Nahumu 3
1 Ole wa mji unaomwaga damu, uliojaa uongo, uliojaa nyara, na usiokosa mateka.
2 Kelele za mijeledi, vishindo vya magurudumu, farasi wanaoenda mbio na mshtuo wa magari ya vita!
3 Wapanda farasi wanaenda mbio, panga zinametameta, na mikuki inang’aa! Majeruhi wengi, malundo ya maiti, idadi ya miili isiyohesabika, watu wanajikwaa juu ya mizoga:
4 haya yote kwa sababu ya wingi wa tamaa za kahaba, anayeshawishi, bibi mkuu wa mambo ya uchawi, anayewatia utumwani mataifa kwa ukahaba wake na pia jamaa za watu kwa ulozi wake.
5 Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni anasema, “Mimi ni kinyume na ninyi. Nitafunika uso wako kwa gauni lako. Nitaonesha mataifa uchi wako na falme aibu yako.
6 Nitakutupia uchafu, nitakufanyia dharau na kukufanya kioja.
7 Wote wanaokuona watakukimbia na kusema, ‘Ninawi inaangamia, nani atakayeomboleza kwa ajili yake?’ Nitampata wapi yeyote wa kukufariji?”
8 Je, wewe ni bora kuliko No-Amoni, uliopo katika Mto Naili, uliozungukwa na maji? Mto ulikuwa kinga yake, nayo maji yalikuwa ukuta wake.
9 Kushi na Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka; Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.
10 Hata hivyo alichukuliwa mateka na kwenda uhamishoni. Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande kwenye mwanzo wa kila barabara. Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima, na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.
11 Wewe pia utalewa; utaenda mafichoni na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.
12 Ngome zako zote ni kama mitini yenye matunda yake ya kwanza yaliyoiva; wakati inapotikiswa, tini huanguka kwenye kinywa chake alaye.
13 Tazama vikosi vyako: wote ni wanawake! Malango ya nchi yako yamekuwa wazi kwa adui zako; moto umeteketeza mapingo yake.
14 Teka maji kwa ajili ya kuzingirwa kwako, imarisha ulinzi wako, Ufanyie udongo wa mfinyanzi kazi, yakanyage matope, karabati tanuru la kuchomea matofali!
15 Huko moto utakuteketeza, huko upanga utakuangusha chini na kama vile panzi, watakumaliza. Ongezeka kama panzi, ongezeka kama nzige!
16 Umeongeza idadi ya wafanyabiashara wako hata wamekuwa wengi kuliko nyota za angani, lakini kama nzige wanaacha nchi tupu kisha huruka na kwenda zake.
17 Walinzi wako ni kama nzige, maafisa wako kama makundi ya nzige wanaotua kwenye kuta wakati wa siku ya baridi; lakini wakati jua linapotokea wanaruka kwenda zao, na hakuna anayejua wanakoenda.
18 Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia; wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.
19 Hakuna kitu kinachoweza kuponya jeraha lako; jeraha lako ni la kukuua. Kila anayesikia habari zako, hupiga makofi kwa kuanguka kwako, kwa kuwa ni nani ambaye hajaguswa na ukatili wako usio na mwisho?
Cross-references
128
- 1Hab 2:12, Zep 3:1–3, Ezk 22:2–3, Ezk 24:6–9, Hos 4:2, Nam 2:12, Isa 42:24, Isa 17:14
- 2Jer 47:3, Nam 2:3–4, Jdg 5:22, Job 39:22–25, Isa 9:5
- 3Hab 3:11, Ezk 39:4, Isa 34:3, Isa 37:36, Gen 3:24, 2Ki 19:35, Nam 2:4, Ezk 31:3–13
- 4Isa 47:9, Isa 47:12–13, Rev 18:2–3, Ezk 16:25–29, Rev 17:1–5, Rev 18:23, Rev 18:9, Isa 23:15–17
- 5Jer 13:26, Jer 13:22, Ezk 23:29, Nam 2:13, Isa 47:2–3, Ezk 16:37, Hab 2:16, Mic 1:11
- 6Mal 2:9, Jer 51:37, Psa 38:5–7, Job 9:31, 1Co 4:9, Nam 1:14, Job 30:8, Heb 10:33
- 7Isa 51:19, Jer 15:5, Rev 18:10, Jer 51:9, Lam 2:13, Num 16:34, Nam 2:9–10, Nam 1:1
- 8Amo 6:2, Ezk 30:14–16, Jer 46:25–26, Ezk 31:2–3, Isa 19:5–10
- 9Ezk 30:5, Ezk 27:10, Jer 46:9, Isa 20:5, 2Ch 12:3, Ezk 38:5, Gen 10:6, 1Ch 1:8
- 10Isa 20:4, Oba 1:11, Jol 3:3, Hos 13:16, Isa 13:16, Lam 2:19, Lam 4:1, Psa 137:8
- 11Luk 23:30, Isa 49:26, Isa 2:10, Rev 6:15–17, Hos 10:8, Jer 4:5, Psa 75:8, Nam 1:10
- 12Rev 6:13, Hab 1:10, Isa 28:4
- 13Jer 51:30, Isa 19:16, Jer 50:37, Nam 2:6, Isa 45:1–2, Psa 147:13, Psa 107:16
- 142Ch 32:3–4, Nam 2:1, Jer 46:3–4, Jol 3:9–11, Isa 22:9–11, Jer 46:9, Isa 8:9, 2Ch 32:11
- 15Jol 1:4, Nam 2:13, Nam 3:13, Jol 2:25, Zep 2:13, Exo 10:13–15
- 16Jer 33:22, Neh 9:23, Gen 22:17, Gen 15:5
- 17Jer 51:27, Rev 9:7
- 181Ki 22:17, Psa 76:5–6, Jer 50:18, Jer 51:57, Isa 13:14, Jer 51:39, Isa 47:1, Ezk 31:3–18
- 19Mic 1:9, Lam 2:15, Job 27:23, Isa 37:18, Jer 46:11, Nam 2:11–12, Isa 10:6–14, Isa 14:8–21
Topics in this chapter
24
Armies, Assyria, Brick, Brick-Kiln, Cankerworm, Chariot, Commerce, Dishonesty, Falsehood, Fence, Grasshopper, Lubims, Merchant, Mortar, Nahum, Nineveh, No, Phut, Pride, Sorcery, Theft and Thieves, War, Whip, Women