Wimbo Ulio Bora 3
1 Usiku kucha kwenye kitanda changu nilimtafuta yule moyo wangu umpendaye; nilimtafuta, lakini sikumpata.
2 Sasa nitaondoka na kuzunguka mjini, katika barabara zake na viwanja; nitamtafuta yule moyo wangu umpendaye. Kwa hiyo nilimtafuta lakini sikumpata.
3 Walinzi walinikuta walipokuwa wakizunguka mji. Nikawauliza, “Je, mmemwona yule moyo wangu umpendaye?”
4 Kitambo kidogo tu baada ya kuwapita nilimpata yule moyo wangu umpendaye. Nilimshika na sikumwachia aende hadi nilipomleta katika nyumba ya mama yangu, katika chumba cha yule aliyenichukua mimba.
5 Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
6 Ni nani huyu anayekuja kutoka jangwani kama nguzo ya moshi, anayenukia manemane na uvumba iliyotengenezwa kwa vikolezo vyote vya mfanyabiashara?
7 Tazama! Ni gari la Sulemani likisindikizwa na mashujaa sitini, walio wakuu sana wa Israeli,
8 wote wamevaa panga, wote wazoefu katika vita, kila mmoja na upanga wake pajani, wamejiandaa kwa ajili ya vitisho vya usiku.
9 Mfalme Sulemani alijitengenezea gari; alilitengeneza kwa mbao kutoka Lebanoni.
10 Nguzo zake alizitengeneza kwa fedha, kitako chake kwa dhahabu. Kiti chake kilipambwa kwa zambarau, gari lake likanakshiwa njumu kwa upendo na binti za Yerusalemu.
11 Tokeni nje, ninyi binti za Sayuni, mkamtazame Mfalme Sulemani akiwa amevaa taji, taji ambalo mama yake alimvika siku ya arusi yake, siku ambayo moyo wake ulishangilia.
Cross-references
76
- 11Pe 1:8, Sng 1:7, Sng 5:6, Isa 26:9, Isa 55:6, Psa 22:2, Sng 5:8, Psa 130:1–2
- 2Rom 13:11, Eph 5:14, Pro 8:34, Pro 8:2–3, Pro 1:20–21, Luk 14:21–23, Psa 77:7–10, Sng 5:5
- 3Sng 5:7, Isa 21:6–8, Ezk 33:2–9, Jhn 20:15, Isa 21:11–12, Isa 56:10, Ezk 3:17, Heb 13:17
- 4Pro 8:17, Sng 8:2, Sng 6:12, Mat 7:7, Pro 4:13, Isa 55:6–7, Isa 45:19, Lam 3:25
- 5Sng 2:7, Sng 8:4, Mic 4:8
- 6Sng 8:5, Sng 4:6, Rev 12:14, Sng 1:13, Sng 1:3, Deu 8:2, Sng 4:12–14, Jol 2:29–31
- 71Sa 28:2, 1Sa 14:52, Sng 3:9, 1Ki 9:22, Heb 1:14, 1Sa 8:16, 1Ki 14:27, 2Ki 6:17
- 8Psa 45:3, Eph 6:16–18, 1Th 5:6–8, Isa 27:3, Psa 149:5–9, Psa 91:5, Neh 4:21–22
- 9Sng 3:7, 2Sa 23:5, Rev 14:6
- 10Rev 1:5, 1Ti 3:15–16, Rev 3:12, Eph 3:18–19, Psa 87:3, Sng 1:5, Rom 5:8
- 11Isa 62:5, Jer 2:2, Hos 2:19–20, Mat 12:42, Heb 13:13, Zep 3:17, Psa 9:14, Rev 1:7