Nehemia 2
1 Katika mwezi wa Nisani, mwaka wa ishirini wa utawala wa Mfalme Artashasta, wakati divai ilipoletwa kwake, niliichukua na kumpa mfalme. Sikuwahi kuonekana mwenye huzuni mbele yake kabla ya hapo.
2 Basi mfalme akaniuliza, “Kwa nini uso wako unaonekana una huzuni wakati wewe si mgonjwa? Jambo hili si kitu kingine bali ni huzuni ya moyo.” Niliogopa sana,
3 lakini nikamwambia mfalme, “Mfalme na aishi milele! Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni wakati mji walipozikwa baba zangu umebaki magofu, na malango yake yameteketezwa kwa moto?”
4 Mfalme akaniambia, “Je, haja yako ni nini?” Ndipo nikaomba kwa Mungu wa mbinguni,
5 na nikamjibu mfalme, “Ikimpendeza mfalme, na kama mtumishi wako amepata kibali machoni pake, anitume kule mji wa Yuda, mahali baba zangu walipozikwa, ili niweze kuujenga upya.”
6 Kisha mfalme, huku malkia akiwa ameketi karibu naye, akaniuliza, “Safari yako itachukua muda gani, nawe utarudi lini?” Ilimpendeza mfalme kunituma, kwa hiyo nikapanga muda.
7 Pia nikamwambia, “Ikimpendeza mfalme, naomba nipewe barua kwa watawala wa Ng’ambo ya Frati, ili wanipe ulinzi hadi nifike Yuda.
8 Naomba nipewe barua nipeleke kwa Asafu, mtunzaji wa msitu wa mfalme, ili anipe miti ya kutengeneza boriti kwa ajili ya malango ya ngome ya Hekalu, na ukuta wa mji, na makao yangu nitakayoishi.” Kwa kuwa mkono wenye neema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu, mfalme akanijalia ombi langu.
9 Basi nilienda kwa watawala wa Ng’ambo ya Frati na kuwapa barua za mfalme. Pia mfalme alikuwa ametuma maafisa wa jeshi na askari wapanda farasi pamoja nami.
10 Sanbalati Mhoroni na Tobia afisa Mwamoni waliposikia kuhusu jambo hili, waliudhika sana kwamba amekuja mtu kuinua ustawi wa Waisraeli.
11 Nilienda Yerusalemu, na baada ya kukaa huko siku tatu,
12 nikaondoka wakati wa usiku pamoja na watu wachache. Sikuwa nimemwambia mtu yeyote kile ambacho Mungu wangu alikuwa ameweka moyoni mwangu kufanya kwa ajili ya Yerusalemu. Hapakuwa na mnyama yeyote nami isipokuwa yule niliyekuwa nimempanda.
13 Nikatoka nje usiku kupitia Lango la Bondeni, kuelekea Kisima cha Joka na Lango la Samadi, nikikagua kuta za Yerusalemu zilizokuwa zimebomolewa, na malango yake yaliyokuwa yameteketezwa kwa moto.
14 Kisha nikaelekea hadi Lango la Chemchemi na Bwawa la Mfalme, lakini hapakuwa na nafasi ya kutosha mnyama wangu kupita,
15 kwa hiyo nikapandia bondeni usiku nikikagua ukuta. Mwishoni nikarudi na kuingia tena kupitia Lango la Bondeni.
16 Maafisa hawakujua nilikoenda wala nilichokuwa nikifanya, kwa sababu nilikuwa bado sijasema lolote kwa Wayahudi, wala makuhani, wala wakuu, wala maafisa, wala mtu yeyote ambaye angefanya kazi.
17 Ndipo nilipowaambia, “Mnaona taabu tuliyo nayo: Yerusalemu imebaki magofu na malango yake yameteketezwa kwa moto. Njooni tujenge upya ukuta wa Yerusalemu, nasi hatutakuwa tena katika aibu hii.”
18 Pia niliwaambia kuhusu mkono wenye neema wa Mungu wangu uliokuwa juu yangu, na kile mfalme alichokuwa ameniambia. Wakajibu, “Haya! Tuanze kujenga tena.” Kwa hiyo wakaanza kazi hii njema.
19 Lakini Sanbalati Mhoroni, Tobia afisa Mwamoni, na Geshemu Mwarabu waliposikia kuhusu jambo hili, walitudhihaki na kutucheka. Wakauliza, “Ni nini hiki mnachokifanya? Je, mnaasi dhidi ya mfalme?”
20 Nikawajibu kwa kusema, “Mungu wa mbinguni atatufanikisha. Sisi watumishi wake tutaanza kujenga upya, lakini ninyi hamna sehemu wala dai lolote, wala kumbukumbu la haki katika Yerusalemu.”
Cross-references
116
- 1Ezr 7:1, Neh 1:11, Neh 1:1, Est 3:7, Ezr 7:7
- 2Pro 15:13, Gen 40:7
- 3Neh 1:3, 1Ki 1:31, Dan 2:4, Psa 137:6, Dan 5:10, 2Ch 28:27, Lam 2:9, Dan 6:6
- 4Php 4:6, Pro 3:6, Neh 1:4, Neh 1:11, Mrk 10:51, 1Ki 3:5, Est 5:6, Est 7:2
- 5Rut 2:13, 2Sa 14:22, Est 7:3, Est 8:5, Est 5:8, Ezr 5:17, Pro 3:4, Est 1:19
- 6Neh 13:6, Isa 65:24, Neh 5:14, Isa 58:12, Neh 2:4, Isa 61:4, Neh 1:11
- 7Ezr 7:21, Neh 2:9, Ezr 8:36, Ezr 6:6, Ezr 8:22
- 8Ezr 7:6, Isa 66:14, Neh 7:2, Dan 1:9, Neh 2:17–18, Ezr 5:5, Gen 32:28, Act 7:10
- 9Ezr 8:22
- 10Neh 2:19, Neh 4:7, Neh 6:1, Neh 13:4, Pro 27:4, Ezk 25:6–8, Act 19:26–27, Neh 4:1–3
- 11Ezr 8:32
- 12Rev 17:17, Ezr 7:27, Jer 31:33, 2Co 8:16, Jer 32:40, Jas 1:16–17, Psa 51:18, Jdg 9:32
- 13Neh 1:3, Neh 2:3, Neh 2:17, 2Ch 26:9, Neh 3:13–14, Neh 2:15, Neh 12:31, Jer 5:10
- 14Neh 3:15, 2Ki 20:20, 2Ch 32:30, 2Ki 18:17
- 152Sa 15:23, Jhn 18:1, Jer 31:38–40
- 17Ezk 5:14, Isa 35:3–4, Lam 3:45–46, Lam 3:51, Psa 79:4, Neh 1:3, Psa 89:50–51, Ezk 22:4–5
- 18Php 2:13, 2Ch 32:5, Eph 6:10, 1Ch 19:13, Hag 1:13–14, 2Sa 2:7, Ezr 6:22, 1Ch 11:10
- 19Neh 6:6, Neh 6:1–2, Psa 44:13–14, Psa 80:6, Mrk 5:40, Heb 11:36, Jer 20:8, Psa 79:4
- 20Act 8:21, Ezr 4:3, Neh 2:4, Isa 56:5, Act 10:31, Psa 35:27, Ecc 7:18, Psa 20:5
Topics in this chapter
32
Arabians, Artaxerxes, Asaph, Blessing, Butler, Cedron, Character, Countenance, Country, Faith, Geshem, Gihon, Government, Hezekiah, Horonite, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Kidron, Letters, Malice, Month, Nehemiah, Passports, Patriotism, Persia, Prayer, Prudence, Queen, Rulers, Sanballat, Tobiah, Women