Kumbukumbu La Torati 13
1 Kama nabii, au yule anayetabiri kupitia ndoto, akijitokeza miongoni mwenu na akawatangazia ishara ya miujiza na ajabu,
2 ikiwa ishara au ajabu ya aliyozungumza ikatokea, naye akasema, “Na tufuate miungu mingine” (miungu ambayo hamjaifahamu) “na tuiabudu,”
3 kamwe msiyasikilize maneno ya nabii wala mwota ndoto huyo. Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawajaribu kuangalia kama mnampenda kwa moyo wote na kwa roho yote.
4 Ni Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambaye mnapaswa kumfuata tena ni yeye mnapaswa kumheshimu. Shikeni maagizo yake na kumtii, mtumikieni na kushikamana naye.
5 Huyo nabii au mwota ndoto lazima auawe, kwa sababu amehubiri uasi dhidi ya Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambaye aliwatoa kutoka nchi ya Misri na kuwakomboa kutoka nchi ya utumwa; amejaribu kuwageuza kutoka njia ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, aliwaagiza mfuate. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu.
6 Kama ndugu yako hasa, au mwanao au binti yako, au mke umpendaye, au rafiki yako wa karibu sana akikushawishi kwa siri, akisema, “Na twende tukaabudu miungu mingine” (miungu ambayo ninyi wala baba zenu hamkuifahamu,
7 miungu ya watu wanaowazunguka, ikiwa karibu au mbali, kutoka mwisho mmoja wa nchi hadi mwingine),
8 usikubali wala usimsikilize. Usimhurumie! Usimwache wala usimkinge.
9 Hakika ni lazima auawe. Ni lazima mkono wako uwe wa kwanza katika kumuua kisha mikono ya watu wengine wote.
10 Mpigeni kwa mawe hadi afe, kwa sababu alijaribu kuwageuza mtoke kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, ambaye aliwatoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.
11 Kisha Israeli wote watasikia na kuogopa, wala hakuna mmoja miongoni mwenu atakayefanya uovu tena.
12 Mkisikia ikisemwa kwamba moja ya miji ambayo Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, anawapa mkae ndani yake
13 kuna wanaume waovu wameinuka miongoni mwenu na wamewapotosha watu wa mji, wakisema, “Twendeni tukaabudu miungu mingine” (miungu ambayo hamkuifahamu),
14 ndipo itakubidi kuuliza, kupima na kuchunguza kwa makini. Kama ni kweli, tena ikihakikishwa kwamba jambo hili linalochukiza limefanyika miongoni mwenu,
15 kwa hakika ni lazima mwaue kwa upanga wale wote wanaoishi katika mji ule. Uharibuni kabisa, pamoja na watu wake na mifugo yake.
16 Kusanyeni nyara zote za mji katika uwanja wa wazi na kuuchoma mji kabisa pamoja na nyara zake zote kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Mwenyezi Mungu, Mungu wenu. Utabaki kuwa magofu milele na hautajengwa tena.
17 Hakuna kimoja kati ya vitu vilivyolaaniwa kitakachokutwa mikononi mwenu, ili Mwenyezi Mungu ageuze hasira yake kali. Atawahurumia na kuwa na rehema kwenu pia kuongeza idadi yenu, kama alivyowaahidi baba zenu,
18 kwa sababu mnamtii Mwenyezi Mungu, Mungu wenu, mkizishika amri zake zote ninazowapa leo na kufanya lililo jema machoni pake.
Cross-references
121
- 1Jer 23:25–28, 1Jn 4:1, Jer 29:8, 1Ki 13:18, Jer 27:9, Isa 9:15, Luk 6:26, 2Th 2:9
- 2Mat 7:22–23, Rev 13:13–14, Mat 24:24, 2Co 11:13–15, Deu 13:6, Deu 18:22, 2Th 2:9–11, Jer 28:9
- 3Deu 8:2, 1Co 11:19, Psa 66:10, 1Jn 4:1, Deu 6:5, Isa 8:20, 2Th 2:11, Mat 24:24
- 4Col 1:10, Deu 10:20, 1Co 6:17, Jer 7:23, 2Ki 23:3, 2Ch 34:31, Deu 30:20, Mic 6:8
- 51Co 5:13, Deu 18:20, Jer 14:15, Deu 17:7, Deu 22:21, Deu 19:19, Deu 24:7, Deu 13:10
- 6Deu 17:2–7, 2Pe 2:1, 1Jn 2:26–27, Eph 4:14, Mic 7:5–7, Pro 18:24, Rev 20:3, Mat 12:48–50
- 8Pro 1:10, Deu 19:13, Deu 7:16, Ezk 9:5–6, 1Jn 5:21, Exo 20:3, Ezk 5:11, Gal 1:8–9
- 9Jhn 8:7, Act 7:58, Deu 17:2–7, Mat 10:37, Luk 14:26
- 10Jos 7:25, 2Ch 24:21, Lev 20:2, Lev 24:23, Num 15:35–36, Lev 24:14–16, Lev 20:27, Exo 20:2
- 11Deu 19:20, Deu 17:13, 1Ti 5:20, Pro 19:25, Pro 21:11
- 12Jos 22:11–34, Jdg 20:1–17
- 131Jn 2:19, 2Co 6:15, Deu 13:6, Deu 13:2, Jud 1:19, Jhn 8:44, 2Sa 23:6, 1Ki 21:10
- 14Deu 17:4, Isa 11:3–4, Jhn 7:24, 1Ti 5:19, Num 35:30, Deu 10:18
- 15Lev 27:28, Deu 7:2, Exo 22:20, Jdg 20:48, Deu 2:34, Rev 17:16, Rev 19:2–3, Rev 18:18–24
- 16Jer 49:2, Jos 8:28, Isa 17:1, Jos 6:24, Isa 25:2, Jos 6:26, Mic 1:6, Num 21:2–3
- 17Jos 7:26, Gen 26:4, Gen 26:24, Deu 7:26, Deu 30:3, Gen 28:14, Jos 6:18, Jos 7:1
- 18Deu 12:28, Mat 7:21, Mat 7:24, Deu 12:25, Mat 6:33, Deu 12:32, Psa 119:6