Kutoka 1
1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokwenda Misri pamoja na Yakobo, kila mmoja na jamaa yake:
2 Reubeni, Simeoni, Lawi na Yuda;
3 Isakari, Zabuloni na Benyamini;
4 Dani na Naftali, Gadi na Asheri.
5 Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu sabini; Yusufu alikuwa tayari yuko Misri.
6 Basi Yusufu na kaka zake wote na kizazi kile chote walikufa,
7 lakini Waisraeli walikuwa wamezaana na kuongezeka sana, idadi yao ikawa kubwa mno, hadi wakaijaza nchi.
8 Kisha mfalme mwingine ambaye hakufahamu habari za Yusufu akatawala Misri.
9 Akawaambia watu wake, “Tazameni, Waisraeli wamekuwa wengi mno kwa idadi kuliko sisi.
10 Njooni, ni lazima tuwashughulikie kwa uangalifu, la sivyo watazidi kuwa wengi zaidi, na ikiwa patatokea vita, watajiunga na adui zetu kupigana nasi, na kuondoka katika nchi hii.”
11 Basi Wamisri wakaweka wasimamizi wa kuwasimamia na kuwatesa Waisraeli kwa kazi ngumu, nao wakajenga miji ya Pithomu na Ramesesi ya kuweka akiba ya Farao.
12 Lakini walivyozidi kuteswa, ndivyo walivyozidi kuongezeka na kuenea katika nchi. Wamisri wakawaogopa Waisraeli,
13 kwa hiyo wakawatumikisha kwa ukatili.
14 Wakafanya maisha ya Waisraeli kuwa machungu kwa kufanya kazi ngumu ya kutengeneza lami na kufyatua matofali, na kazi zote za mashambani; katika kazi zao zote ngumu, Wamisri waliwatumia Waisraeli kwa ukatili.
15 Mfalme wa Misri akawaita wakunga waliowazalisha Waebrania, ambao majina yao yalikuwa Shifra na Pua, akawaambia,
16 “Mtakapowazalisha wanawake Waebrania, chunguzeni wanapojifungua. Ikiwa ni mtoto wa kiume, muueni; lakini ikiwa ni msichana, mwacheni aishi.”
17 Lakini hao wakunga walimcha Mungu na hawakufanya kile mfalme wa Misri alichowaambia kufanya, bali wakawaacha watoto wa kiume waishi.
18 Ndipo mfalme wa Misri akawaita hao wakunga, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivi? Mbona mmeacha watoto wa kiume waishi?”
19 Wakunga wakamjibu Farao, “Wanawake wa Waebrania ni tofauti na wanawake wa Misri; wao wana nguvu, nao hujifungua watoto kabla wakunga hawajafika.”
20 Kwa hiyo Mungu akawatendea mema wakunga hao. Waisraeli wakaongezeka na kuendelea kuwa wengi zaidi.
21 Kwa vile hao wakunga walimcha Mungu, Mungu akawajalia kuwa na jamaa zao wenyewe.
22 Kisha Farao akatoa agizo hili kwa watu wake wote: “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania lazima atupwe katika Mto Naili, bali kila mtoto wa kike aachwe aishi.”
Cross-references
107
- 11Ch 2:1–2, Gen 46:8–26, Gen 35:23–26, Gen 29:31–30:21, Gen 35:18, Exo 6:14–16, Rev 7:4–8, Gen 49:3–27
- 2Gen 35:22
- 3Exo 28:20, Gen 35:23
- 5Deu 10:22, Gen 46:26–27, Jdg 8:30, Exo 1:20
- 6Gen 50:26, Gen 50:24, Act 7:14–16
- 7Gen 46:3, Deu 26:5, Gen 1:28, Gen 47:27, Gen 35:11, Gen 9:1, Neh 9:23, Gen 48:4
- 8Act 7:18, Ecc 2:18–19, Ecc 9:15
- 9Psa 105:24–25, Jas 3:14–16, Ecc 4:4, Num 22:4–5, Pro 27:4, Pro 14:28, Tit 3:3, Jas 4:5
- 10Act 7:19, Psa 83:3–4, Pro 1:11, Psa 105:25, Psa 10:2, Jas 3:15–18, Pro 21:30, 1Co 3:18–20
- 11Gen 15:13, Gen 47:11, Exo 2:11, Exo 3:7, Psa 81:6, Deu 26:6, Exo 6:6–7, Num 20:15
- 12Psa 105:24, Exo 1:9, Rom 8:28, Act 5:28–33, Jhn 12:19, Act 4:2–4
- 13Deu 4:20
- 14Act 7:19, Num 20:15, Exo 2:23, Exo 6:9, Act 7:34, Psa 81:6, Isa 58:6, Exo 5:7–21
- 16Exo 1:22, Mat 21:38
- 17Act 5:29, Exo 1:21, Mat 10:28, Ecc 12:13, Luk 12:5, Act 4:18–20, Dan 6:13, Pro 16:6
- 18Ecc 8:4, 2Sa 13:28
- 19Jos 2:4–24, 2Sa 17:19–20, 1Sa 21:2
- 20Isa 3:10, Ecc 8:12, Pro 11:18, Heb 6:10, Exo 1:12, Psa 111:5, Psa 61:5, Psa 145:19
- 211Ki 11:38, 1Sa 2:35, Psa 37:3, Ecc 8:12, 2Sa 7:27–29, 1Ki 2:24, 1Sa 25:28, 2Sa 7:11–13
- 22Act 7:19, Pro 1:16, Pro 4:16, Exo 1:16, Rev 16:4–6, Psa 105:25, Gen 41:1, Exo 7:19–21