Kutoka 17
1 Jumuiya yote ya Israeli ikaondoka kutoka Jangwa la Sini, ikisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine kama Mwenyezi Mungu alivyoagiza. Wakapiga kambi huko Refidimu, lakini hapakuwa na maji ya watu kunywa.
2 Kwa hiyo wakagombana na Musa wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Musa akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Mwenyezi Mungu?”
3 Lakini watu walikuwa na kiu huko, wakanung’unika dhidi ya Musa, wakisema, “Kwa nini ulitutoa kule Misri, ukatuleta hapa utuue kwa kiu sisi, watoto wetu na mifugo yetu?”
4 Kisha Musa akamlilia Mwenyezi Mungu, akasema, “Niwafanyie nini watu hawa? Sasa wanakaribia kunipiga kwa mawe.”
5 Mwenyezi Mungu akamjibu Musa, “Nenda mbele ya watu. Wachukue pamoja nawe baadhi ya wazee wa Israeli, na uchukue mkononi mwako ile fimbo uliyopiga nayo Mto Naili, nawe uende.
6 Huko nitasimama mbele yako karibu na mwamba wa Horebu. Uupige mwamba na maji yatatoka ndani yake kwa ajili ya watu kunywa.” Kwa hiyo Musa akafanya haya mbele ya wazee wa Israeli.
7 Naye akapaita mahali pale Masa na Meriba, kwa sababu Waisraeli waligombana na kumjaribu Mwenyezi Mungu wakisema, “Je, Mwenyezi Mungu yu pamoja nasi au la?”
8 Waamaleki wakaja na kuwashambulia Waisraeli huko Refidimu.
9 Musa akamwambia Yoshua, “Chagua baadhi ya watu wetu na uende kupigana na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima nikiwa na fimbo ya Mungu mkononi mwangu.”
10 Kwa hiyo Yoshua akapigana na Waamaleki kama Musa alivyomwagiza, nao Musa, Haruni na Huri wakapanda juu ya kilima.
11 Ikawa wakati wote Musa alipokuwa amenyanyua mikono yake, Waisraeli walikuwa wakishinda, lakini kila aliposhusha mikono yake Waamaleki walishinda.
12 Mikono ya Musa ilipochoka, wakachukua jiwe na kumpa alikalie. Haruni na Huri wakaishikilia juu mikono ya Musa, mmoja upande huu na mwingine upande huu. Wakaitegemeza mikono yake ikabaki thabiti hadi jua lilipozama.
13 Kwa hiyo Yoshua akalishinda jeshi la Waamaleki kwa upanga.
14 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Andika mambo haya katika kitabu ili yakumbukwe, na uhakikishe kwamba Yoshua amesikia, kwa sababu nitafuta kabisa kumbukumbu la Amaleki chini ya mbingu.”
15 Musa akajenga madhabahu na kuiita Yehova Nisi.
16 Musa akasema, “Kwa maana mikono iliinuliwa dhidi ya kiti cha enzi cha Mwenyezi Mungu, sasa Mwenyezi Mungu atakuwa na vita dhidi ya Waamaleki kizazi hadi kizazi.”
Cross-references
96
- 1Exo 19:2, Exo 16:1, Num 33:12–14, Exo 17:8
- 2Psa 78:18, 1Co 10:9, Psa 78:41, Deu 6:16, Heb 3:9, Isa 7:12, Act 15:10, Num 20:2–5
- 3Exo 16:2–3, Exo 15:24
- 41Sa 30:6, Num 14:10, Jhn 10:31, Jhn 8:59, Act 14:19, Exo 15:25, Act 7:50, Num 16:19
- 5Exo 7:19–20, Num 20:8–11, Ezk 2:6, Act 20:23–24
- 61Co 10:4, Num 20:9–11, Neh 9:15, Psa 105:41, Deu 8:15, Psa 78:15–16, Jhn 4:10, Psa 114:8
- 7Psa 81:7, Num 20:13, Psa 95:8, Deu 9:22, Heb 3:8–9, Exo 17:2, Act 7:37–39, Num 20:24
- 8Gen 36:12, Deu 25:17–19, 1Sa 30:1, Num 24:20, 1Sa 15:2, Psa 83:7, Gen 36:16
- 9Exo 4:20, Deu 32:44, Exo 24:13, Exo 4:2, Heb 4:8, Num 31:3–4, Exo 17:13, Num 11:28
- 10Exo 24:14, Exo 31:2, Jos 11:15, Exo 17:12, Jhn 2:5, Jhn 15:14, Mat 28:20
- 111Ti 2:8, Jas 5:16, Luk 18:1, Psa 56:9
- 12Isa 35:3, Php 1:19, Heb 12:12, Eph 6:18, Mrk 14:37–40, 2Co 1:11, 1Th 5:25, Col 4:2
- 13Jos 10:42, Jos 10:28, Jos 11:12, Jos 10:37, Jos 10:32
- 14Exo 34:27, 1Sa 30:17, 1Sa 30:1, Num 24:20, Num 33:2, Deu 25:17–19, 2Sa 8:12, Exo 12:14
- 15Gen 22:14, Jdg 6:24, Psa 60:4, Gen 33:20
- 16Psa 21:8–11, Isa 66:1, Act 7:49
Topics in this chapter
31
Aaron, Afflictions and Adversities, Altar, Amalekites, Armies, Backsliders, Blessing, Chiding, Evil for Good, Government, Horeb, Hur, Infidelity, Ingratitude, Intercession, Israel, Jehovah-Nissi, Joshua, Massah, Meekness, Meribah, Miracles, Moses, Murmuring, Persecution, Prayer, Presumption, Rephidim, Symbols and Similitudes, Trouble, Water