Ruthu 1
1 Waamuzi walipotawala Israeli, kulikuwa na njaa katika nchi. Mtu mmoja kutoka nchi ya Bethlehemu ya Yuda, pamoja na mke wake na wanawe wawili, akaenda kuishi katika nchi ya Moabu.
2 Mtu huyu aliitwa Elimeleki, mkewe aliitwa Naomi, na hao wanawe wawili waliitwa Maloni na Kilioni. Walikuwa Waefrathi kutoka Bethlehemu ya Yuda. Wakaenda katika nchi ya Moabu, wakaishi huko.
3 Elimeleki mumewe Naomi akafa, hivyo Naomi akabaki na wanawe wawili.
4 Nao wakaoa wanawake Wamoabu, jina la mmoja aliitwa Orpa, na wa pili aliitwa Ruthu. Baada ya kuishi huko miaka kumi,
5 Maloni na Kilioni pia wakafa. Basi Naomi akabaki hana mume wala wanawe wawili.
6 Aliposikia akiwa huko Moabu kwamba Mwenyezi Mungu amewasaidia watu wake kwa kuwapa chakula, Naomi na wakwe wake wakajiandaa kurudi nyumbani.
7 Yeye na wakwe wake wawili wakaondoka pale walipokuwa wakiishi na kushika njia kurudi nchi ya Yuda.
8 Ndipo Naomi akawaambia wale wakwe wake wawili, “Rudini, kila mmoja wenu nyumbani mwa mama yake. Mwenyezi Mungu na awatendee mema kama mlivyowatendea hao waliofariki, na mimi pia.
9 Mwenyezi Mungu na amjalie kila mmoja wenu maisha mema nyumbani mwa mume mwingine.” Kisha akawabusu, nao wakalia kwa sauti kubwa,
10 wakamwambia, “Tutarudi pamoja na wewe kwa watu wako.”
11 Lakini Naomi akasema, “Rudini nyumbani, binti zangu. Kwa nini mnifuate? Je, mimi nitaweza tena kuwa na wana wengine ambao wataweza kuwaoa ninyi?
12 Rudini nyumbani, binti zangu; mimi ni mzee kiasi kwamba siwezi kumpata mume mwingine. Hata kama ningefikiria kuwa bado kuna tumaini kwangu, hata kama ningekuwa na mume usiku huu na kuwazaa wana,
13 je, mngesubiri hadi wakue? Mngebakia bila kuolewa mkiwasubiri? La, hasha, binti zangu. Nimepata uchungu kuliko ninyi, kwa sababu mkono wa Mwenyezi Mungu umekuwa kinyume nami!”
14 Kisha wakalia tena kwa sauti. Orpa akambusu mama mkwe wake, akaenda zake, lakini Ruthu akaambatana naye.
15 Naomi akamwambia, “Tazama, mwenzako anarejea kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudi pamoja naye.”
16 Lakini Ruthu akajibu, “Usinisihi nikuache au niache kukufuata. Utakakoenda nami nitaenda, na wewe utakapoishi nitaishi. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
17 Pale utakapofia nami nitafia hapo, na papo hapo nitazikwa. Mwenyezi Mungu na aniadhibu vikali, kama kitu kingine chochote kitanitenga nawe isipokuwa kifo.”
18 Naomi alipotambua kwamba Ruthu amenuia kufuatana naye, hakuendelea kumsihi tena.
19 Kwa hiyo hao wanawake wawili wakaondoka, wakafika Bethlehemu. Walipofika Bethlehemu, mji mzima ulitaharuki, wanawake wakashangaa, wakasema, “Huyu aweza kuwa ni Naomi?”
20 Akawaambia, “Msiniite tena Naomi; niiteni Mara, kwa sababu Mwenyezi amenitendea mambo machungu sana.
21 Mimi niliondoka hali nimejaa, lakini Mwenyezi Mungu amenirudisha mtupu. Kwa nini kuniita Naomi? Mwenyezi Mungu amenitendea mambo machungu; Mwenyezi ameniletea msiba.”
22 Kwa hiyo Naomi alirudi pamoja na Ruthu Mmoabu mkwe wake, nao wakafika Bethlehemu mwanzoni mwa kuvuna shayiri.
Cross-references
119
- 1Gen 12:10, Gen 26:1, Ezk 14:13, Lev 26:19, 2Ki 8:1–2, Jdg 17:8, Gen 43:1, Jol 1:16–20
- 2Gen 35:19, 1Sa 17:21, Mic 5:2, 1Sa 1:1
- 3Psa 34:19, Heb 12:6, 2Ki 4:1, Heb 12:10–11
- 4Mat 1:5, Deu 7:3, 1Ki 11:1–2, Deu 23:3
- 5Deu 32:39, Psa 89:30–32, Isa 49:21, Luk 7:12, Mat 22:25–27, Jer 2:19
- 6Psa 132:15, Psa 111:5, Exo 3:16, Exo 4:31, Exo 16:4–6, Mat 6:11, Luk 1:68, 1Sa 2:21
- 72Ki 8:3, Rut 1:10, Exo 18:27, Rut 1:14
- 8Rut 1:5, Rut 2:20, Col 3:18, Col 3:24, Eph 6:2–3, Eph 5:22, Jos 24:15–28, 2Ti 1:16–18
- 9Rut 3:1, Gen 29:11, Act 20:37, Gen 45:15, Gen 27:27
- 10Zec 8:23, Psa 119:63, Psa 16:3
- 11Deu 25:5, Gen 38:11
- 12Gen 17:17, 1Ti 5:9
- 13Job 19:21, Psa 32:4, Jdg 2:15, Psa 38:2, Psa 39:9–10, 1Sa 5:11, Deu 2:15
- 14Pro 18:24, Mat 16:24, Mat 10:37, Jhn 6:66–69, Mat 19:22, Heb 10:39, 1Ki 19:20, Pro 17:17
- 15Zep 1:6, Jdg 11:24, Jos 24:15, Psa 125:5, 2Ki 2:2, Psa 36:3, Luk 14:26–33, Heb 10:38
- 162Sa 15:21, Rut 2:11–12, 2Ki 2:2–6, Psa 45:10, Mat 8:19, Jhn 13:37, 1Th 1:9, Isa 14:1
- 171Sa 3:17, 1Ki 2:23, 2Ki 6:31, 2Sa 19:13, 1Sa 25:22, 1Ki 20:10, 2Sa 3:35, 1Ki 19:2
- 18Act 21:14, Act 2:42, Eph 6:10
- 19Mat 21:10, Lam 2:15, Isa 23:7
- 20Job 6:4, Heb 12:11, Psa 88:15, Isa 38:13, Job 19:6, Psa 73:14, Lam 3:1–20, Job 5:17
- 211Sa 2:7–8, Job 1:21, Job 13:26, Job 16:8, Job 10:17
- 22Rut 2:23, 2Sa 21:9, Exo 9:31–32
Topics in this chapter
29
Afflictions and Adversities, Benedictions, Bereavement, Bethlehem, Blessing, Canaan, Children, Chilion, Constancy, Converts, Daughter-in-Law, Decision, Elimelech, Friendship, God, Imprecation, Kiss, Love, Mahlon, Moabites, Mother-in-Law, Naomi, Oath, Orpah, Parents, Readings, Select, Ruth, Widow, Women