Isaya 38
1 Katika siku hizo Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Nabii Isaya mwana wa Amozi akaenda kwake na kumwambia, “Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu: Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona.”
2 Hezekia akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Mwenyezi Mungu:
3 “Ee Mwenyezi Mungu, kumbuka jinsi nilivyoenenda mbele zako kwa uaminifu na kujitoa kwa moyo wangu wote, na kufanya yaliyo mema machoni pako.” Naye Hezekia akalia kwa uchungu.
4 Ndipo neno la Mwenyezi Mungu likamjia Isaya, kusema:
5 “Nenda ukamwambie Hezekia, ‘Hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, Mungu wa baba yako Daudi: Nimeyasikia maombi yako na nimeona machozi yako. Nitakuongezea miaka kumi na tano katika maisha yako.
6 Nami nitakuokoa wewe pamoja na mji huu kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Nitaulinda mji huu.
7 “ ‘Hii ndiyo ishara ya Mwenyezi Mungu kwako kwamba Mwenyezi Mungu atafanya kile alichoahidi:
8 Nitafanya kivuli cha jua kwenye ngazi iliyojengwa na Ahazi kirudi nyuma madaraja kumi.’ ” Hivyo jua likarudi nyuma madaraja kumi ambayo lilikuwa limeshuka.
9 Maandiko ya Hezekia mfalme wa Yuda baada ya kuugua kwake na kupona:
10 Nilisema, “Katika ustawi wa maisha yangu, je, ni lazima nipite katika malango ya mauti, na kupokonywa miaka yangu iliyobaki?”
11 Nilisema, “Sitamwona tena Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu katika nchi ya walio hai, wala sitamtazama tena mwanadamu, wala kuwa na wale ambao sasa wanakaa katika ulimwengu huu.
12 Kama hema la mchunga mifugo, nyumba yangu imebomolewa na kutwaliwa kutoka kwangu. Kama mfumaji nimevingirisha maisha yangu, naye amenikatilia mbali kutoka kitanda cha mfumi. Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.
13 Nilingoja kwa uvumilivu hadi mapambazuko, lakini alivunja mifupa yangu yote kama simba. Mchana na usiku uliyakomesha maisha yangu.
14 Nililia kama mbayuwayu au korongo, niliomboleza kama hua aombolezaye. Macho yangu yalififia nilipotazama mbinguni. Ee Bwana, ninataabika, njoo unisaidie!”
15 Lakini niseme nini? Amesema nami, naye yeye mwenyewe amelitenda hili. Nitatembea kwa unyenyekevu katika miaka yangu yote kwa sababu ya haya maumivu makali ya nafsi yangu.
16 Bwana, kwa mambo kama haya watu huishi, nayo roho yangu hupata uzima katika hayo pia. Uliniponya na kuniacha niishi.
17 Hakika ilikuwa ya faida yangu ndiyo maana nikapata maumivu makali. Katika upendo wako ukaniokoa kutoka shimo la uharibifu; umeziweka dhambi zangu zote nyuma yako.
18 Kwa maana kaburi haliwezi kukusifu, mauti haiwezi kuimba sifa zako; wale wanaoshuka shimoni hawawezi kuutarajia uaminifu wako.
19 Walio hai, walio hai: hao wanakusifu, kama ninavyofanya leo. Baba huwaambia watoto wao habari za uaminifu wako.
20 Mwenyezi Mungu ataniokoa, nasi tutaimba kwa vyombo vya nyuzi siku zote za maisha yetu katika Hekalu la Mwenyezi Mungu.
21 Isaya alikuwa amesema, “Tengenezeni dawa ya kubandika ya tini, mweke juu ya jipu, naye atapona.”
22 Hezekia alikuwa ameuliza, “Kutakuwa na ishara gani kwamba nitapanda kwenda Hekalu la Mwenyezi Mungu?”
Cross-references
148
- 1Isa 38:1–8, 2Ch 32:24, 2Ki 20:1–11, 2Sa 17:23, Jon 3:10, Act 9:37, Php 2:27–30, Isa 37:21
- 2Mat 6:6, 1Ki 8:30, Psa 50:15, Psa 91:15
- 3Heb 5:7, Heb 6:10, Psa 18:20–27, Neh 13:14, 2Ch 31:20–21, 2Co 1:12, Neh 13:22, Neh 5:19
- 5Psa 34:5–6, 1Jn 5:14–15, Rev 7:17, Luk 1:13, Psa 147:3, Psa 56:8, 2Ki 19:20, 2Co 7:6
- 6Isa 37:35, Isa 12:6, Isa 31:4–5, 2Ch 32:22, 2Ti 4:17
- 7Isa 37:30, Jdg 6:37–39, Isa 7:11–14, Jdg 6:17–22, 2Ki 20:8–21, Gen 9:13, Isa 38:22
- 82Ki 20:9–11, Jos 10:12–14, 2Ch 32:24, Mat 16:1, 2Ch 32:31
- 91Sa 2:1–10, Jon 2:1–9, Psa 116:1–4, Psa 18:1, Psa 30:11–12, 2Ch 29:30, Jdg 5:1–31, Deu 32:39
- 10Psa 102:24, 2Co 1:9, Psa 107:18, Job 7:7, Job 17:11–16, Isa 38:1, Job 6:11
- 11Psa 27:13, Psa 116:8–9, Psa 31:22, Ecc 9:5–6, Job 35:14–15, Psa 6:4–5
- 12Heb 1:12, 2Co 5:1, Psa 73:14, Isa 13:20, Isa 1:8, Psa 102:11, Job 6:9, Psa 31:22
- 13Dan 6:24, Psa 51:8, Psa 39:10, 1Co 11:30–32, 1Ki 13:24–26, Job 16:12–14, Job 10:16–17, Hos 5:14
- 14Isa 59:11, Psa 69:3, Job 30:29, Nam 2:7, Psa 123:1–4, Ezk 7:16, Psa 119:122–123, Job 17:3
- 151Ki 21:27, Job 7:11, Job 10:1, Jhn 12:27, 1Sa 1:10, Jos 7:8, Ezr 9:10, Psa 39:9–10
- 161Co 11:32, Heb 12:10–11, Mat 4:4, Psa 119:25, Job 33:19–28, Isa 64:5, Deu 8:3, 2Co 4:17
- 17Isa 43:25, Jon 2:6, Mic 7:18–19, Psa 30:3, Jer 31:34, Psa 86:13, Psa 40:2, Psa 85:2
- 18Ecc 9:10, Psa 6:5, Psa 30:9, Psa 115:17–18, Psa 88:10–11, Num 16:33, Luk 16:26–31, Mat 25:46
- 19Deu 6:7, Psa 119:175, Psa 78:3–6, Deu 4:9, Gen 18:19, Exo 12:26–27, Jos 4:21–22, Deu 11:19
- 20Psa 116:2, Psa 150:4, Psa 145:2, Psa 30:11–12, Psa 51:15, Psa 33:2, Psa 66:13–15, Hab 3:19
- 212Ki 20:7–8, Jhn 9:6, Mrk 7:33
- 222Ki 20:8, Jhn 5:14, Psa 118:18–19, Psa 122:1, Psa 84:1–2, Psa 42:1–2, Psa 84:10–12
Parallel passages
1
- Hezekiah's Illness2Ki 20:1–11, Isa 38:1–8
Topics in this chapter
44
Afflictions and Adversities, Ahaz, Boil, Corruption, Crane, Death, Dial, Disease, Faith, Fig, Gates, God, Harp, Hezekiah, Hope, Humility, Immortality, Instruction, Isaiah, Life, Lion, Medicine, Miracles, Murmuring, Obedience, Oppression, Parents, Praise, Prayer, Prophecy, Psalms, Repentance, Sincerity, Sun, Sun-Dial, Swallow, Symbols and Similitudes, Tears, Tent, Time, Truth, Weaving, Weeping, Worship