Wimbo Ulio Bora 7
1 Ee binti ya mwana wa mfalme, tazama jinsi inavyopendeza miguu yako katika viatu! Miguu yako yenye madaha ni kama vito vya thamani, kazi ya mikono ya fundi stadi.
2 Kitovu chako ni kama bilauri ya mviringo ambayo kamwe haikosi divai iliyochanganywa. Kiuno chako ni kichuguu cha ngano kilichozungukwa kwa yungiyungi.
3 Matiti yako ni kama wana-paa wawili, mapacha wa paa.
4 Shingo yako ni kama mnara wa pembe ya ndovu. Macho yako ni vidimbwi vya Heshboni karibu na lango la Beth-Rabi. Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni ukitazama kuelekea Dameski.
5 Kichwa chako kinakuvika taji kama Mlima Karmeli. Nywele zako ni kama zulia la urujuani; mfalme ametekwa na mashungi yake.
6 Tazama jinsi ulivyo mzuri na unavyopendeza, ee pendo, kwa uzuri wako!
7 Umbo lako ni kama la mtende, nayo matiti yako kama vishada vya matunda.
8 Nilisema, “Nitakwea mtende, nami nitayashika matunda yake.” Matiti yako na yawe kama vishada vya mzabibu, harufu nzuri ya pumzi yako kama matofaa,
9 na kinywa chako kama divai bora kuliko zote. Mpendwa Divai na iende moja kwa moja hadi kwa mpenzi wangu, ikitiririka polepole juu ya midomo na meno.
10 Mimi ni mali ya mpenzi wangu, nayo shauku yake ni juu yangu.
11 Njoo, mpenzi wangu, twende mashambani, twende tukalale huko vijijini.
12 Hebu na twende mapema katika mashamba ya mizabibu tuone kama mizabibu imechipua, kama maua yake yamefunguka, na kama mikomamanga imetoa maua: huko nitakupa penzi langu.
13 Mitunguja hutoa harufu zake nzuri, kwenye milango yetu kuna matunda mazuri, mapya na ya zamani, ambayo nimekuhifadhia wewe, mpenzi wangu.
Cross-references
90
- 1Psa 45:13, Php 1:27, Eph 4:15–16, 2Co 6:18, Exo 35:35, Dan 2:32, Luk 15:22, Col 2:19
- 2Sng 5:14, Rom 7:4, Jer 1:5, Isa 46:3, Pro 3:8, Psa 45:16
- 3Sng 4:5, Sng 6:6
- 4Sng 4:4, Psa 144:12, Sng 4:8–9, 1Ki 10:22, Gen 15:2, Heb 5:14, 1Ki 9:19, Eph 3:18–19
- 5Isa 35:2, Sng 4:1, Mat 28:20, Sng 1:17, Psa 68:24, Mic 7:14, Eph 4:15–16, Eph 1:22
- 6Sng 4:10, Psa 45:11, Sng 1:15–16, Isa 62:4–5, Sng 7:10, Sng 4:7, Sng 2:14, Zep 3:17
- 7Sng 4:5, Psa 92:12, Sng 1:13, Eph 4:13, Eph 3:17, Isa 66:10, Sng 7:3, Sng 8:8
- 82Co 2:14, Jhn 14:21–23, Sng 1:3, Sng 2:3, Sng 2:5, Sng 4:16–5:1, Jer 32:41
- 9Sng 5:16, Col 3:16–17, Isa 62:8–9, Pro 16:24, Act 2:11–13, Act 4:31–32, Zec 9:15–17, Sng 2:14
- 10Psa 45:11, Sng 2:16, Sng 6:3, Gal 2:20, Sng 7:5–6, Psa 147:11, Job 14:15, Jhn 17:24
- 11Sng 2:10–13, Sng 4:8, Sng 1:4
- 12Sng 6:11, 1Th 3:5–6, 2Co 13:5, Sng 7:6, Eph 6:24, Sng 4:16, Heb 4:16, Psa 122:5
- 13Gen 30:14, Mat 13:52, Php 1:11, Sng 4:13, Isa 23:18, 1Co 8:8–9, 1Pe 4:11, Sng 4:16–5:1