1 Yohana 2
1 Watoto wangu wapendwa, nawaandikia haya ili msitende dhambi. Lakini mtu yeyote akitenda dhambi, tunaye Mwombezi kwa Baba: ndiye Isa Al-Masihi, Mwenye Haki.
2 Yeye ndiye dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu, wala si kwa ajili ya dhambi zetu tu, bali pia kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote.
3 Basi katika hili twajua ya kuwa tumemjua, tukizishika amri zake.
4 Mtu yeyote asemaye kuwa, “Ninamjua,” lakini hazishiki amri zake, ni mwongo, wala ndani ya mtu huyo hamna kweli.
5 Lakini mtu yeyote anayelitii neno lake, upendo wa Mungu umekamilika ndani yake kweli kweli. Katika hili twajua kuwa tumo ndani yake:
6 Yeyote anayesema anakaa ndani yake hana budi kuenenda kama Isa alivyoenenda.
7 Wapendwa, siwaandikii ninyi amri mpya bali ile ya zamani, ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo. Amri hii ya zamani ni lile neno mlilosikia.
8 Lakini nawaandikia amri mpya, yaani lile neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu, kwa sababu giza linapita na ile nuru ya kweli tayari inang’aa.
9 Yeyote anayesema yumo nuruni lakini anamchukia ndugu yake bado yuko gizani.
10 Yeye ampendaye ndugu yake anakaa nuruni, wala hakuna kitu chochote ndani yake cha kumkwaza.
11 Lakini yeyote amchukiaye ndugu yake, yuko gizani na anaenenda gizani, wala hajui anakoenda, kwa sababu giza limempofusha macho.
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu dhambi zenu zimesamehewa kwa ajili ya Jina lake.
13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.
14 Nawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu.
15 Msiupende ulimwengu wala mambo yaliyo ulimwenguni. Mtu yeyote akiupenda ulimwengu, upendo wa Baba haumo ndani yake.
16 Kwa maana kila kitu kilichomo ulimwenguni, yaani tamaa ya mwili, tamaa ya macho na kiburi cha uzima, havitokani na Baba bali hutokana na ulimwengu.
17 Nao ulimwengu unapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu milele.
18 Watoto wadogo, huu ni wakati wa mwisho! Kama mlivyosikia kwamba anayempinga Al-Masihi anakuja, hivyo basi wanaompinga Al-Masihi wengi wamekwisha kuja. Kutokana na hili twajua kwamba huu ni wakati wa mwisho.
19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu hasa. Kwa maana kama wangekuwa wa kwetu, wangekaa pamoja nasi; lakini kutoka kwao kulionesha kwamba hakuna hata mmoja wao aliyekuwa wa kwetu.
20 Lakini ninyi mmepakwa mafuta na yeye Aliye Mtakatifu, nanyi nyote mnaijua kweli.
21 Siwaandikii kwa sababu hamuijui kweli, bali kwa sababu mnaijua, nanyi mnajua hakuna uongo unaotoka katika kweli.
22 Je, mwongo ni nani? Mwongo ni mtu yule asemaye kwamba Isa si Al-Masihi. Mtu kama huyo ndiye anayempinga Al-Masihi, yaani yeye humkana Baba na Mwana.
23 Hakuna yeyote amkanaye Mwana aliye na Baba. Yeyote anayemkubali Mwana anaye na Baba pia.
24 Bali ninyi, hakikisheni kwamba lile mlilosikia tangu mwanzo linadumu ndani yenu. Kama lile mlilosikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana na ndani ya Baba.
25 Hii ndiyo ahadi yake kwetu, yaani uzima wa milele.
26 Nawaandikia mambo haya kuhusu wale watu ambao wanajaribu kuwapotosha.
27 Bali ninyi, upako mlioupata kutoka kwake unadumu ndani yenu, wala ninyi hamna haja ya mtu yeyote kuwafundisha. Lakini kama vile upako wake unavyowafundisha kuhusu mambo yote nayo ni kweli wala si uongo, basi kama ulivyowafundisha kaeni ndani yake.
28 Sasa basi, watoto wapendwa, kaeni ndani yake, ili atakapofunuliwa, tuwe na ujasiri, wala tusiaibike mbele zake wakati wa kuja kwake.
29 Mkijua kuwa yeye ni mwenye haki, mwajua kwamba kila atendaye haki amezaliwa naye.
Cross-references
229
- 11Ti 2:5, Rom 8:34, Jhn 14:6, 1Jn 1:8–10, Heb 7:24–26, 2Co 5:21, Tit 2:11–13, 1Jn 4:4
- 21Jn 4:14, 1Pe 3:18, 1Jn 4:10, Jhn 1:29, 1Pe 2:24, Jhn 4:42, 2Co 5:18–21, Jhn 11:51–52
- 3Jhn 14:15, Jhn 15:10, 1Jn 5:3, Luk 6:46, 1Jn 4:13, Jhn 15:14, 1Jn 3:22–24, Heb 5:9
- 41Jn 1:6, Tit 1:16, Jas 2:14–16, 1Jn 1:8, 1Jn 4:20, 1Jn 2:9, Hos 8:2–3, 1Jn 1:10
- 5Jhn 14:23, Jhn 14:21, 1Jn 4:12–13, Luk 11:28, 1Jn 3:24, Psa 119:2, Rev 14:12, 1Jn 5:2
- 61Pe 2:21, Jhn 13:15, 1Co 11:1, 1Jn 3:6, Jhn 15:4–6, Eph 5:2, Mat 11:29, 1Jn 1:6–7
- 71Jn 3:11, Lev 19:18, Mrk 12:29–34, 2Jn 1:5–6, Gal 5:13–14, Rom 13:8–10, Mat 22:37–40, 1Jn 3:23
- 8Eph 5:8, Rom 13:12, Jhn 13:34, Jhn 8:12, 2Co 4:4–6, Jhn 12:46, Jhn 1:9, Jhn 1:4–5
- 91Jn 4:20, 1Jn 2:11, 1Jn 3:13–17, Psa 82:5, 2Pe 1:9, 1Co 13:1–3, 1Jn 2:4, 1Jn 1:6
- 101Jn 3:14, Rom 9:32–33, Hos 6:3, Rom 14:13, 2Pe 1:10, Mat 13:21, Mat 18:7, Jhn 8:31
- 11Jhn 12:35, Tit 3:3, 1Jn 1:6, Rev 3:17, Pro 4:19, 2Co 4:4, Jhn 12:40, 1Jn 2:9
- 12Act 10:43, Act 13:38, Eph 1:7, Psa 106:8, Act 4:12, Psa 25:11, Luk 7:47–50, Col 1:14
- 13Jhn 14:7, 1Jn 2:14, 1Jn 4:4, 1Jn 1:1, Luk 10:22, 1Jn 5:4–5, Jhn 17:3, Eph 6:10–12
- 14Psa 119:11, 1Jn 2:13, Col 3:16, Jhn 15:7, Eph 6:10, Jhn 8:31, Jhn 5:38, Rev 2:7
- 15Jas 4:4, Rom 12:2, Mat 6:24, Col 3:1–2, Luk 16:13, 1Jn 5:4–5, Jhn 15:19, 1Jn 3:17
- 16Rom 13:14, Gal 5:17, Psa 119:36–37, Gen 3:6, Pro 27:20, Eph 2:3, 1Pe 2:11, 2Pe 2:10
- 17Mat 24:35, Rom 12:2, 1Co 7:31, 1Pe 4:2, Heb 10:36, Mrk 3:35, Isa 40:6–8, 1Pe 1:24–25
- 181Jn 4:3, 2Jn 1:7, 1Jn 2:22, Mat 24:24, Mat 24:5, 1Jn 4:1, 2Ti 4:3–4, 2Th 2:3–12
- 19Act 20:30, 1Co 11:19, Luk 8:13, Jud 1:19, 2Pe 2:20–21, Mat 13:20–21, 2Ti 2:19, Jhn 6:37–39
- 201Jn 2:27, Jhn 14:26, 2Co 1:21–22, Isa 61:1, Psa 23:5, Pro 28:5, Act 10:38, Heb 1:9
- 212Pe 1:12, Jud 1:5, Pro 1:5, Pro 9:8–9, Rom 15:14–15
- 222Jn 1:7, 1Jn 4:3, 1Jn 2:18, Jud 1:4, 1Jn 2:23, 1Jn 2:4, 1Jn 4:20, 1Jn 1:6
- 231Jn 4:15, Jhn 8:19, Jhn 5:23, Jhn 10:30, 2Jn 1:9–11, Jhn 15:23–24, 1Jn 5:1, Jhn 14:9–10
- 24Jhn 14:23, Jhn 15:9–10, 1Jn 4:13, 1Jn 4:16, 2Jn 1:5–6, Rev 3:3, Jhn 15:7, 1Jn 2:7
- 25Jhn 10:28, Tit 3:7, Jud 1:21, Jhn 17:2–3, Tit 1:2, 1Ti 6:12, 1Jn 1:2, Rom 5:21
- 262Pe 2:1–3, 2Jn 1:7, 1Jn 3:7, Act 20:29–30, Mrk 13:22, Col 2:8, 1Ti 4:1, 2Co 11:13–15
- 27Jhn 14:26, 1Jn 2:20–21, 1Co 2:13, Jhn 16:13, Jer 31:33–34, Heb 8:10–11, 1Th 2:13, Jhn 15:4–7
- 281Jn 4:17, Mrk 8:38, 1Th 3:13, 1Jn 3:2, 1Jn 3:21, Col 3:4, Heb 9:28, 1Jn 2:1
- 29Jhn 3:3–5, 1Jn 3:7, Jhn 1:13, 1Jn 5:1, 1Jn 4:7, 1Jn 3:9–10, Jas 1:18, 1Jn 5:4
Topics in this chapter
54
Advocate, Ambition, Anointing, Antichrist, Assurance, Atonement, Blindness, Boldness, Character, Children, Commandments, Confession, Covetousness, Darkness, Decision, Depravity of Man, Example, Eye, Fellowship, Fraternity, God, Gospel, Hatred, Holiness, Holy Spirit, Hypocrisy, Immortality, Jesus, the Christ, Life, Love, Lust, Malice, Minister, Christian, Obedience, Perfection, Perseverance, Pride, Prophecy, Propitiation, Regeneration, Righteous, Righteousness, Salvation, Satan, Sin, Symbols and Similitudes, Temptation, Unbelief, Unction, War, Wisdom, Word of God, Worldliness, Young Men