Isaya 20
1 Mwaka ule jemadari mkuu alitumwa na Mfalme Sargoni wa Ashuru, naye akaja Ashdodi, akaushambulia na kuuteka,
2 wakati huo Mwenyezi Mungu alisema kwa kinywa cha Isaya mwana wa Amozi. Akamwambia, “Vua gunia kutoka mwilini mwako na viatu kutoka miguuni mwako.” Naye akafanya hivyo, akitembea uchi, bila viatu.
3 Kisha Mwenyezi Mungu akasema, “Kama mtumishi wangu Isaya alivyotembea uchi na bila viatu kwa miaka mitatu, kama ishara na dalili mbaya dhidi ya nchi ya Misri na Kushi,
4 vivyo hivyo mfalme wa Ashuru atawaongoza mateka wa Wamisri, na watu wa uhamisho wa Kushi, uchi na bila viatu, vijana hata wazee, wakiwa matako wazi, kwa aibu ya Wamisri.
5 Wale waliotegemea Kushi na kujivunia Misri wataogopa na kuaibika.
6 Katika siku ile watu wanaoishi katika pwani hii watasema, ‘Tazama lililowapata wale tuliowategemea, wale tuliowakimbilia kwa msaada na wokovu kutoka mikononi mwa mfalme wa Ashuru! Tutawezaje basi kupona?’ ”
Cross-references
45
- 12Ki 18:17, 1Sa 6:17, Amo 1:8, Jer 25:29–30, Jer 25:20, 1Sa 5:1
- 2Mic 1:8, 1Sa 19:24, Mat 3:4, Ezk 24:23, Ezk 24:17, Zec 13:4, Isa 13:1, Mic 1:11
- 3Isa 8:18, Num 14:34, Ezk 4:5–6, Isa 18:1–7, Isa 37:9, Rev 11:2–3, Isa 43:3
- 4Isa 19:4, Jer 13:26, Jer 13:22, Mic 1:11, Isa 47:3, Rev 3:18, Jer 46:26, Ezk 30:18
- 5Isa 30:3, Isa 30:5, Jer 17:5, 1Co 3:21, Jer 9:23–24, 2Ki 18:21, Ezk 29:6–7, Isa 36:6
- 6Mat 23:33, Heb 2:3, 1Th 5:3, Isa 28:17, Isa 31:1–3, Jer 30:15–17, Isa 30:15–16, Isa 10:3