Kutoka 25
1 Mwenyezi Mungu akamwambia Musa,
2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa niaba yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa.
3 “Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: “dhahabu, fedha na shaba;
4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, za rangi nyekundu, pamoja na kitani safi; singa za mbuzi;
5 ngozi za kondoo dume zilizopakwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo; mbao za mshita;
6 mafuta ya zeituni kwa ajili ya taa; vikolezo kwa ajili ya mafuta ya upako, pamoja na uvumba wa harufu nzuri;
7 na vito vya shohamu na vito vingine vya thamani vya kuweka kwenye kizibau na kile kifuko cha kifuani.
8 “Kisha uwaamuru wanitengenezee mahali patakatifu, nami nitakaa miongoni mwao.
9 Tengeneza Maskani hii na vyombo vyake vyote sawasawa na kielelezo nitakachokuonesha.
10 “Nao watatengeneza Sanduku la mbao za mshita, lenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, upana wa dhiraa moja na nusu, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 Utalifunika hilo Sanduku kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulifanyia ukingo wa dhahabu juu yake kulizunguka.
12 Utalisubu kwa pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
13 Kisha utatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
14 Utaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
15 Hiyo mipiko itabakia daima katika hizo pete za hilo Sanduku; haitaondolewa.
16 Kisha weka ndani ya hilo Sanduku ule Ushuhuda nitakaokupa.
17 “Tengeneza kifuniko cha upatanisho cha dhahabu safi, chenye urefu wa dhiraa mbili na nusu, na upana wa dhiraa moja na nusu.
18 Tengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
19 Tengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; watengeneze makerubi hao wawe kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
20 Makerubi hao watakuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao wataelekeana, wakitazama hicho kifuniko.
21 Weka huo Ushuhuda nitakaokupa ndani ya hilo Sanduku la Agano, na uweke hicho kifuniko juu ya hilo Sanduku.
22 Hapo juu ya hicho kifuniko, kati ya hao makerubi wawili walio juu ya hilo Sanduku la Ushuhuda, hapo ndipo nitakutana nawe na kukupa maagizo yangu kwa ajili ya Waisraeli.
23 “Tengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
24 Ifunike kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
25 Kisha tengeneza upapi wenye upana wa nyanda moja, na ufanyie ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
26 Tengeneza pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na uzifungie kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
27 Pete hizo zitakuwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko itakayotumika kuibebea hiyo meza.
28 Tengeneza mipiko hiyo kwa mbao za mshita, uifunike na dhahabu, uitumie kubeba hiyo meza.
29 Tengeneza sahani zake na masinia yake kwa dhahabu safi, pamoja na bilauri na bakuli zake kwa ajili ya kumiminia sadaka.
30 Utaweka mikate ya Wonesho juu ya meza hii iwe mbele yangu daima.
31 “Tengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vinavyofanana na ua, matovu yake na maua yake viwe kitu kimoja.
32 Matawi sita yatatokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
33 Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vitakuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yanayotokeza kwenye kile kinara cha taa.
34 Juu ya kinara chenyewe vitakuwa vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi, yakiwa na matovu yake na maua yake.
35 Tovu moja litakuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani matawi sita kwa jumla.
36 Matovu na matawi yote yatakuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakifuliwa kwa dhahabu safi.
37 “Kisha tengeneza taa zake saba na uziweke juu ya kinara hicho ili ziangaze mbele yake.
38 Mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote zitakuwa za dhahabu safi.
39 Utatumia talanta moja ya dhahabu safi kutengeneza hicho kinara na vifaa vyake vyote.
40 Hakikisha kuwa umevitengeneza sawasawa na ule mfano uliooneshwa kule mlimani.
Cross-references
178
- 22Co 9:7, Neh 11:2, Ezr 2:68, Ezr 7:16, Ezr 1:6, Ezr 3:5, 1Ch 29:1–30, Psa 110:3
- 3Deu 8:9, Job 28:2
- 4Rev 19:8, Gen 41:42, Ezk 16:10
- 5Exo 26:14–15, Exo 26:37–27:1, Exo 36:20, Exo 26:26
- 6Exo 27:20, Exo 30:23–38, Exo 25:37, Exo 40:24–25
- 7Exo 28:4, Exo 28:6–30
- 82Co 6:16, Rev 21:3, 1Ki 6:13, Exo 29:45, Heb 9:1–2, Zec 2:10, Heb 3:6, Zec 8:3
- 9Exo 25:40, Heb 8:5, Act 7:44, Heb 9:9, 1Ch 28:11–19
- 10Heb 9:4, Exo 37:1–3, Deu 10:1–3, Rev 11:19, 2Ch 8:11
- 11Exo 25:24, 2Ch 3:4, Exo 30:3, 1Ki 6:20
- 12Exo 37:5, Exo 25:15, Exo 38:7, Exo 27:7, Exo 26:29, Exo 25:26
- 13Exo 40:20, Num 4:11, Num 4:8, 1Ch 15:15, Exo 37:4, Exo 30:5, Exo 27:6, Num 4:14
- 151Ki 8:8, 2Ch 5:9
- 161Ki 8:9, Deu 31:26, Heb 9:4, Exo 16:34, Rom 3:2, Act 7:44, Deu 10:2–5, Exo 34:29
- 17Exo 37:6, Heb 9:5, Rom 3:25, Heb 4:16, Exo 40:20, 1Ch 28:11, Lev 16:12–15, 1Jn 2:2
- 18Heb 9:5, Ezk 10:20, 1Ki 8:6–7, Ezk 10:2, 1Ch 28:18, 1Sa 4:4, Gen 3:24, 1Ki 6:23–28
- 201Ki 8:7, 1Ch 28:18, Heb 9:5, Eph 3:10, Heb 1:14, 1Pe 1:12, 2Ch 3:10, Ezk 28:14
- 21Exo 26:34, Rom 10:4, Exo 25:16–17
- 22Exo 29:42–43, Num 7:89, Isa 37:16, 2Ki 19:15, Psa 80:1, Lev 16:2, Num 17:4, 1Sa 4:4
- 23Exo 37:10–16, Heb 9:2, 2Ch 4:8, 1Ki 7:48, Num 3:31, 2Ch 4:19, Lev 24:6, 1Ch 28:16
- 24Exo 25:11, 1Ki 6:20–22
- 25Exo 37:2, Exo 30:3
- 27Exo 25:28, Exo 25:14
- 28Act 9:15, Exo 25:14, Exo 25:27, Num 10:17
- 29Num 4:7, Exo 37:16, Rev 3:20, Jer 52:18–19, Num 7:31–33, Num 7:19, 2Ch 4:22, Num 7:13
- 30Mat 12:4, Lev 24:5–9, Exo 39:36, Num 4:7, 1Ch 9:32, 1Sa 21:6, Exo 35:13, Mal 1:12
- 311Ki 7:49, Exo 37:17–24, Zec 4:2, Heb 9:2, Rev 1:12, Rev 1:20–2:1, Exo 35:14, 2Ch 13:11
- 33Num 17:4–8, Exo 37:19–20, Zec 4:3, Jer 1:11–12
- 36Exo 25:18, Num 8:4, 1Ki 10:16–17, 2Ch 9:15
- 37Num 8:2, Rev 1:20–2:1, Zec 4:2, Lev 24:2–4, 2Ch 13:11, Exo 27:21, Rev 1:12, Jhn 12:5
- 38Jer 52:18, Exo 37:23, 2Ki 12:13, 1Ki 7:50, Num 4:9, Isa 6:6, 2Ch 4:21, 2Ki 25:14
- 40Heb 8:5, Exo 26:30, Act 7:44, Exo 25:9, Num 8:4, 1Ch 28:19, 1Ch 28:11, Exo 39:42–43
Topics in this chapter
45
Almond, Ark, Badger, Beaten Work, Bowl, Breastplate, Candlestick, Cherubim, Church, Colors, Cotton, Dyeing, Ephod, God, Gold, Handbreadth, Inspiration, Israel, Lamp, Law, Liberality, Measure, Mercy-Seat, Oil, Onyx, Porpoise, Priest, Prophets, Quotations and Allusions, Revelation, Sanctuary, Seal, Shekinah, Shewbread (Showbread), Shittim, Skin, Snuffdishes, Spices, Spoons, Sweet Incense, Tabernacle, Tongs, Types, Word of God, Worship