Yohana 21
1 Baada ya haya Isa akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionesha kwao hivi:
2 Simoni Petro, Tomaso (aitwaye Didimasi), Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo, na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutaenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
4 Mara baada ya kupambazuka, Isa akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Isa.
5 Isa akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu, na tazama, wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
7 Basi yule mwanafunzi aliyependwa na Isa akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana Isa!” Simoni Petro aliposikia kwamba ni Bwana Isa, akajifunga nguo yake (kwa kuwa alikuwa ameitoa), naye akajitosa baharini.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa mia mbili.
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake, na mikate.
10 Isa akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu ufuoni. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa mia moja hamsini na watatu (153). Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
12 Isa akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa ni Bwana Isa.
13 Isa akaja, akachukua ule mkate, akawapa, na vivyo hivyo akawagawia wale samaki.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Isa kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
15 Walipokwisha kula, Isa akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Isa akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
16 Isa akamuuliza tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Isa akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
17 Kwa mara ya tatu Isa akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Isa alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Isa akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka. Lakini utakapokuwa mzee, utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
19 Isa alisema haya ili kuashiria aina ya kifo ambacho Petro angemtukuza nacho Mungu. Kisha Isa akamwambia Petro, “Nifuate!”
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Isa akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Isa walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Isa, “Bwana, na huyu je?”
22 Isa akamjibu, “Ikiwa nataka aishi hadi nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Isa, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Isa hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi hadi nitakaporudi, inakuhusu nini?”
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya, na ndiye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Isa alifanya. Kama yote yangeandikwa, nadhani hata ulimwengu wote haungekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu ambavyo vingeandikwa.
Querverweise
132
- 1Jhn 6:1, Mat 28:16, Jhn 6:23, Mat 28:7, Jhn 20:19–29, Mat 26:32
- 2Mat 4:21–22, Jhn 1:45–2:1, Jhn 4:46, Jhn 20:28, Jhn 11:16, Jhn 2:11, Luk 5:10, Jos 19:28
- 3Luk 5:5, Mat 4:18–20, Luk 5:10–11, 2Th 3:7–9, 1Th 2:9, 1Co 3:7, 2Ki 6:1–7, Act 18:3
- 4Jhn 20:14, Luk 24:15–16, Mrk 16:12, Luk 24:31
- 5Php 4:19, Php 4:11–13, Luk 24:41–43, Heb 13:5, Psa 37:3, 1Jn 2:13, 1Jn 2:18
- 6Luk 5:4–7, Act 2:41, Act 4:4, Jhn 2:5, Heb 2:6–9
- 7Jhn 13:23, Jhn 21:24, Jhn 20:2, Mat 14:28–29, Jhn 19:26, 2Co 5:14, Jhn 21:20, Sng 8:7
- 9Jhn 21:13, Jhn 21:10, 1Ki 19:5–6, Jhn 18:18
- 11Luk 5:6–8, Act 2:41
- 12Act 10:41, Jhn 16:19, Luk 9:45, Gen 32:29–30, Jhn 4:27, Jhn 21:15, Mrk 9:32
- 13Jhn 21:9, Act 10:41, Luk 24:42–43
- 14Jhn 20:26, Jhn 20:19
- 15Isa 40:11, 1Jn 4:19, Rom 15:1, 2Co 5:14–15, 1Pe 1:8, 1Pe 5:1–4, Eph 6:24, Ezk 34:23
- 16Act 20:28, 1Pe 5:2, 1Pe 2:25, Jhn 10:11–16, Psa 100:3, Psa 95:7, Luk 19:10, Luk 15:3–7
- 17Jhn 13:38, Mrk 14:72, Jhn 16:30, Jhn 21:15–16, Jhn 14:15, Jhn 15:10, 2Pe 1:12–15, Eph 4:30
- 18Jhn 13:36, Act 12:3–4, Act 21:11
- 192Pe 1:14, Jhn 21:22, Mat 10:38, Php 1:20, Mrk 8:33–38, 1Sa 12:20, Jhn 13:36–37, Jhn 18:32
- 20Jhn 21:7, Jhn 20:2, Jhn 21:24, Jhn 13:23–26
- 21Luk 13:23–24, Mat 24:3–4, Act 1:6–7
- 22Rev 2:25, Rev 3:11, Mrk 9:1, Mat 16:27–28, 1Co 4:5, Jas 5:7, Mat 24:44, Mat 24:3
- 23Deu 29:29, Job 33:13, Dan 4:35, Act 1:15, Job 28:28
- 24Jhn 19:35, Jhn 15:27, 3Jn 1:12, 1Jn 1:1–2, 1Jn 5:6
- 25Psa 40:5, Jhn 20:30–31, Psa 71:15, Job 26:14, Heb 11:32, Act 10:38, Act 20:35, Mat 11:5