1 Samweli 17
1 Wakati huo Wafilisti wakakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita, nao wakakusanyika huko Soko katika Yuda. Wakapiga kambi huko Efes-Damimu, kati ya Soko na Azeka.
2 Sauli na Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde la Ela na kupanga jeshi ili kupigana vita na Wafilisti.
3 Wafilisti wakawa katika kilima kimoja, na Waisraeli katika kilima kingine, nalo bonde likiwa kati yao.
4 Shujaa aliyeitwa Goliathi, aliyetoka Gathi, akajitokeza kutoka kambi ya Wafilisti. Alikuwa na urefu dhiraa sita na shibiri moja.
5 Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya shaba kifuani mwake yenye uzito wa shekeli elfu tano.
6 Miguuni mwake alivaa mabamba ya shaba, na alikuwa na mkuki wa shaba mgongoni mwake.
7 Mpini wa huo mkuki ulikuwa kama mti wa mfumaji, na ncha ya chuma yake ilikuwa na uzito wa shekeli mia sita. Mbeba ngao wake alitangulia mbele yake.
8 Goliathi alisimama na kuwaambia majeshi ya Israeli kwa sauti kuu, akisema, “Kwa nini mmetoka kupanga vita? Je, mimi si Mfilisti, na ninyi ni watumishi wa Sauli? Chagueni mtu na anishukie mimi.
9 Kama anaweza kupigana nami na kuniua, tutakuwa chini yenu; lakini nikimshinda na kumuua, ninyi mtakuwa chini yetu, na mtatutumikia.”
10 Kisha yule Mfilisti akasema, “Siku hii ya leo nayatukana majeshi ya Israeli! Nipeni mtu tupigane.”
11 Kwa kusikia maneno ya Wafilisti, Sauli na Waisraeli wote wakafadhaika na kuogopa.
12 Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefrathi jina lake Yese aliyekuwa ametoka Bethlehemu ya Yuda. Yese alikuwa na wana wanane, naye wakati wa Sauli alikuwa mzee sana.
13 Wana wakubwa watatu wa Yese walikuwa wamefuatana na Sauli vitani: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Eliabu, wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama.
14 Daudi ndiye alikuwa mdogo wa wote. Hao wakubwa watatu wakamfuata Sauli,
15 lakini Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili kuchunga kondoo wa baba yake huko Bethlehemu.
16 Kwa siku arobaini huyo Mfilisti alikuwa akija mbele kila siku asubuhi na jioni na kujionesha.
17 Wakati huo Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Chukua hii efa ya bisi na hii mikate kumi kwa ajili ya ndugu zako uwapelekee upesi kambini mwao.
18 Chukua pamoja na hizi jibini kumi kwa jemadari wa kikosi chao. Ujue hali ya ndugu zako na uniletee taarifa za uhakika kutoka kwao.
19 Wao wako pamoja na Sauli na wanaume wote wa Israeli huko kwenye Bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.”
20 Asubuhi na mapema Daudi akaondoka, akaliacha kundi la kondoo pamoja na mchungaji, akapakia vitu vile na kuondoka, kama vile Yese alivyokuwa amemwagiza. Akafika kambini wakati jeshi lilikuwa likitoka kwenda kwenye sehemu yake ya kupigania, huku wakipiga ukelele wa vita.
21 Israeli na Wafilisti walikuwa wakipanga safu zao wakitazamana.
22 Daudi akaacha vile vitu vyake kwa mtunza vifaa, akakimbilia katika safu za vita na kuwasalimu ndugu zake.
23 Alipokuwa akisema nao, Goliathi, yule Mfilisti shujaa kutoka Gathi, akajitokeza mbele ya safu zake na kupiga ile kelele yake ya kawaida ya matukano, naye Daudi akayasikia.
24 Waisraeli walipomwona yule mtu, wote wakamkimbia kwa woga mkuu.
25 Basi Waisraeli walikuwa wakisema, “Je, mnaona jinsi mtu huyu anavyoendelea kujitokeza. Hujitokeza ili kutukana Israeli. Mfalme atatoa utajiri mwingi kwa yule mtu atakayemuua. Pia atamwoza binti yake na atasamehe jamaa ya baba yake kulipa kodi katika Israeli.”
26 Daudi akauliza watu waliokuwa wamesimama karibu naye, “Je, atatendewa nini mtu atakayemuua huyu Mfilisti na kuondoa aibu hii katika Israeli? Ni nani huyu Mfilisti asiyetahiriwa hata atukane majeshi ya Mungu aliye hai?”
27 Wakarudia yale yaliyokuwa yamesemwa na kumwambia kuwa, “Hili ndilo atakalotendewa mtu yule atakayemuua.”
28 Eliabu nduguye mkubwa Daudi alipomsikia akizungumza na watu hasira ikawaka juu yake akamuuliza, “Kwa nini umeteremka kuja hapa? Nao wale kondoo wachache kule nyikani umewaacha na nani? Ninajua jinsi ulivyo na kiburi na jinsi moyo wako ulivyo mwovu; umekuja hapa kutazama vita tu.”
29 Daudi akasema, “Sasa nimefanya nini? Je, siwezi hata kuongea.”
30 Daudi akamgeukia mtu mwingine na kumuuliza jambo lilo hilo, nao watu wakamjibu vilevile kama mwanzo.
31 Lile Daudi alilosema likasikiwa na kuelezwa kwa Sauli, naye Sauli akatuma aitwe.
32 Daudi akamwambia Sauli, “Mtu yeyote asife moyo kwa habari ya huyu Mfilisti; mtumishi wako ataenda kupigana naye.”
33 Sauli akamjibu Daudi, “Wewe hutaweza kwenda kupigana dhidi ya huyu Mfilisti; wewe ni kijana tu, naye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
34 Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako amekuwa akichunga kondoo wa baba yake. Simba au dubu alipokuja na kuchukua kondoo kutoka kundi,
35 nilifuatia, nikampiga na nikampokonya kondoo kwenye kinywa chake. Aliponigeukia, nilimkamata nywele zake, nikampiga na kumuua.
36 Mtumishi wako ameshaua simba na dubu pia; huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa sababu ameyatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
37 Mwenyezi Mungu ambaye aliniokoa toka katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa kutoka mikono ya huyu Mfilisti.” Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, naye Mwenyezi Mungu na awe pamoja nawe.”
38 Ndipo Sauli akamvika Daudi silaha zake mwenyewe za vita. Akamvika dirii na chapeo ya shaba kichwani mwake.
39 Daudi akajifunga upanga juu ya hayo mavazi na kujaribu kutembea kwa sababu alikuwa hana uzoefu navyo. Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda nikiwa nimevaa hivi, kwa sababu sina uzoefu navyo.” Hivyo akavivua.
40 Kisha akachukua fimbo yake mkononi, akachagua mawe laini matano katika kijito, akayaweka kwenye kifuko ndani ya mfuko wake wa kichungaji, akiwa na kombeo yake mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
41 Wakati ule ule, yule Mfilisti, akiwa na mbeba ngao wake mbele yake, akaendelea kujongea karibu na Daudi.
42 Mfilisti akamwangalia Daudi kote na kumwona kuwa ni kijana tu, mwekundu na mzuri wa kupendeza, naye akamdharau.
43 Akamwambia Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata unanijia na fimbo?” Yule Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
44 Tena Mfilisti akamwambia, “Njoo hapa, nami nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni nyama yako.”
45 Daudi akamwambia yule Mfilisti. “Wewe unanijia na upanga, mkuki na fumo, lakini mimi ninakujia kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, Mungu wa majeshi ya Israeli, ambaye wewe umemtukana.
46 Siku hii Mwenyezi Mungu atakutia mkononi mwangu, nami nitakupiga na kukukata kichwa chako. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya jeshi la Wafilisti, nayo dunia yote itajua kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Wale wote waliokusanyika hapa watajua kuwa Mwenyezi Mungu haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; kwa kuwa vita ni vya Mwenyezi Mungu, naye atawatia ninyi wote mikononi mwetu.”
48 Yule Mfilisti aliposogea karibu ili kumshambulia, Daudi akaenda mbio kuelekea safu ya vita kukutana naye.
49 Daudi akatia mkono wake mfukoni na kuchukua jiwe, akalirusha kwa kombeo, nalo likampiga yule Mfilisti kwenye paji la uso. Lile jiwe likaingia kipajini mwa uso, akaanguka kifudifudi.
50 Basi Daudi akamshinda huyo Mfilisti kwa kombeo na jiwe; bila kuwa na upanga mkononi mwake akampiga huyo Mfilisti na kumuua.
51 Daudi akakimbia na kusimama juu yake. Akaushika upanga wa huyo Mfilisti na kuuvuta toka kwenye ala yake. Baada ya kumuua, akakata kichwa chake kwa ule upanga. Wafilisti walipoona kuwa shujaa wao amekufa, wakageuka na kukimbia.
52 Ndipo wanaume wa Israeli na Yuda wakainuka kwenda mbele wakipiga kelele na kufuatia Wafilisti hadi kwenye ingilio la Gathi kwenye malango ya Ekroni. Maiti zao zilitawanyika kando ya barabara ya Shaaraimu hadi Gathi na Ekroni.
53 Waisraeli waliporudi kutoka kuwafukuza Wafilisti, waliteka nyara kutoka kambi yao.
54 Daudi akachukua kichwa cha yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu, naye akaweka silaha za huyo Mfilisti katika hema lake mwenyewe.
55 Sauli alipomwona Daudi anaenda kukabiliana na huyo Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, “Abneri, yule kijana ni mwana wa nani?” Abneri akajibu, “Hakika kama uishivyo, ee mfalme, mimi sifahamu.”
56 Mfalme akasema, “Uliza huyu kijana ni mwana wa nani.”
57 Mara Daudi aliporudi kutoka kumuua huyo Mfilisti, Abneri akamchukua na kumleta mbele ya Sauli. Daudi alikuwa bado anakishikilia kichwa cha yule Mfilisti.
58 Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akasema, “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese wa Bethlehemu.”
Cross-references
252
- 1Jos 15:35, 1Sa 13:5, 2Ch 28:18, 1Ch 11:13, Jos 10:10–11, Jdg 3:3, Jer 34:7, 2Ch 11:7
- 21Sa 21:9, 1Sa 17:19
- 4Jos 11:22, 1Sa 17:23, 1Ch 20:4–8, 2Sa 21:16–22, 1Ch 11:23, 1Sa 27:4, 1Sa 21:9–10, Deu 3:11
- 61Sa 17:45, 1Ki 10:16, 2Ch 9:15
- 72Sa 21:19, 1Ch 11:23, 1Sa 17:41, 1Ch 20:5
- 81Sa 8:17, 1Sa 17:26, 2Sa 11:11, 1Ch 21:3
- 91Sa 11:1
- 101Sa 17:25–26, 1Sa 17:45, 1Sa 17:36, 2Sa 21:21, Neh 2:19, Num 23:7–8, Psa 9:4–5, Job 40:9–12
- 11Jos 1:9, Deu 31:8, Pro 28:1, Psa 27:1, Isa 57:11, Isa 51:12–13
- 12Gen 35:19, 1Sa 16:10–11, 1Sa 16:18, 1Ch 2:13–16, 1Sa 17:58, Rut 4:22, Luk 3:31–32, Mat 1:6
- 131Ch 2:13, 2Sa 13:32, 1Sa 17:28, 1Sa 16:6–9, 2Sa 13:3, 2Sa 21:21
- 141Sa 16:11, Gen 25:23
- 151Sa 16:11, 1Sa 16:19–23
- 16Mat 4:2, Luk 4:2
- 171Sa 25:18, Rut 2:14, Luk 11:13, 2Sa 17:28, Mat 7:11
- 18Gen 37:14, 1Sa 16:20, 2Sa 17:29, 1Th 3:5–6, Act 15:36, Job 10:10
- 201Sa 26:5, Luk 19:43, 1Sa 17:28, Eph 6:1–2, 1Sa 26:7
- 22Luk 10:5–6, Gen 37:14, Mat 10:12–13, Jdg 18:15, Isa 10:28
- 231Sa 17:8–10
- 24Isa 7:2, Isa 30:17, Deu 32:30, Lev 26:36, Num 13:33, 1Sa 17:11, 1Sa 13:6–7
- 25Jos 15:16, Rev 2:7, Rev 3:12, Rev 3:5, Rev 3:21, Mat 17:26, Rev 2:17, 1Sa 18:17–27
- 26Deu 5:26, 1Sa 11:2, 1Sa 17:10, 1Sa 17:36, 1Sa 14:6, 2Ki 19:4, Psa 44:13, Dan 9:16
- 271Sa 17:25
- 28Mat 10:36, Pro 18:19, Gen 37:11, Gen 37:4, Gen 37:8, Mrk 3:21, 1Sa 16:13, Jud 1:10
- 291Pe 3:9, 1Co 2:15, Pro 15:1, Act 11:2–4
- 301Sa 17:26–27
- 31Pro 22:29
- 32Deu 20:1–3, 1Sa 16:18, Psa 3:6, Isa 35:4, Psa 27:1–3, Num 14:9, 1Sa 14:6, Heb 12:12
- 33Num 13:31, Deu 9:2, Rev 13:4, 1Sa 17:42, 1Sa 17:56, Psa 11:1
- 352Ti 4:17–18, Amo 3:12, Dan 6:22, Jdg 14:5–6, Psa 91:13, Act 28:4–6, 2Sa 23:20
- 361Sa 17:10, Isa 36:8–10, Ezk 32:19, Isa 36:15, Act 12:1–2, Zec 12:3, 1Sa 17:26, Rom 2:28–29
- 372Ti 4:17–18, Psa 138:7–8, 2Co 1:9–10, Psa 18:16–17, Psa 63:7, 1Ch 22:11, 1Sa 20:13, 1Sa 7:12
- 392Co 10:4–5, Zec 4:6, Hos 1:7
- 401Co 1:27–29, Jdg 20:16, Jdg 15:15–16, Mat 10:10, Jdg 3:31, Jdg 7:16–20
- 421Sa 16:12, 1Sa 17:33, Psa 123:3–4, Pro 16:18, 2Co 11:27–29, Neh 4:2–4, 1Ki 20:18, 2Ki 18:23–24
- 431Sa 24:14, 2Sa 3:8, 2Sa 9:8, 2Sa 16:9, 2Ki 8:13, Gen 27:29, Pro 26:2, Num 22:6
- 44Ezk 28:9–10, Pro 18:12, 1Ki 20:10–11, Jer 9:23, 1Sa 17:46, Ecc 9:11–12, Ezk 28:2, Ezk 39:17–20
- 452Co 10:4, 2Ch 32:8, 2Co 3:5, Php 4:13, Psa 18:2, Psa 124:8–125:1, 2Sa 22:33–35, 1Sa 17:36
- 46Isa 52:10, Jos 4:24, 2Ki 19:19, 1Ki 8:43, Deu 28:26, Dan 6:26–27, Rev 19:17–18, Dan 2:47
- 47Psa 44:6–7, Zec 4:6, Hos 1:7, Pro 21:30–31, 1Sa 14:6, 2Ch 20:15–17, 2Ch 14:11, Rom 8:31
- 48Pro 28:1, Psa 27:1
- 491Co 1:27–28, 2Ki 9:24, 1Ki 22:34
- 50Jdg 15:15, 1Sa 21:9, 1Sa 23:21, 1Sa 17:39, Jdg 3:31, 1Sa 13:22
- 511Sa 21:9, Heb 11:34, 2Sa 23:21, Psa 7:15–16, Est 7:10, Heb 2:14
- 52Jos 15:11, Jdg 7:23, Jos 15:45–46, 1Sa 14:21–22, Jos 15:33–36, 2Sa 23:10
- 53Jer 4:20, Jer 30:16, 2Ki 7:7–16
- 54Exo 16:33, 1Sa 21:9, Jos 4:7–8
- 551Sa 16:21–22, 1Sa 17:58
- 571Sa 17:54
- 581Sa 17:12, 1Sa 16:18–19
Topics in this chapter
61
Abinadab, Abner, Armies, Armor-Bearer, Azekah, Battle, Beam, Bethlehem, Boasting, Brass, Bread, Captain, Championship, Cheese, Coat of Mail, Corn, Courage, Cowardice, Daughter, David, Decision, Dog (Sodomite?), Doubting, Elah, Eliab, Ephes-Dammin, Faith, Food, Gath, God, Goliath, Greaves, Heart, Helmet, Iron, Israel, Javelin, Jesse, Lion, Mail, Marriage, Measure, Meekness, Pas-Dammim, Philistines, Rising, Sarcasm, Saul, Shaaraim, Shammah, Shekel, Shepherd, Sling, Socoh, Spear, Suffering, Target, Trophies, Uncharitableness, War, Zeal, Religious