Wimbo Ulio Bora 5
1 Nimekuja kwenye bustani yangu, dada yangu, bibi arusi wangu; nimekusanya manemane yangu pamoja na manukato yangu. Nimekula sega langu la asali na asali yangu; nimekunywa divai yangu na maziwa yangu. Rafiki Kuleni, enyi rafiki, mnywe; kunyweni ya kutosha, ee wapenzi.
2 Nililala lakini moyo wangu ulikuwa macho. Sikiliza! Mpenzi wangu anabisha: “Nifungulie, dada yangu, mpendwa wangu, hua wangu, usiye na hitilafu. Kichwa changu kimeloa umande, na nywele zangu manyunyu ya usiku.”
3 Nimevua joho langu: je, ni lazima nivae tena? Nimenawa miguu yangu: je, ni lazima niichafue tena?
4 Mpenzi wangu aliweka mkono wake kwenye tundu la komeo; moyo wangu ulianza kugonga kwa ajili yake.
5 Niliinuka kumfungulia mpenzi wangu, mikono yangu ikidondosha manemane, vidole vyangu vikitiririka manemane, penye vipini vya komeo.
6 Nilimfungulia mpenzi wangu, lakini mpenzi wangu alishaondoka; alikuwa ameenda zake. Moyo wangu ulishuka kwa kuondoka kwake. Nilimtafuta lakini sikumpata. Nilimwita lakini hakunijibu.
7 Walinzi walinikuta walipokuwa wakifanya zamu za ulinzi mjini. Walinipiga, wakanijeruhi, wakaninyang’anya joho langu, hao walinzi wa kuta!
8 Enyi binti za Yerusalemu, ninawaagiza: mkimpata mpenzi wangu, mtamwambia nini? Mwambieni ninazimia kwa mapenzi.
9 Je, mpenzi wako ni bora kuliko wengine namna gani, wewe uliye mzuri kupita wanawake wote? Je, mpenzi wako ni mzuri kuliko wengine, namna gani, hata unatuagiza hivyo?
10 Mpenzi wangu anang’aa, tena ni mwekundu, wa kuvutia miongoni mwa wanaume kumi elfu.
11 Kichwa chake ni dhahabu safi kuliko zote, nywele zake ni za mawimbi na ni nyeusi kama kunguru.
12 Macho yake ni kama ya hua kandokando ya vijito vya maji, aliyeogeshwa kwenye maziwa, yaliyopangwa kama vito vya thamani.
13 Mashavu yake ni kama matuta ya mimea ya manukato. Midomo yake ni kama yungiyungi inayodondosha manemane.
14 Mikono yake ni fimbo za dhahabu iliyopambwa kwa krisolitho. Mwili wake ni kama pembe ya ndovu iliyong’arishwa iliyopambwa na yakuti samawi.
15 Miguu yake ni nguzo za marumaru zilizosimikwa katika vitako vya dhahabu safi. Sura yake ni kama Lebanoni, bora kama miti yake ya mierezi.
16 Kinywa chake chenyewe ni utamu, kwa ujumla yeye ni wa kupendeza. Huyu ndiye mpenzi wangu, huyu ndiye rafiki yangu, ee binti za Yerusalemu.
Cross-references
120
- 1Sng 6:2, Sng 4:16, Rev 22:17, Sng 4:9–14, Sng 8:13, Isa 55:1–2, Pro 9:5, Isa 58:11
- 2Rev 3:20, Sng 2:14, Zec 4:1, Sng 6:9, Psa 119:1, Psa 24:7–10, Sng 4:9, Gen 31:40–41
- 3Luk 11:7, Pro 13:4, Pro 3:28, Mat 25:5, Mat 26:38–43, Pro 22:13, Rom 7:22–23
- 4Act 16:14, Php 2:13, 2Co 8:1–2, Gen 43:30, Sng 1:4, Psa 110:3, 2Co 8:16, 1Ki 3:26
- 5Sng 5:13, Eph 3:17, Sng 3:6, Sng 5:2, 2Co 7:9–11, 2Co 7:7, Rev 3:20, Luk 12:36
- 6Sng 5:2, Rev 3:19, Hos 5:15, Psa 80:4, Sng 6:1, Psa 28:1, Luk 22:61–62, Lam 3:8
- 7Sng 3:3, Act 5:40–41, Mat 23:29–36, 2Co 11:13, Isa 6:10–11, Mat 21:33–41, Mat 23:2, Heb 12:2
- 8Sng 2:7, Sng 2:5, Psa 42:1–3, Sng 3:5, Psa 119:81–83, Rom 15:30, Gal 6:1–2, Psa 63:1–3
- 9Sng 1:8, Sng 6:1, Sng 6:9–10, Psa 87:3, Mat 16:13–17, Isa 53:2, Psa 45:13, Jhn 1:14
- 10Psa 45:2, Php 2:9–11, Psa 45:17, Sng 2:1, 1Sa 16:12, Heb 2:10, Deu 32:31, Heb 7:26
- 11Sng 5:2, Dan 7:9, Sng 7:5, Eph 1:21–22, Rev 1:14, Dan 2:37–38
- 12Sng 1:15, Sng 4:1, Heb 4:13
- 13Sng 1:10, Sng 6:2, Sng 2:1, Psa 45:2, Sng 3:6, Sng 4:11, Isa 50:6, Luk 4:22
- 14Exo 24:10, Isa 54:11, Sng 7:2, Psa 99:4, Ezk 1:16, Exo 15:6, Exo 28:20, Isa 52:13
- 151Ki 4:33, Rev 1:15–16, Hos 14:7, Exo 26:19, Mat 17:2, Act 2:28, Sng 2:14, Zec 9:17
- 16Psa 45:2, Sng 7:9, Sng 2:3, Jas 2:23, Hos 3:1, Psa 119:103, Jas 4:4, Gal 2:20