Mwanzo 15
1 Baada ya jambo hili, neno la Mwenyezi Mungu likamjia Abramu katika maono, akaambiwa: “Usiogope, Abramu. Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.”
2 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mungu Mwenyezi, utanipa nini na mimi sina mtoto, na atakayerithi nyumba yangu ni huyu Eliezeri Mdameski?”
3 Abramu akasema, “Hukunipa watoto, hivyo mtumishi katika nyumba yangu ndiye atakuwa mrithi wangu.”
4 Ndipo neno la Mwenyezi Mungu lilipomjia, likanena: “Mtu huyu hatakuwa mrithi wako, bali mwana atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi.”
5 Akamtoa nje na kusema, “Tazama juu mbinguni na uhesabu nyota, kama hakika utaweza kuzihesabu.” Ndipo akamwambia, “Hivyo ndivyo uzao wako utakavyokuwa.”
6 Abramu akamwamini Mwenyezi Mungu, naye kwake jambo hili likahesabiwa kuwa haki.
7 Pia akamwambia, “Mimi ndimi Mwenyezi Mungu, niliyekutoa Uru ya Wakaldayo nikupe nchi hii uimiliki.”
8 Lakini Abramu akasema, “Ee Bwana Mungu Mwenyezi, nitawezaje kujua kwamba nitaimiliki?”
9 Ndipo Mwenyezi Mungu akamwambia, “Niletee ndama jike, mbuzi, na kondoo dume, kila mmoja wa miaka mitatu, pamoja na hua na kinda la njiwa.”
10 Abramu akamletea hivi vyote, akampasua kila mnyama vipande viwili, akavipanga kila kimoja kuelekea mwenzake, lakini hata hivyo ndege hakuwapasua vipande viwili.
11 Kisha ndege walao nyama wakatua juu ya mizoga, lakini Abramu akawafukuza.
12 Jua lilipokuwa linatua, Abramu akashikwa na usingizi mzito, na giza nene na la kutisha likaja juu yake.
13 Kisha Mwenyezi Mungu akamwambia, “Ujue hakika kwamba wazao wako watakuwa wageni katika nchi isiyo yao, nao watafanywa watumwa na kuteswa kwa miaka mia nne.
14 Lakini nitaliadhibu taifa lile watakalolitumikia kama watumwa, na baadaye watatoka huko na mali nyingi.
15 Wewe hata hivyo utaenda kwa baba zako kwa amani, na kuzikwa katika uzee mwema.
16 Katika kizazi cha nne wazao wako watarudi hapa, kwa maana uovu wa Waamori bado haujafikia kipimo.”
17 Jua lilipokuwa limezama na giza limeingia, tanuru la moshi na mwali wa moto unaowaka vikatokea na kupita kati ya vile vipande vya nyama.
18 Siku hiyo Mwenyezi Mungu akafanya agano na Abramu, na kumwambia, “Nitawapa wazao wako nchi hii, kuanzia Kijito cha Misri hadi mto ule mkubwa, Frati:
19 yaani nchi ya Wakeni, Wakenizi, Wakadmoni,
20 Wahiti, Waperizi, Warefai,
21 Waamori, Wakanaani, Wagirgashi na Wayebusi.”
Cross-references
136
- 1Isa 41:10, Psa 119:114, Psa 84:11, Heb 13:5–6, Gen 26:24, Isa 41:14, Lam 3:24, Deu 33:26–29
- 2Gen 25:21, 1Sa 1:11, Act 7:5, Gen 12:1–3, Pro 17:2, Isa 56:5, Psa 127:3, Gen 43:19
- 3Gen 14:14, Pro 29:21, Ecc 2:7
- 4Gen 17:16, 2Sa 7:12, Gal 4:28, Gen 21:12, 2Ch 32:21, Phm 1:12, 2Sa 16:11
- 5Heb 11:12, Rom 4:18, Deu 1:10, Exo 32:13, Gen 22:17, Deu 10:22, Jer 33:22, 1Ch 27:23
- 6Jas 2:23, Gal 3:6–14, Rom 4:9, Rom 4:20–25, Rom 4:3–6, Psa 106:31, Heb 11:8, Rom 4:11
- 7Gen 12:1, Act 7:2–4, Psa 105:42, Rom 4:13, Gen 13:15–17, Psa 105:44, Neh 9:7–8, Gen 12:7
- 8Luk 1:18, Luk 1:34, 2Ki 20:8, Isa 7:11, Jdg 6:36–40, Jdg 6:17–24, Psa 86:17, Gen 24:2–4
- 9Lev 14:22, Lev 14:30, Luk 2:24, Lev 9:2, Lev 3:6, Lev 3:1, Lev 1:14, Isa 15:5
- 10Jer 34:18–19, Lev 1:17, Gen 15:17
- 11Mat 13:4, Psa 119:13, Ezk 17:7, Ezk 17:3
- 12Gen 2:21, Job 33:15, Dan 10:8–9, Act 9:8–9, 1Sa 26:12, Psa 4:3–5, Job 4:13–14
- 13Act 7:6–7, Exo 1:11, Exo 12:40–41, Act 7:17, Gal 3:17, Exo 1:1–2, Lev 19:34, Psa 105:11–12
- 14Neh 9:9–11, Exo 6:5–6, Exo 12:32–38, Jos 24:4–7, Exo 7:1–14, 1Sa 12:8, Psa 135:14, Deu 4:20
- 15Job 5:26, Gen 25:7–9, 2Ch 34:28, Num 27:13, Dan 12:13, Act 13:36, Jdg 2:10, Ecc 12:7
- 161Ki 21:26, Dan 8:23, Exo 12:40, Mat 23:32–35, 1Th 2:16, 2Pe 3:8–9, Zec 5:5–11
- 17Jer 34:18–19, Jdg 6:21, Jer 11:4, 1Ch 21:26, Exo 3:2–3, Isa 62:1, Deu 4:20, Jdg 13:20
- 18Jos 1:3–4, Gen 12:7, Gen 24:7, Gen 13:15, Deu 11:24, Num 34:5, Exo 23:27–31, Isa 27:12
- 19Num 24:21–22
- 20Isa 17:5, Gen 14:5
- 21Deu 7:1, Exo 34:11, Exo 23:23–28, Exo 33:2, Gen 10:15–19, Mat 8:28
Topics in this chapter
53
Abraham, Adoption, Afflictions and Adversities, Amorites, Blessing, Canaan, Canaanites, Chaldea, Children, Concubinage, Condescension of God, Covenant, Damascus, Death, Doubting, Dove, Turtle, Egypt, Eliezer, Euphrates, Faith, Fire, Girgashites, Goat, God, Grace of God, Heir, Inheritance, Israel, Jebusites, Justification, Kenites, Kenizzites, Lamp, Land, Miracles, Offerings, Old Age, Perizzites, Pigeon, Prayer, Probation, Quotations and Allusions, Religion, Rephaim, Righteous, Righteousness, Rulers, Shield, Sign, Steward, Symbols and Similitudes, Ur, Vision