Amosi 3
1 Sikilizeni neno hili alilosema Mwenyezi Mungu dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
2 “Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
3 Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
4 Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
5 Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati hakuna chochote cha kunasa?
6 Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji unapopatwa na maafa, je, si Mwenyezi Mungu amesababisha?
7 Hakika Bwana Mungu Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
8 Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mungu Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
9 Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
10 Mwenyezi Mungu asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
11 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mungu Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
12 Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wanaokaa Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
13 “Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, yeye Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni.
14 “Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
15 Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Mwenyezi Mungu.
Cross-references
107
- 1Amo 2:10, Mic 3:1, Jer 8:3, 2Ch 20:15, Ezk 37:16–17, Hos 4:1, Isa 48:12, Jer 31:1
- 2Deu 7:6, Exo 19:5–6, Deu 10:15, 1Pe 4:17, Zec 14:17–18, Deu 32:9, Jer 14:10, Jer 9:25
- 32Co 6:14–16, Gen 17:1, Gen 5:22, Gen 6:9
- 4Hos 11:10, Psa 104:21, Amo 1:2, Hos 5:14, Amo 3:8
- 5Ecc 9:12, Dan 9:14, Jer 31:28
- 6Isa 45:7, Isa 14:24–27, Zep 1:16, Gen 50:20, 2Co 5:11, Jer 10:7, Jer 4:5, Jer 6:1
- 7Jhn 15:15, Gen 18:17, Psa 25:14, Rev 1:1, Dan 9:22–27, Gen 6:13, Rev 4:1, Dan 10:21
- 8Act 4:20, Jer 20:9, Amo 3:4, Amo 1:2, Amo 7:12–17, Rev 5:5, Amo 2:12, 1Co 9:16
- 9Amo 4:1, Amo 6:1, Amo 1:8, 1Sa 5:1, Jer 22:8–9, Amo 8:6, Jer 50:2, Jer 31:5
- 10Zep 1:9, Jer 4:22, Zec 5:3–4, Psa 14:4, Amo 6:12, Jer 5:4, Hab 2:8–11, Amo 5:7
- 112Ki 18:9–11, Amo 2:5, Amo 6:14, 2Ki 15:19, 2Ki 17:3–6, Isa 10:5–6, Isa 8:7–8, Hos 11:5–6
- 121Sa 17:34–37, Rom 11:4–5, Isa 31:4, 1Ki 20:30, 2Ki 16:9, 1Ki 20:34, Amo 9:2–3, 1Ki 22:25
- 132Ch 24:19, Eph 4:17, Deu 30:18–19, Amo 5:27, Act 2:40, Ezk 2:7, Jos 22:22, Act 18:5–6
- 142Ki 23:15, Hos 10:5–8, 2Ch 34:6–7, Hos 10:14–15, Amo 5:5–6, Mic 1:6–7, 2Ch 31:1, Amo 9:1
- 151Ki 22:39, Jer 36:22, Amo 6:11, Isa 5:9, Jdg 3:20, Psa 45:8, Amo 3:11
Topics in this chapter
32
Afflictions and Adversities, Ashdod, Beth-El, Communion, Damascus, Dishonesty, Fellowship, Friendship, Gin, God, House, Hunting, Idolatry, Ingratitude, Israel, Prophecies Concerning, Ivory, Judgment, Lion, Meekness, Mysteries, Palace, Prophets, Rulers, Secret, Shepherd, Sin, Snare, Summer, Trumpet, War, Wicked (People), Winter