Wagalatia 1
1 Paulo mtume, si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Isa Al-Masihi na Mungu Baba Mwenyezi aliyemfufua Isa kutoka kwa wafu,
2 na ndugu wote walio pamoja nami.
3 Neema na amani zitokazo kwa Mungu, Baba yetu, na kwa Bwana wetu Isa Al-Masihi ziwe nanyi,
4 yeye aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu.
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen.
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Al-Masihi na kuifuata Injili nyingine,
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Al-Masihi.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Al-Masihi.
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Isa Al-Masihi.
13 Ninyi mmekwisha kusikia kuhusu maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyotesa makundi ya waumini wa Mungu kwa nguvu na kujaribu kuwaangamiza.
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika langu, maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilienda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana Isa.
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
21 Baadaye nilienda sehemu za Siria na Kilikia.
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makundi ya waumini huko Yudea yaliyo katika Al-Masihi.
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo awali alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
Cross-references
168
- 1Gal 1:11–12, 1Co 1:1, Act 9:15–16, Rom 1:1, Rev 1:5, 2Co 1:1, Eph 3:8, Act 22:14–21
- 21Co 16:1, Php 4:21, Act 16:5–6, Act 18:23, Php 2:22, Act 9:31, Act 15:41
- 32Jn 1:3, 2Co 13:14, Rom 1:7–15, Php 1:2, 2Th 1:2, 1Co 1:3, 1Th 1:1, 2Co 1:2
- 4Mat 20:28, Rom 4:25, Gal 2:20, 1Pe 2:24, 1Jn 2:15–17, 1Jn 5:19–20, 2Co 4:4, Tit 2:14
- 5Rom 11:36, Jud 1:25, Psa 72:19, Heb 13:21, Psa 41:13, 1Ti 1:17, 1Ch 29:13, Rev 5:12
- 62Co 11:4, Gal 5:7–8, Isa 29:13, Psa 106:13, Gal 3:1–5, 1Ti 1:3, Gal 4:9–15, Jer 2:12–13
- 7Act 15:24, Rom 16:17–18, Gal 5:10, 2Co 11:13, Act 15:1–5, Rev 20:3, 2Ti 4:3–4, 2Jn 1:10
- 82Co 11:13–14, Gal 1:9, Rev 22:18–19, 1Co 16:22, Rom 9:3, Mat 25:41, 1Ti 1:19–20, Mrk 14:71
- 9Rom 16:17, Pro 30:6, Rev 22:18–19, Deu 4:2, Deu 12:32–13:11, 2Co 13:1–2, Php 3:1, 2Co 1:17
- 101Th 2:4, Act 5:29, Eph 6:6, Jas 4:4, Mat 22:16, Col 3:22, 2Co 5:9–11, Rom 2:29
- 11Gal 1:1, Eph 3:3–8, 1Co 2:9–10, 1Co 11:23, 1Co 15:1–3, Rom 2:16
- 12Gal 1:16, 1Co 2:10, Gal 1:1, 2Co 12:1, 1Co 11:23
- 13Act 8:3, Act 22:3–5, 1Co 15:9, Act 26:4–5, Act 26:9–11, 1Ti 1:13, Act 9:21, Act 9:26
- 14Col 2:8, Act 26:5, Act 22:3, Php 3:4–6, Mat 15:6, 1Pe 1:8, Act 26:9, Jer 9:14
- 15Jer 1:5, Isa 49:5, Isa 49:1, 2Ti 1:9, Eph 1:5, 1Co 1:9, 2Th 2:13–14, Rom 1:1
- 16Mat 16:17, Eph 3:5–10, Eph 6:12, Eph 1:17–18, Mat 26:41, Deu 33:9, Rom 11:13, 1Co 2:9–13
- 17Act 9:20–25, 2Co 11:32–33, Gal 1:18
- 18Act 9:22–23, Act 9:26–29, Act 22:17–18
- 19Mat 13:55, Mrk 6:3, Mat 12:46, 1Co 9:5, Mat 10:3, Jud 1:1, Mrk 3:18, Act 12:17
- 20Rom 9:1, 2Co 11:31, 2Co 11:10–11
- 21Act 15:41, Act 9:30, Act 6:9, Act 11:25–26, Act 13:1, Act 15:23, Act 21:3, Act 21:39
- 221Th 2:14, Rom 16:7, 2Th 1:1, Act 9:31, Php 1:1, 1Th 1:1, 1Co 1:30
- 231Co 15:8–10, 1Ti 1:13–16, Act 9:13, Act 9:20, Act 9:26, Act 6:7
- 24Act 11:18, Luk 15:10, Mat 9:8, Luk 2:14, Luk 15:32, Col 1:3–4, 2Th 1:12, 2Th 1:10
Topics in this chapter
40
Accursed, Affections, Arabia, Arabians, Atonement, Backsliders, Benedictions, Bigotry, Call, Church, Cilicia, Damascus, Doctrines, Flattery, Galatia, Gentiles, Glorifying God, God, Gospel, Grace of God, Heresy, Ignorance, Instability, Intercession, James, Jesus, the Christ, Minister, Christian, Oath, Paul, Peace, Persecution, Peter, Prayer, Predestination, Redemption, Salvation, Suffering, Syria, Word of God, Zeal, Religious