Yohana 13
1 Sikukuu ya Pasaka ilikuwa imekaribia. Isa alijua kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni; naam, aliwapenda hadi mwisho.
2 Isa alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia wazo la kumsaliti Isa ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
3 Isa, akijua kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
4 aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
7 Isa akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Isa akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.”
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
10 Isa akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi. Akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana’; hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri kwenu mkiyatenda.
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni kutimiza andiko lisemalo, ‘Yeye aliyekula chakula changu ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
21 Baada ya kusema haya, Isa alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
23 Mmoja wa wanafunzi wake, ambaye Isa alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Isa.
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Isa, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
26 Isa akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Isa akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda, litende haraka.”
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Isa alimwambia hivyo.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Isa alikuwa anamwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini kitu.
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Isa akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe, naye atamtukuza mara moja.
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi: Niendako, ninyi hamwezi kuja.
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane. Kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
35 Mkipendana ninyi kwa ninyi kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unaenda wapi?” Isa akamjibu, “Ninakoenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
38 Isa akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Querverweise
254
- 1Jhn 12:23, 1Jn 4:19, Jhn 13:34, Jhn 16:28, Jhn 13:3, Rev 1:5, Jhn 18:4, Eph 5:25–26
- 2Jas 1:13–17, Act 5:3, Jhn 13:26–27, Luk 22:31, Jhn 6:70–71, Luk 22:3, Rev 17:17, 2Co 8:16
- 3Jhn 3:35, Mat 11:27, Heb 1:2, Mat 28:18, Jhn 8:42, Jhn 17:2, Php 2:9–11, Jhn 16:27–28
- 42Co 8:9, Luk 22:27, Php 2:6–8, Luk 12:37, Luk 17:7
- 5Luk 7:44, Psa 51:2, 1Ti 5:10, Gen 19:2, Gen 18:4, Tit 3:3–5, 2Ki 3:11, Rev 7:14
- 6Mat 3:11–14, Jhn 1:27, Luk 5:8
- 7Dan 12:8, Jhn 12:16, Jhn 14:26, Jas 5:7–11, Jhn 13:10–12, Jhn 13:36, Dan 12:12, Hab 2:1–3
- 8Act 22:16, Tit 3:5, Ezk 36:25, Heb 10:22, Eph 5:26, 1Co 6:11, Rev 7:14, Col 2:23
- 9Psa 51:2, Psa 51:7, Psa 26:6, 1Pe 3:21, Heb 10:22, Mat 27:24, Jer 4:14
- 10Jhn 15:3, 2Co 7:1, 2Co 5:17, Num 19:19–21, Eph 5:26–27, Lev 17:15–16, Num 19:12–13, Lev 16:26
- 11Jhn 13:26, Jhn 13:18, Jhn 13:21, Jhn 13:2, Jhn 6:64–71, Jhn 2:25, Mat 26:24–25, Jhn 17:12
- 12Jhn 13:7, Ezk 24:24, Jhn 13:4, Mat 13:51, Ezk 24:19
- 13Luk 6:46, 1Co 12:3, Php 2:11, Jhn 11:28, Rom 14:8–9, Jas 2:19, Mat 23:8–10, Php 3:8
- 141Pe 5:5, Act 20:35, Rom 12:16, Gal 5:13, Luk 22:26–27, Mrk 10:43–45, 1Pe 4:1, Heb 5:8–9
- 15Mat 11:29, 1Jn 2:6, 1Pe 3:17–18, 1Pe 2:21, Eph 5:2, Rom 15:5
- 16Jhn 15:20, Luk 6:40, Mat 10:24–25, Jhn 3:5, Jhn 3:3
- 17Luk 11:28, Jas 4:17, Jas 1:25, Mat 7:24–25, Luk 12:47–48, Ezk 36:27, Exo 40:16, Psa 19:11
- 18Psa 41:9, Mat 26:23, Jhn 17:12, Mrk 14:20, Jhn 13:26, Jhn 13:10–11, Jhn 6:70, Jhn 15:19
- 19Isa 43:10, Jhn 14:29, Jhn 16:4, Rev 1:17–18, Jhn 8:23–24, Isa 48:5, Mat 24:25, Jhn 8:58
- 20Luk 10:16, Luk 9:48, Mat 25:40, Mrk 9:37, Mat 10:40–42, Gal 4:14, Jhn 12:44–48, Col 2:6
- 21Mat 26:21, Jhn 13:18, Mrk 14:18, Luk 22:21–22, Act 1:16–17, Jhn 12:27, 2Co 2:12–13, Jhn 11:33
- 22Luk 22:23, Mrk 14:19, Mat 26:22, Gen 42:1
- 23Jhn 19:26, Jhn 20:2, Jhn 21:7, Jhn 21:20, Rev 1:16–18, 2Sa 12:3, Jhn 21:24, Jhn 13:25
- 24Act 13:16, Act 12:17, Luk 1:22, Luk 5:7, Act 21:40
- 25Jhn 21:20, Est 7:5, Gen 44:4–12
- 26Mat 26:23, Jhn 13:30, Mrk 14:19–20, Luk 22:21, Jhn 6:70–71, Jhn 12:4–6
- 27Luk 22:3, Jhn 13:2, Mat 12:45, Pro 1:16, Jas 1:13–15, Act 5:3, Ecc 9:3, Jer 2:24–25
- 29Act 20:34–35, Eph 4:28, Jhn 12:5–6, Jhn 13:1, Gal 2:10
- 30Isa 59:7, Pro 4:16, Rom 3:15, Job 24:13–15, Luk 22:53
- 311Pe 4:11, Jhn 14:13, Jhn 7:39, Jhn 16:14, 1Pe 1:21, Eph 3:10, Heb 5:5–9, Eph 1:5–8
- 32Rev 22:3, Rev 22:1, Jhn 17:1, Jhn 17:4–6, Isa 53:10–12, Jhn 12:23, Rev 3:21, 1Pe 3:22
- 33Jhn 7:33–34, Jhn 16:16–22, 1Jn 2:1, Jhn 8:21–24, Jhn 12:35–36, Jhn 14:4–6, Jhn 14:19, 1Jn 4:4
- 34Eph 5:2, Lev 19:18, Jhn 15:17, 1Pe 1:22, 1Jn 3:23, Gal 6:2, 1Co 12:26–27, 1Jn 4:21–5:1
- 351Jn 4:20–21, 1Jn 2:10, 1Jn 3:10–14, Jhn 17:21, 1Jn 2:5, Act 4:32–35, Gen 13:7–8, Act 5:12–14
- 362Pe 1:14, Jhn 21:21–22, Jhn 13:33, Jhn 14:2, Jhn 21:18–19, Jhn 14:4–5, Jhn 16:17
- 37Act 20:24, Act 21:13, Mrk 14:27–31, Jhn 21:15, Mat 26:31–35, Luk 22:31–34
- 38Luk 22:34, Mat 26:34, Mrk 14:30, Pro 16:18, Luk 22:56–62, Mat 26:69–75
Themen in diesem Kapitel
44
Ablution, Apostles, Betrayal, Church, Commandments, Confidence, Eating, Eucharist (the Lord's Supper), Example, Faith, False Confidence, Feasts, Feet, Fellowship, Foot, Fraternity, God, Gospel, Heart, Heaven, Humility, Ignorance, Jesus, the Christ, John, Judas (Jude), Love, Master, Minister, Christian, Obedience, Passover, Peter, Predestination, Presumption, Prophecy, Quotations and Allusions, Regeneration, Righteous, Righteousness, Satan, Servant, Simon, Sin, Towel, Traitor