2 Yohana 1
1 Mzee.
2 kwa sababu ya ile kweli inayokaa ndani yetu, na ambayo itaendelea kukaa nasi milele.
3 Neema, rehema na amani zinazotoka kwa Mungu Baba Mwenyezi na kwa Isa Al-Masihi, Mwanawe Baba, zitakuwa pamoja nasi katika kweli na upendo.
4 Imenipa furaha kuu kuona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile Baba alivyotuagiza.
5 Sasa, mama mteule mpendwa, si kwamba ninakuandikia amri mpya, bali ile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo. Tupendane kila mmoja na mwenzake.
6 Hili ndilo pendo: kwamba tuenende kwa kuzitii amri zake. Hii ndiyo amri yake kama vile mlivyosikia tangu mwanzo, kwamba mwenende katika upendo.
7 Wadanganyifu wengi, wasiokubali kwamba Isa Al-Masihi amekuja katika mwili, wametawanyika ulimwenguni. Mtu kama huyo ni mdanganyifu na anampinga Al-Masihi.
8 Jihadharini msije mkapoteza kile mlichokitenda, bali mpate kupewa thawabu kamilifu.
9 Mtu yeyote asiyedumu katika mafundisho ya Al-Masihi bali ameyaacha, yeye hana Mungu. Yeyote anayedumu katika mafundisho ana Baba na Mwana pia.
10 Msimpokee mtu yeyote anayewajia ambaye hawaletei mafundisho haya, wala msimkaribishe nyumbani mwenu.
11 Yeyote amkaribishaye mtu kama huyo anashiriki katika matendo yake maovu.
12 Ninayo mengi ya kuwaandikia, lakini sitaki kutumia karatasi na wino. Badala yake, nataraji kuja kwenu na kuongea nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ipate kuwa timilifu.
13 Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu. Amen.
Cross-references
94
- 11Ti 2:4, Jhn 8:32, 1Jn 3:18, 1Pe 1:22–23, 1Pe 5:1, 2Jn 1:5, 2Jn 1:13–15, 1Jn 2:21
- 21Jn 2:14, 1Jn 1:8, 1Jn 2:17, 1Pe 1:23–25, Jhn 15:7, 2Pe 1:12, Col 3:16, 2Ti 1:5
- 3Rom 1:7, 1Jn 4:10, 1Ti 1:2, 1Ti 1:14, Gal 5:6, 2Jn 1:1, 2Ti 1:13, 1Jn 2:23–24
- 43Jn 1:3–4, Eph 5:8, 1Jn 2:6, Hos 14:9, Eph 5:2, 1Jn 1:6–7, Mal 2:6, 1Th 3:6–10
- 5Jhn 15:12, 1Jn 3:11, Jhn 13:34–35, 1Th 4:9, 1Jn 3:23, 1Jn 4:20, 1Pe 4:8, 1Jn 3:14–18
- 61Jn 5:3, Jhn 15:10, 1Jn 2:24, Jhn 14:15, Gal 5:13–14, 1Jn 2:5, Jhn 15:14, Rom 13:8–9
- 71Jn 4:1–3, 1Jn 2:26, 1Jn 2:18–22, 2Pe 2:1–3, 1Ti 3:16, Jhn 1:14, Rev 13:14, Rev 12:9
- 8Heb 10:35, Rev 3:11, 1Co 3:14, 1Co 3:8, Heb 12:15, Gal 3:4, Jhn 4:36, Mrk 13:9
- 9Jhn 7:16–17, Col 3:16, 1Jn 2:22–24, 1Jn 1:3, Jhn 15:6, Jhn 14:6, Jhn 5:23, Act 2:42
- 10Tit 3:10, Rom 16:17–18, 2Th 3:6, 2Ti 3:5–6, 2Th 3:14, 1Co 5:11, 2Jn 1:11, 1Co 16:22
- 111Ti 5:22, Eph 5:11, Psa 50:18, Rev 18:4
- 12Jhn 16:12, 3Jn 1:13–14, Num 12:8, Jhn 17:13, 1Jn 1:4, Jhn 15:11, 1Co 16:5–7, Rom 15:24
- 132Jn 1:1–13, 1Pe 5:13
Topics in this chapter
28
Antichrist, Backsliders, Benedictions, Church, Commandments, Company, Complicity, Deceit, Decision, Doctrines, Elder, Fellowship, God, Heresy, Holiness, Ink, Jesus, the Christ, John, Love, Minister, Christian, Obedience, Paper, Particeps Criminis, Righteous, Righteousness, Salutations, Truth, Watchfulness