Kutoka 31
1 Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia Musa,
2 “Tazama, nimemchagua Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda,
3 nami nimemjaza Roho wa Mungu, pamoja na ustadi, uwezo na ujuzi katika aina zote za ufundi,
4 ili kubuni michoro ya kupendeza katika ufundi wa dhahabu, fedha na shaba,
5 kuchonga vito na kuvitia mahali, kufanya ufundi kwa mbao, na kujishughulisha na aina zote za ufundi.
6 Tena nimemteua Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, ili kumsaidia.
7 “Hema la Kukutania, Sanduku la Ushuhuda pamoja na kiti cha rehema juu yake, pia na vifaa vyote vya kwenye hema:
8 meza na vifaa vyake, kinara cha taa cha dhahabu safi na vifaa vyake vyote, madhabahu ya kufukizia uvumba,
9 madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake vyote, sinia na kinara chake,
10 pamoja na mavazi matakatifu yaliyofumwa ya kuhani Haruni, na mavazi kwa ajili ya wanawe wakati wanahudumu katika kazi ya ukuhani,
11 pia mafuta ya upako na uvumba wenye harufu nzuri kwa ajili ya Mahali Patakatifu.
12 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa,
13 “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni lazima mzishike Sabato zangu. Hii itakuwa ni ishara kati yangu na ninyi kwa vizazi vijavyo, ili mpate kujua kwamba Mimi Ndimi Mwenyezi Mungu, niwafanyaye ninyi watakatifu.
14 “ ‘Mtaishika Sabato, kwa sababu ni takatifu kwenu. Yeyote atakayeinajisi lazima auawe, yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima akatiliwe mbali na watu wake.
15 Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba ni Sabato ya mapumziko, takatifu kwa Mwenyezi Mungu. Yeyote afanyaye kazi yoyote siku ya Sabato ni lazima auawe.
16 Waisraeli wataishika Sabato, kuiadhimisha kwa vizazi vijavyo kuwa agano la milele.
17 Itakuwa ishara kati yangu na Waisraeli milele, kwa kuwa kwa muda wa siku sita Mwenyezi Mungu aliumba mbingu na dunia, akapumzika siku ya saba, akastarehe.’ ”
18 Mwenyezi Mungu alipomaliza kusema na Musa juu ya Mlima Sinai, Mungu akampa vile vibao viwili vya Ushuhuda, vibao vya mawe vilivyoandikwa kwa kidole cha Mungu.
Cross-references
90
- 2Exo 36:1, Exo 35:30, Jhn 3:27, Exo 37:1, Mrk 3:16–19, Isa 45:3–4, 1Ch 2:19–20, Exo 33:12
- 3Exo 35:31, 1Ki 7:14, Isa 28:26, 1Co 12:4–11, Isa 28:6, 1Ki 3:9
- 4Exo 26:1, 1Ki 7:14, Exo 25:32–35, 2Ch 2:13–14, Exo 28:15, 2Ch 2:7
- 5Exo 28:9–21
- 6Exo 28:3, Exo 35:10, Exo 35:34–36:1, Jas 1:16–17, Act 13:2, Luk 10:1, Exo 37:1–29, Ecc 4:9–12
- 7Exo 36:8–37:9, Exo 26:1–37, Exo 25:10–22, Exo 27:9–19
- 8Exo 37:10–28, Exo 25:23–40, Exo 30:1–10
- 9Exo 38:1–8, Exo 27:1–8, Exo 30:18–21, Exo 40:11
- 10Lev 8:7–8, Num 4:5–14, Exo 39:1–43, Lev 8:13, Exo 28:1–43
- 11Exo 37:29, Exo 30:23–38
- 13Ezk 20:12, Ezk 20:20, Lev 19:30, 1Th 5:23, Exo 20:8–11, Exo 31:17, Lev 20:8, Jhn 17:17
- 14Exo 35:2–3, Num 15:32–36, Exo 20:8, Ezk 20:12–13, Isa 58:13–14, Ezk 44:24, Ezk 20:24, Ezk 20:21
- 15Gen 2:2, Exo 16:23, Lev 23:3, Exo 34:21, Exo 31:17, Jer 17:24–27, Exo 35:2, Luk 13:14
- 16Jer 50:5, Gen 17:11, Gen 9:13
- 17Exo 31:13, Gen 1:31, Gen 2:2–3, Ezk 20:12, Heb 4:10, Ezk 20:20, Heb 4:3–4, Jer 32:41
- 18Deu 4:13, Exo 32:15–16, Deu 5:22, Exo 24:12, Exo 8:19, 2Co 3:3, Exo 34:1–4, Deu 9:9–11
Topics in this chapter
32
Ahisamach, Aholiab, Anthropomorphisms, Art, Bezalel, Blessing, Carpentry, Carving, Covenant, Decalogue, Genius, Holy Spirit, Hur, Israel, Lapidary, Law, Master Workman, Mechanic, Mercy-Seat, Oil, Revelation, Sabbath, Sanctification, Sanitation, Smith, Stones, Tabernacle, Table, Tailoring, Token, Wisdom, Word of God