Kutoka 16
1 Jumuiya yote ya Waisraeli wakaondoka Elimu, wakafika Jangwa la Sini, lililokuwa kati ya Elimu na Sinai, siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili baada ya kutoka Misri.
2 Huko jangwani, jumuiya yote wakawanung’unikia Musa na Haruni.
3 Waisraeli wakawaambia, “Laiti tungekufa kwa mkono wa Mwenyezi Mungu huko Misri! Huko tuliketi tukizunguka masufuria ya nyama na tukala vyakula tulivyovitaka, lakini ninyi mmetuleta huku jangwani ili mpate kuua mkutano huu wote kwa njaa.”
4 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Tazama! Nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Watu watatoka kila siku na kukusanya kitakachowatosha kwa siku ile, kwa njia hii, nitawajaribu nione kama watafuata maelekezo yangu.
5 Siku ya sita watatayarisha kile waletacho ndani, nacho kitakuwa mara mbili kuliko ya kile walichokusanya kila siku.”
6 Kwa hiyo Musa na Haruni wakawaambia Waisraeli wote, “Jioni mtajua kuwa Mwenyezi Mungu ndiye aliwatoa Misri,
7 kisha asubuhi mtauona utukufu wa Mwenyezi Mungu, kwa sababu amesikia manung’uniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani hata mtunung’unikie?”
8 Kisha Musa akasema, “Mtajua kuwa alikuwa Mwenyezi Mungu wakati atakapowapa nyama mle ifikapo jioni na mikate yote mtakayohitaji asubuhi kwa sababu amesikia manung’uniko yenu dhidi yake. Sisi ni nani? Hamnung’uniki dhidi yetu, bali dhidi ya Mwenyezi Mungu.”
9 Kisha Musa akamwambia Haruni, “Iambie jumuiya yote ya Waisraeli kwamba, ‘Mje mbele zake Mwenyezi Mungu, kwa maana amesikia manung’uniko yenu.’ ”
10 Haruni alipokuwa akizungumza na jumuiya yote ya Waisraeli, wakatazama kuelekea jangwani, na huko wakaona utukufu wa Mwenyezi Mungu ukitokeza katika wingu.
11 Mwenyezi Mungu akamwambia Musa,
12 “Nimesikia manung’uniko ya Waisraeli. Waambie, ‘Jioni mtakula nyama, na asubuhi mtashiba mikate. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, Mungu wenu.’ ”
13 Jioni ile kware wakaja wakaifunika kambi na asubuhi kulikuwa na utando wa umande kuzunguka kambi.
14 Umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya mchanga wa jangwa.
15 Waisraeli walipoona, wakaambiana, “Hiki ni nini?” Kwa kuwa hawakujua kilikuwa kitu gani. Musa akawaambia, “Huu ndio mkate ambao Mwenyezi Mungu amewapa mle.
16 Hivi ndivyo Mwenyezi Mungu ameamuru: ‘Kila mmoja akusanye kiasi anachohitaji. Chukueni pishi moja kwa kila mtu mliye naye katika hema lenu.’ ”
17 Waisraeli wakafanya kama walivyoambiwa; baadhi yao wakakusanya zaidi, wengine pungufu.
18 Nao walipopima katika pishi, yule aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa. Kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji.
19 Kisha Musa akawaambia, “Mtu yeyote asibakize chochote hadi asubuhi.”
20 Hata hivyo, wengine hawakuzingatia aliyosema Musa, wakahifadhi kiasi fulani hadi asubuhi, lakini kile alichohifadhi kikajaa mabuu na kuanza kunuka. Kwa hiyo Musa akawakasirikia.
21 Kila asubuhi, kila mmoja alikusanya kiasi alichohitaji na jua lilipokuwa kali, iliyeyuka.
22 Siku ya sita, wakakusanya mara mbili, kiasi cha pishi mbili kwa kila mtu, nao viongozi wa jumuiya wakaja kumwarifu Musa.
23 Musa akawaambia, “Hivi ndivyo alivyoagiza Mwenyezi Mungu: ‘Kesho itakuwa Sabato ya mapumziko, Sabato takatifu kwa Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo okeni kile mnachotaka kuoka na mchemshe kile mnachotaka kuchemsha. Hifadhini chochote kinachobaki na mkiweke hadi asubuhi.’ ”
24 Kwa hiyo wakavihifadhi hadi asubuhi, kama Musa alivyoagiza, na havikunuka wala kuwa na mabuu.
25 Musa akawaambia, “Kuleni leo, kwa sababu leo ni Sabato kwa Mwenyezi Mungu. Hamtapata chochote juu ya nchi leo.
26 Kwa siku sita mtakusanya, lakini siku ya saba, yaani Sabato, hakutakuwa chochote.”
27 Hata hivyo, baadhi ya watu wakatoka kwenda kukusanya siku ya saba, lakini hawakupata chochote.
28 Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia Musa, “Je, mtaacha kushika maagizo na maelekezo yangu hadi lini?
29 Fahamuni kuwa Mwenyezi Mungu amewapa ninyi Sabato, ndiyo sababu katika siku ya sita amewapa mikate ya siku mbili. Kila mmoja inampasa kukaa pale alipo katika siku ya saba. Hata mmoja haruhusiwi kutoka.”
30 Kwa hiyo watu wakapumzika siku ya saba.
31 Waisraeli wakaita ile mikate mana. Ilikuwa myeupe kama mbegu za mtama, na ladha yake ilikuwa kama mkate mwembamba uliotengenezwa kwa asali.
32 Musa akasema, “Hivi ndivyo alivyoagiza Mwenyezi Mungu: ‘Chukueni pishi ya mana na kuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo ili vione mikate niliyowapa mle jangwani nilipowatoa katika nchi ya Misri.’ ”
33 Kwa hiyo Musa akamwambia Haruni, “Chukua gudulia na uweke pishi moja ya mana ndani yake. Kisha uweke mbele za Mwenyezi Mungu ili kihifadhiwe kwa ajili ya vizazi vijavyo.”
34 Kama Mwenyezi Mungu alivyomwagiza Musa, hatimaye Haruni aliiweka ile mana ndani ya Sanduku la Ushuhuda ili aweze kuihifadhi.
35 Waisraeli wakala mana kwa miaka arobaini, mpaka walipofika katika nchi iliyokaliwa na watu; walikula mana hadi walipofika mpakani mwa Kanaani.
36 (Pishi moja ni sehemu ya kumi ya kipimo cha efa.)
Cross-references
179
- 1Num 33:10–12, Exo 17:1, Exo 15:27
- 2Exo 15:24, 1Co 10:10, Psa 106:25, Psa 106:7, Psa 106:13, Exo 14:11, Gen 19:4
- 3Num 11:4–5, Num 20:3–5, Exo 17:3, Deu 28:67, Lam 4:9, Jer 2:6, Num 14:2, Exo 2:23
- 41Co 10:3, Psa 78:24–25, Deu 8:2, Psa 105:40, Exo 15:25, Jhn 6:31–32, Deu 8:16, Mat 6:11
- 5Exo 16:22–23, Lev 25:21–22, Exo 35:2–3
- 6Exo 6:7, Num 16:28, Exo 16:12–13, Num 16:30, Exo 16:3, Exo 16:8, Exo 32:7, Psa 77:20
- 7Isa 40:5, Num 16:11, Jhn 11:40, Exo 16:10, Isa 35:2, Jhn 11:4, Exo 40:34, Num 16:42
- 8Rom 13:2, 1Sa 8:7, Luk 10:16, 1Th 4:8, Num 14:27, Num 21:7, Exo 16:12, Isa 32:6
- 9Num 16:16, Exo 16:8, Exo 16:2
- 10Exo 16:7, Num 16:19, Num 16:42, 1Ki 8:10–11, Exo 13:21–22, Lev 9:6, Exo 40:34–38, Mat 17:5
- 12Jol 3:17, Exo 16:7–8, Ezk 39:22, Exo 6:7, Jer 31:24, Exo 4:5, Zec 13:9, Exo 7:17
- 13Num 11:9, Psa 105:40, Psa 78:27–28, Num 11:31–33
- 14Psa 78:24, Neh 9:15, Num 11:7–9, Psa 105:40, Deu 8:3, Psa 147:16, Exo 16:31
- 15Exo 16:4, Jhn 6:58, Jhn 6:31–32, Exo 16:31, Deu 8:3, 1Co 10:3, Jhn 6:49, Neh 9:20
- 16Exo 16:36, Exo 16:18, Exo 16:32–33
- 182Co 8:14–15
- 19Exo 12:10, Exo 23:18, Mat 6:34, Exo 16:23
- 20Mrk 10:14, Mat 6:19, Luk 12:33, Eph 4:26, Mrk 3:5, Jas 5:2–3, Heb 13:5, Luk 12:15
- 21Ecc 9:10, Mat 6:33, Pro 6:6–11, Jhn 12:35, 2Co 6:2, Ecc 12:1
- 22Exo 16:5, Exo 34:31, Exo 16:16, Lev 25:22, Lev 25:12
- 23Lev 23:3, Exo 20:8–11, Exo 31:15, Exo 35:2–3, Gen 2:2–3, Exo 23:12, Mrk 2:27–28, Luk 23:56
- 24Exo 16:20, Exo 16:33
- 25Exo 16:23, Neh 9:14, Exo 16:29
- 26Exo 20:9–11, Deu 5:13, Ezk 46:1, Luk 13:14
- 27Pro 20:4
- 28Psa 78:10, 2Ki 17:14, Psa 106:13, Psa 78:22, Num 14:11, Ezk 20:13, Ezk 20:16, Mrk 9:19
- 29Exo 31:13, Isa 58:13–14, Ezk 20:12, Luk 23:56, Neh 9:14
- 30Lev 23:3, Deu 5:12–14, Heb 4:9
- 31Num 11:6–9, Sng 2:3, Exo 16:15
- 32Psa 105:5, Psa 111:4–5, Luk 22:19, Psa 103:1–2, Heb 2:1
- 33Heb 9:4
- 34Exo 25:21, Exo 25:16, Exo 27:21, Num 17:10, Exo 40:20, Exo 30:36, Exo 31:18, Deu 10:5
- 35Neh 9:20–21, Jos 5:12, Jhn 6:30–58, Deu 8:2–3, Psa 78:24–25, Num 33:38, Deu 1:8, Deu 34:1–4
- 36Exo 16:16, Exo 16:32–33
Topics in this chapter
38
Aaron, Ark, Blessing, Bread, Church, Cloud, Condescension of God, Coriander, Disobedience to God, Evil for Good, Forty, Frugality, Gluttony, God, Honey, Infidelity, Ingratitude, Instruction, Israel, Manna, Measure, Meekness, Memorial, Miracles, Moses, Murmuring, Omer, Patience, Quail, Quotations and Allusions, Reproof, Sabbath, Servant, Sin, Sinai, Thankfulness, Trouble, Worm