Ufunuo 15
1 Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
2 Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
3 Nao wakaimba wimbo wa Musa, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
4 Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Mwenyezi Mungu na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
5 Baada ya haya nikatazama, nalo Hekalu la Hema la Ushuhuda lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
6 Ndani ya lile Hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani iliyong’aa, na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
7 Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele.
8 Nalo lile Hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle Hekaluni hadi yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.
Cross-references
60
- 1Lev 26:21, Rev 15:6–7, Rev 21:9, Dan 4:2–3, Rev 19:15, Dan 12:6–7, Mat 13:41–42, Dan 6:27
- 2Rev 4:6, Rev 12:11, Rev 19:1–7, Rev 5:8, 1Pe 1:7, Rev 21:18, Mat 3:11, Rev 13:14–14:5
- 3Psa 111:2, Exo 15:1–18, Psa 139:14, Rev 5:9–13, Psa 145:17, Isa 33:22, Heb 3:5, Hos 14:9
- 4Psa 86:9, Mal 1:11, Jer 10:7, Psa 22:27, Rev 11:15, Rev 14:7, Isa 66:22–23, Zec 14:16
- 5Rev 11:19, Num 1:50, Mat 27:51, Num 1:53, Exo 38:21, Exo 25:21
- 6Rev 1:13, Rev 15:1, Ezk 44:17–18, Exo 28:5–8, Rev 14:15, Luk 24:4
- 7Rev 5:8, Rev 10:6, Rev 16:2–17:1, Rev 21:9, Rev 15:1, Jer 25:15, Psa 75:8, Rev 4:6–9
- 8Isa 6:4, 1Ki 8:10–11, Exo 40:34–35, 2Ch 5:13–14, 2Th 1:9, Psa 29:9, Rev 15:1, Psa 18:8–14