amri ambazo nimeziandika ziwe mwongozo wao.”
13 Basi Musa akaondoka na Yoshua mtumishi wake, naye Musa akapanda juu kwenye mlima wa Mungu.
14 Musa akawaambia wazee wa Israeli, “Tungojeni hapa hadi tutakapowarudia. Haruni na Huri wako pamoja nanyi, na kila aliye na shauri aweza kuwaendea wao.”
15 Musa alipopanda juu mlimani, wingu liliufunika huo mlima,
16 nao utukufu wa Mwenyezi Mungu ukatua juu ya Mlima Sinai. Kwa muda wa siku sita wingu lilifunika mlima, na siku ya saba Mwenyezi Mungu akamwita Musa kutoka kati ya lile wingu.
17 Kwa Waisraeli utukufu wa Mwenyezi Mungu ulionekana kama moto uteketezao juu ya mlima.
18 Kisha Musa akaingia ndani ya lile wingu alivyokuwa akipanda mlimani. Naye akakaa huko mlimani kwa muda wa siku arobaini, usiku na mchana.
Cross-references
125
- 1Num 11:16, Exo 6:23, Lev 10:1–2, Exo 28:1, Exo 19:24, Exo 3:5, Exo 19:20, Exo 1:5
- 2Exo 24:18, Exo 24:15, Exo 24:13, Heb 10:21–22, Num 16:5, Heb 9:24, Jer 49:19, Jer 30:21
- 3Exo 19:8, Exo 24:7, Jos 24:22, Deu 6:1, Deu 5:1, Deu 4:1, Deu 4:45, Deu 5:27–28
- 4Deu 31:9, Gen 28:18, Jos 4:8–9, Luk 22:30, Gal 2:9, Rev 21:14, Gen 28:22, Gen 31:45
- 5Exo 18:12, Exo 19:22, Lev 3:1–17, Lev 7:11–21, Lev 1:1–17
- 61Pe 1:19, Exo 24:8, Heb 9:18, Lev 4:6, Lev 3:8, Exo 29:20, Exo 12:22, 1Pe 1:2
- 7Deu 31:11–13, Exo 24:3–4, Heb 9:18–23, Jer 7:23–24, Act 13:15, Col 4:16, 1Th 5:27
- 8Heb 10:4–5, Exo 24:6, Ezk 36:25, Mat 26:28, 1Co 11:25, Heb 13:20, Heb 9:18–21, 1Pe 1:2
- 9Exo 24:1
- 10Jhn 1:18, Ezk 10:1, Exo 33:20, Exo 33:23, Gen 32:30, 1Ti 6:16, Rev 4:3, Ezk 1:26–28
- 11Exo 18:12, Luk 15:23–24, Gen 31:54, Gen 16:13, 1Co 10:16–18, Exo 19:21, Deu 12:7, Ecc 9:7
- 12Deu 5:22, Exo 31:18, Exo 32:15–16, Heb 9:4, Jer 31:33, 2Co 3:3, Exo 24:15, 2Co 3:7
- 13Num 11:28, Exo 33:11, Exo 3:1, Exo 17:9–14, Exo 32:17
- 14Exo 17:12, Exo 17:10, Gen 22:5, 1Sa 13:8–13, Exo 32:1, 1Sa 10:8, Exo 18:25–26
- 15Exo 19:9, Mat 17:5, Exo 19:16, 2Ch 6:1
- 16Exo 16:10, Num 16:42, Ezk 1:28, Lev 9:23, Exo 24:17, Exo 20:10, Exo 19:11, Num 14:10
- 17Heb 12:29, Deu 4:24, Deu 4:36, Exo 3:2, Heb 12:18, Exo 19:18, Hab 3:4–5, Ezk 1:27
- 18Deu 9:9, Exo 34:28, Deu 10:10, Deu 9:25, Deu 9:18, Exo 9:33, Mrk 1:13, Exo 24:17
Topics in this chapter
38
Aaron, Abihu, Altar, Atonement, Blood, Cloud, Colors, Covenant, Decalogue, Decision, Fasting, Forty, God, Government, Hur, Instability, Israel, Joshua, Law, Miracles, Nadab, Obedience, Peace Offerings, Pillar, Prophets, Purification, Quotations and Allusions, Revelation, Seventy, Sinai, Stones, Symbols and Similitudes, Table, Theocracy, Vision, Word of God, Worship, Young Men