Yoshua 16
1 Mgawanyo wa Yusufu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
2 Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waarki huko Atarothi,
3 ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
4 Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yusufu, walipokea urithi wao.
5 Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, kufuatana na koo zao: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
6 na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
7 Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
8 Kutoka Tapua, mpaka ulienda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, kufuatana na koo zao.
9 Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
10 Hawakuwatoa Wakanaani walioishi Gezeri; hadi leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu, lakini wanatumikishwa kwa kazi ngumu.
Cross-references
39
- 1Jos 18:12, Jos 8:15, 2Ki 2:19–21, Jos 15:61
- 2Jos 18:13, Gen 28:19, 2Sa 16:16, Jdg 1:22–26, 1Ch 27:33
- 3Jos 10:33, Jos 18:13, 2Ch 8:5, 1Ki 9:15–17, Num 34:6, 1Ch 7:24, 1Ch 7:28
- 4Jos 17:14
- 5Jos 18:13, Jos 16:2
- 6Jos 17:7, Jos 18:1
- 71Ch 7:28, Jos 6:26, Jos 3:16, Num 33:48, Jos 6:1
- 8Jos 17:8–9, Jos 16:3–6, Num 34:6, Jos 12:17, Jos 19:28
- 9Jos 17:9
- 10Jdg 1:29, Deu 7:1–2, Jos 17:13, 1Ki 9:16, 1Ki 9:21, Num 33:52–55, Jos 15:63