Kumbukumbu La Torati 25
1 Watu wanapokuwa na ugomvi, wapeleke mahakamani na waamuzi wataamua shauri hilo; watawaachia wasio na kosa na kuwahukumu wenye hatia.
2 Kama mtu mwenye hatia anastahili kupigwa, mwamuzi atamwamuru alale chini ili apigwe mbele yake idadi ya mijeledi kulingana na kosa lake,
3 lakini kamwe asipigwe zaidi ya mijeledi arobaini. Akipigwa zaidi ya mijeledi arobaini, nduguyo atadhalilika machoni pako.
4 Usimfunge maksai kinywa anapopura nafaka.
5 Ikiwa ndugu wanaishi pamoja, naye mmoja wao akafa bila kuacha mwana, kamwe mjane wake asiolewe nje ya jamaa hiyo. Ndugu wa mumewe atamchukua, amwoe na kutimiza wajibu wa shemeji kwake.
6 Mwana wa kwanza atakayemzaa atapewa jina la ndugu aliyekufa ili jina lake lisifutike katika Israeli.
7 Hata hivyo, ikiwa ndugu huyo wa mume hataki kuoa huyo mke wa nduguye, mjane atawaendea wazee kwenye lango la mji na kusema, “Ndugu wa mume wangu anakataa kuendeleza jina la nduguye katika Israeli. Hataki kutimiza wajibu wa shemeji kwangu.”
8 Ndipo wazee wa mji wake watamwita na kuzungumza naye. Kama atashikilia kukataa akisema, “Sitaki kumwoa,”
9 mjane wa nduguye atamwendea mbele ya wazee, atamvua kiatu kimoja na kumtemea mate usoni, na kusema, “Hivi ndivyo ambavyo hufanywa kwa mtu ambaye atakataa kuendeleza jamaa ya ndugu yake.”
10 Jamaa ya mtu huyo itafahamika katika Israeli kama Jamaa ya Aliyevuliwa Kiatu.
11 Ikiwa watu wawili wanapigana na mke wa mmoja wao akaja kumwokoa mumewe na yule anayemshambulia, naye mke huyo akifika na kumkamata sehemu za siri,
12 huyo mwanamke utamkata mkono wake. Usimhurumie.
13 Usiwe na mawe ya kupimia ya aina mbili katika mkoba wako, moja zito na jingine jepesi.
14 Usiwe na vipimo viwili tofauti katika nyumba yako, kimoja kikubwa, kingine kidogo.
15 Ni lazima uwe na uzito na vipimo sahihi na vya haki, ili upate kuishi maisha marefu katika nchi anayokupa Mwenyezi Mungu, Mungu wako.
16 Kwa maana Mwenyezi Mungu, Mungu wako, humchukia yeyote ambaye hufanya mambo kama haya, yeyote anayetenda kwa udanganyifu.
17 Kumbuka kile Waamaleki walichowatendea mlipokuwa njiani mkitoka Misri.
18 Mlipokuwa mmechoka na kuishiwa nguvu kwa safari yenu, waliwalaki njiani, wakawapiga wale wote waliokuja nyuma. Waamaleki hawakumwogopa Mungu.
19 Mwenyezi Mungu, Mungu wako, atakapokupa pumziko mbali na adui zako wote wanaokuzunguka katika nchi anayokupa kuimiliki kuwa urithi, utafutilia mbali kumbukumbu lote la Waamaleki chini ya mbingu. Usisahau!
Cross-references
93
- 1Pro 17:15, Deu 17:8–9, Deu 1:16–17, Isa 1:17, Mat 3:10, Deu 16:18–20, Pro 31:8–9, Jer 21:12
- 2Luk 12:47–48, Mat 27:26, 1Pe 2:24, Act 5:40, Mat 10:17, 1Pe 2:20, Act 16:22–24
- 3Job 18:3, Jas 2:2–3, Luk 15:30, 2Co 11:24–25, Luk 18:9–12
- 41Ti 5:17–18, 1Co 9:9–10, Pro 12:10, Hos 10:11, Isa 28:27
- 5Mat 22:24, Luk 20:28, Mrk 12:19, Gen 38:8–9, Rut 1:12–13, Rut 3:9, Rut 4:5
- 6Psa 9:5, Psa 109:13, Deu 21:19, Deu 29:20, Gen 28:8–10, Rut 4:10–12, Deu 9:14, Rut 4:1–7
- 7Rut 4:1–2, Rut 4:5–6
- 8Rut 4:6
- 9Rut 4:7–8, Num 12:14, Mat 27:30, Jhn 1:27, Mrk 1:7, Mat 26:67, Rut 4:10–11, Isa 20:2
- 12Deu 19:13, Deu 7:2, Deu 19:21
- 13Pro 11:1, Lev 19:35–37, Pro 16:11, Amo 8:5, Mic 6:11–12, Pro 20:10, Ezk 45:10–11
- 15Exo 20:12, Deu 4:40, 1Pe 3:10, Deu 11:9, Deu 5:16, Psa 34:12, Deu 6:18, Deu 5:33
- 16Pro 11:1, Rev 21:27, Deu 22:5, Amo 8:5–7, 1Co 6:9–11, 1Th 4:6, Deu 18:12, Pro 20:23
- 17Exo 17:8–16, Num 25:17–18, Num 24:20
- 18Rom 3:18, Psa 36:1, Neh 5:15, Neh 5:9, Pro 16:6
- 19Exo 17:14, Exo 17:16, Deu 9:14, 1Sa 14:48, Jos 23:1, 1Sa 15:1–35, Psa 83:7–17, Jos 7:22–25
Topics in this chapter
33
Abomination, Amalekites, Animals, Beating, Brother, Bullock, Court, Dishonesty, Forty, Government, Honesty, Inheritance, Israel, Judge, Justice, Labor, Marriage, Measure, Pity, Punishment, Quotations and Allusions, Retaliation, Reward, Rulers, Scourging, Shoe, Sin, Spitting, Strangers, Threshing, Wages, Weights, Widow