Yohana 6
1 Baada ya haya, Isa alienda ng’ambo ya Bahari ya Galilaya (ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia).
2 Umati mkubwa wa watu waliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa.
3 Kisha Isa akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
4 Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
5 Isa alipotazama na kuona umati ule mkubwa wa watu wakimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”
6 Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.
7 Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”
8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia,
9 “Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa watu hawa wote?”
10 Isa akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi (palikuwa na wanaume wapatao elfu tano).
11 Ndipo Isa akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12 Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.”
13 Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.
14 Baada ya watu kuona muujiza ule Isa aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”
15 Isa akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.
16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.
17 Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Isa alikuwa hajajumuika nao.
18 Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19 Wanafunzi walipokuwa wameenda mwendo wa maili tatu au nne, walimwona Isa akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.
20 Lakini Isa akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”
21 Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.
22 Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ng’ambo waliona kwamba palikuwa na mashua moja tu, na kwamba Isa hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.
23 Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana Isa kumshukuru Mungu.
24 Mara wale watu wakatambua kwamba Isa hakuwa hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Isa.
25 Walipomkuta Isa ng’ambo ya bahari wakamuuliza, “Mwalimu, umefika lini huku?”
26 Isa akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27 Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba Mwenyezi amemtia muhuri.”
28 Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”
29 Isa akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”
30 Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?
31 Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’ ”
32 Isa akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Musa aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.
33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
34 Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”
35 Isa akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.
36 Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.
37 Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuza nje kamwe.
38 Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
39 Haya ndio mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
40 Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.”
41 Wayahudi wakaanza kunung’unika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
42 Wakasema, “Huyu si Isa, mwana wa Yusufu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
43 Hivyo Isa akawaambia, “Acheni kunung’unikiana ninyi kwa ninyi.
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
45 Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
46 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
47 Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele.
48 Mimi ni mkate wa uzima.
49 Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
50 Lakini hapa kuna mkate kutoka mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
51 Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”
52 Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
53 Hivyo Isa akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
54 Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho.
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56 Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
58 Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.”
59 Isa alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
60 Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
61 Isa alipojua kwamba wafuasi wake wananung’unika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
62 Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?
63 Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
64 Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Isa alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
65 Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
66 Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
67 Hivyo Isa akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
68 Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
69 Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
70 Ndipo Isa akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
71 (Hapa alikuwa anasema kuhusu Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Isa.)
Querverweise
485
- 1Mrk 6:31–44, Jhn 6:23, Luk 5:1, Mat 4:18, Jhn 21:1, Num 34:11, Mat 14:13–21, Luk 9:10–17
- 2Mat 4:24–25, Mat 12:15, Mat 15:30–31, Jhn 2:11, Mrk 6:33, Mat 14:14
- 3Jhn 6:15, Luk 9:28, Mat 14:23, Mat 15:29, Luk 6:12–13
- 4Jhn 2:13, Jhn 11:55, Deu 16:1, Jhn 5:1, Jhn 12:1, Jhn 13:1, Lev 23:7, Exo 12:6–14
- 5Luk 9:12–13, Mat 15:33, Jhn 4:35, Jhn 1:43, Mat 14:14–15, Mrk 6:34–35
- 6Gen 22:1, 2Ch 32:31, Deu 13:3, Deu 8:16, Deu 8:2, Deu 33:8
- 7Mrk 6:37, Num 11:21–22, Jhn 12:5, 2Ki 4:43, Mat 18:28
- 8Jhn 1:40–44, Mat 4:18
- 92Ki 4:42–44, Mat 14:17, Mrk 6:38, Luk 9:13, Psa 78:19, Mrk 8:19, Mat 16:9, 2Co 8:9
- 10Luk 9:14–16, Mat 14:18–19, Mrk 8:6–7, Mat 15:35–36, Mrk 6:39–41
- 111Th 5:18, Jhn 6:23, Rom 14:6, Mat 15:36, Luk 24:30, 1Ti 4:4–5, 1Co 10:31, Act 27:35
- 12Luk 1:53, Luk 9:17, Neh 9:25, Neh 8:10, Mrk 6:42–44, Mat 14:20–21, Mat 15:37–38, Pro 18:9
- 13Pro 11:24–25, 1Ki 7:15–16, 2Ki 4:2–7, 2Co 9:8–9, 2Ch 25:9, Php 4:19
- 14Deu 18:15–18, Mat 21:11, Act 7:37, Mat 11:3, Act 3:22–24, Gen 49:10, Jhn 1:21, Jhn 7:40
- 15Jhn 18:36, Jhn 7:3–4, Jhn 6:15–21, Luk 19:38, Mrk 11:9, Mrk 6:45–52, Mat 14:22–33, Jhn 2:24–25
- 17Mrk 6:45, Jhn 6:24–25, Jhn 2:12, Jhn 4:46
- 18Psa 135:7, Psa 107:25, Mat 14:24
- 19Mrk 6:47–49, Mat 14:25–26, Psa 93:4, Jhn 14:18, Job 9:8, Jon 1:13, Ezk 27:26, Luk 24:36–39
- 20Mat 14:27–31, Isa 43:1–2, Isa 44:8, Isa 41:10, Isa 41:14, Rev 1:17–18, Mrk 6:50, Psa 35:3
- 21Mrk 6:51, Mat 14:32–33, Rev 3:20, Psa 24:7–10, Sng 3:4
- 22Mrk 6:45, Mat 14:22, Jhn 6:15–21, Jhn 6:2
- 23Jhn 6:1, Jhn 6:11–12
- 24Jhn 6:17, Luk 8:40, Mrk 1:37, Mrk 6:53, Mat 14:34, Jhn 20:15, Jhn 6:59, Jhn 7:11
- 25Jhn 1:38–39, Mat 23:7
- 26Jas 4:3–4, Php 3:19, Php 2:21, Ezk 33:31, 1Ti 6:5, Act 8:18–21, Rom 16:18, Psa 106:12–14
- 27Col 3:2, Isa 55:2, Jhn 6:54, 2Ti 2:19, Rom 6:23, Jhn 6:40, Mat 6:19, Jhn 6:51
- 28Act 16:30, Act 9:6, Luk 10:25, Mat 19:16, Deu 5:27, Act 2:37, Mic 6:7–8, Jer 42:3–6
- 291Jn 3:23, Act 16:31, Jhn 3:36, Heb 5:9, 1Jn 5:1, Rom 4:4–5, Mrk 16:16, Jhn 5:39
- 30Jhn 12:37, 1Co 1:22, Jhn 10:38, Jhn 6:36, Mrk 15:32, Exo 4:8, Mrk 8:11, 1Ki 13:5
- 31Neh 9:15, Psa 105:40, Psa 78:24–25, Exo 16:4–15, Exo 16:35, Jhn 6:49, Num 11:6–9, Deu 8:3
- 32Jhn 15:1, Jhn 6:58, Exo 16:4, Jhn 6:33, Jhn 6:35, Jhn 6:41, Psa 78:23, Jhn 1:9
- 33Jhn 8:42, Jhn 17:8, Jhn 3:13, 1Jn 1:1–2, Jhn 6:50, Jhn 6:38, 1Ti 1:15, Jhn 16:28
- 34Jhn 4:15, Jhn 6:26, Psa 4:6
- 35Jhn 6:48–58, Isa 55:1–3, Rev 22:17, Jhn 6:41, Isa 49:10, Jhn 7:37–38, Rev 7:16, Mat 11:28
- 361Pe 1:8–9, Jhn 6:26, Jhn 12:37, Luk 16:31, Jhn 6:40, Jhn 6:30, Jhn 6:64, Jhn 15:24
- 37Mat 11:28, Jhn 6:39, Jhn 17:24, Jhn 10:28–29, Jhn 17:2, Jhn 17:6, Isa 55:7, 2Ti 2:19
- 38Jhn 5:30, Jhn 4:34, Php 2:7–8, Jhn 3:31, Psa 40:7–8, Jhn 6:33, Isa 53:10, Jhn 3:13
- 39Jhn 17:12, Jhn 6:40, Jhn 18:9, Jhn 6:54, Jhn 10:27–30, Jhn 6:44, Jud 1:1, Rom 8:11
- 40Jhn 5:24, Rom 6:23, Jhn 6:54, Jhn 11:25, Jhn 3:15–18, Jhn 4:14, Jhn 14:19, Jhn 1:14
- 41Jhn 6:51–52, Jhn 6:48, Jhn 6:33, Jhn 7:12, Jhn 6:60, Jhn 6:66, Jud 1:16, Luk 5:30
- 42Luk 4:22, Mrk 6:3, Mat 13:55–56, 1Co 15:47, Jhn 7:27–28, Rom 1:3–4, Jhn 6:38, Jhn 6:62
- 43Heb 4:13, Jhn 6:64, Jhn 16:19, Mrk 9:33, Mat 16:8
- 44Jhn 6:65, Mat 11:25–27, Jhn 6:39–40, Eph 2:4–10, Jhn 12:32, Mat 16:17, Jhn 6:45, Tit 3:3–5
- 45Isa 54:13, Jer 31:33–34, Heb 10:16, Heb 8:10–11, 1Th 4:9, Mic 4:2, Isa 2:3, Jhn 6:65
- 46Jhn 1:18, Jhn 7:29, Mat 11:27, Luk 10:22, 1Jn 4:12, 1Ti 6:16, Col 1:15, Jhn 14:9–10
- 47Jhn 3:36, Col 3:3–4, Jhn 5:24, Jhn 3:16, Rom 5:9–10, Jhn 6:54, Jhn 3:18, Jhn 6:40
- 48Jhn 6:51, 1Co 11:24–25, 1Co 10:16–17, Jhn 6:41, Jhn 6:33–35
- 49Jud 1:5, 1Co 10:3–5, Heb 3:17–19, Num 26:65, Zec 1:5, Jhn 6:31, Jhn 6:58
- 50Jhn 6:33, Rom 8:10, Jhn 6:58, Jhn 6:51, Jhn 8:51, Jhn 6:42, Jhn 3:13, Jhn 11:25–26
- 51Jhn 6:33, Luk 22:19, Heb 10:5–12, Tit 2:14, Jhn 3:13, Mat 20:28, Heb 10:20, 2Co 5:21
- 52Jhn 9:16, Jhn 10:19, Jhn 6:41, 1Co 2:14, Jhn 7:40–43, Act 17:32, Jhn 3:9, Jhn 3:4
- 531Jn 5:12, Mat 26:26–28, Jhn 6:55, Jhn 6:47, Jhn 15:4, Jhn 6:26–27, Jhn 3:3, Rev 2:17
- 54Jhn 6:39–40, Php 3:7–10, Gal 2:20, Jhn 6:27, Pro 9:4–6, Psa 22:26, Jhn 4:14, Isa 55:1–3
- 55Jhn 6:32, Jhn 8:31, Jhn 8:36, Jhn 1:9, Jhn 15:1, 1Jn 5:20, Jhn 1:47, Psa 4:7
- 561Jn 3:24, Jhn 15:4–5, Rev 3:20, Jhn 14:20, Jhn 17:21–23, Psa 91:9, 1Jn 4:15–16, Jhn 14:23
- 57Jhn 5:26, Gal 2:20, Jhn 17:21, Jhn 3:17, Col 3:3–4, Jer 10:10, Psa 18:46, Jhn 11:25–26
- 58Jhn 3:36, Jhn 6:47–51, Jhn 6:31–34, Jhn 6:41
- 59Jhn 6:24, Pro 8:1–3, Jhn 18:20, Luk 4:31, Psa 40:9–10, Pro 1:20–23
- 60Jhn 6:66, Jhn 8:43, Jhn 8:31, Mat 11:6, Jhn 6:41–42, 2Pe 3:16, Heb 5:11
- 61Jhn 2:24–25, Jhn 6:64, Rev 2:23, Heb 4:13, Jhn 21:17, Mat 11:6
- 62Jhn 3:13, Mrk 16:19, Eph 4:8–10, Luk 24:51, Jhn 17:4–5, Act 1:9, Jhn 16:28, 1Pe 3:22
- 63Gal 5:25, Heb 4:12, Psa 119:93, Jhn 6:68, Psa 119:130, Psa 119:50, 1Pe 1:23, Deu 32:47
- 642Ti 2:19, Jhn 10:26, Heb 4:13, Psa 139:2–4, Jhn 2:24–25, Rom 8:29, Jhn 6:70–71, Jhn 6:61
- 65Jhn 6:44–45, Jhn 6:37, Jhn 3:27, Jhn 10:26–27, Eph 2:8–9, 2Ti 2:25, Jas 1:16–18, Tit 3:3–7
- 66Luk 9:62, 1Jn 2:19, Jhn 6:60, Heb 10:38, Jhn 8:31, Mat 19:22, 2Ti 4:10, Jhn 6:64
- 67Rut 1:11–18, Jhn 6:70, Luk 14:25–33, Jos 24:15–22, 2Sa 15:19–20
- 68Psa 73:25, Jhn 5:24, 1Jn 5:11–13, Jhn 6:63, Act 4:12, Act 5:20, Mat 16:16, Jhn 6:40
- 69Jhn 11:27, Luk 9:20, Mrk 8:29, 1Jn 5:1, 1Jn 5:20, Jhn 20:28, Jhn 1:45–49, Rom 1:3
- 70Jhn 13:27, Jhn 13:2, Jhn 17:12, Jhn 6:64, Jhn 13:18, Rev 3:9–10, Jhn 13:21, Jhn 15:19
- 71Mat 26:14–16, Psa 41:9, Jud 1:4, Act 1:16–20, Jhn 13:26, Jhn 18:2–6, Act 2:23, Psa 55:13–14
Parallelstellen
2
- Feeding the Five ThousandMat 14:13–21, Mrk 6:30–44, Luk 9:10–17, Jhn 6:1–14
- Walking on the WaterMat 14:22–33, Mrk 6:45–52, Jhn 6:15–21
Themen in diesem Kapitel
64
Andrew, Apostasy, Atonement, Backsliders, Barley, Blessing, Blindness, Blood, Bread, Capernaum, Conviction, Covetousness, Cowardice, Death, Decision, Duty, Economics, Faith, Fellowship, Flesh, Gifts From God, God, Grace of God, Holiness, Holy Spirit, Hypocrisy, Immortality, Instability, Jesus, the Christ, Life, Manna, Miracles, Murmuring, Penitent, Perseverance, Peter, Philip, Prayer, Predestination, Prophecy, Quickening, Quotations and Allusions, Rabbi, Regeneration, Resurrection, Righteous, Salvation, Seal, Seekers, Simon, Sin, Spirituality, Suffering, Symbols and Similitudes, Thankfulness, Tiberias, Types, Unbelief, Will, Wine, Wisdom, Word of God, Words, Zeal, Religious