Yohana 8
1 Lakini Isa akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
2 Alfajiri na mapema Isa akaja tena Hekaluni; watu wote wakakusanyika, naye akaketi, akaanza kuwafundisha.
3 Walimu wa Torati na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
4 Wakamwambia Isa, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
5 Katika sheria, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, hadi wafe. Sasa wewe wasemaje?”
6 Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Isa akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
7 Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
8 Akainama tena na kuandika ardhini.
9 Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Isa akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
10 Isa akainuka na kumwambia, “Mwanamke, wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
11 Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja, Bwana.” Isa akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako. Kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
12 Kisha Isa akasema nao tena, akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata, hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki, kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
14 Isa akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli, kwa sababu najua nilikotoka na ninakoenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakoenda.
15 Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu; mimi simhukumu mtu yeyote.
16 Lakini hata nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
17 Imeandikwa katika Torati yenu kwamba ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
18 Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
19 Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Isa akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
20 Isa alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
21 Isa akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi, ninyi hamwezi kuja.”
22 Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
23 Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini; mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu; mimi si wa ulimwengu huu.
24 Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu; kwa maana msipoamini kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
25 Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Isa akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
26 Nina mambo mengi ya kusema kuwahusu ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kuaminika, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia kuhusu Baba yake wa Mbinguni.
28 Kisha Isa akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua Mwana wa Adamu juu, ndipo mtajua kuwa mimi ndiye yule niliyesema, na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu, bali ninasema yale tu Baba yangu amenifundisha.
29 Yeye aliyenituma yu pamoja nami; hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.”
30 Wengi waliomsikia Isa akisema maneno haya wakamwamini.
31 Kisha Isa akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
32 Ndipo mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka huru.”
33 Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Ibrahimu, nasi hatujakuwa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
34 Isa akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima.
36 Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
37 Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Ibrahimu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
38 Ninasema yale niliyoyaona nikiwa mbele za Baba yangu, nanyi mnafanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
39 Wakajibu, “Baba yetu ni Ibrahimu.” Isa akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Ibrahimu, mngefanya mambo yale aliyofanya Ibrahimu.
40 Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya jambo la namna hii.
41 Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
42 Isa akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
44 Ninyi ni watoto wa baba yenu, ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli, maana hamna kweli ndani yake. Anaposema uongo, yeye husema lugha yake ya asili kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
45 Lakini kwa sababu nimewaambia kweli, hamkuniamini!
46 Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
47 Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
48 Wayahudi wakamjibu Isa, “Je, hatuko sahihi tunaposema kwamba wewe ni Msamaria, na kwamba una pepo mchafu?”
49 Isa akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
50 Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
51 Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu, hataona mauti milele.”
52 Ndipo Wayahudi wakapaza sauti, wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu! Ibrahimu alikufa, na manabii vilevile, nawe unasema kuwa mtu akitii neno lako hatakufa milele.
53 Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu ambaye alikufa, na manabii ambao pia walikufa? Unafikiri wewe ni nani?”
54 Isa akawajibu, “Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
55 Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
56 Baba yenu Ibrahimu alishangilia kwamba angeiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
57 Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, nawe wasema umemwona Ibrahimu?”
58 Isa akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Ibrahimu hajakuwa, Mimi niko.”
59 Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Isa akajificha, naye akatoka Hekaluni.
Querverweise
409
- 1Mat 21:1, Mrk 11:1, Luk 19:37
- 2Mat 26:55, Luk 21:37, Luk 4:20, Luk 5:3, Mat 5:1–2, Jer 25:3, Jhn 4:34, Ecc 9:10
- 5Lev 20:10, Deu 22:21–24, Ezk 16:38–40, Mat 5:17, Mat 19:6–8, Mat 22:16–18, Ezk 23:47
- 6Jer 17:13, Luk 10:25, Mat 19:3, Ecc 3:7, Amo 5:10, Psa 38:12–14, Amo 5:13, Num 14:22
- 7Mat 7:1–5, Rom 2:21–25, Rom 2:1–3, Deu 17:6–7, Mat 23:25–28, Heb 4:12–13, Col 4:6, Psa 50:16–20
- 9Rom 2:15, Ecc 7:22, 1Jn 3:20, Gen 42:21–22, Job 5:12–13, Psa 71:13, Jhn 8:10, Rom 2:22
- 10Isa 41:11–12
- 11Jhn 5:14, Jhn 3:17, Jhn 8:15, Isa 1:16–18, Luk 15:7, Luk 5:32, Pro 28:13, Job 34:31
- 12Jhn 12:46, Jhn 9:5, Jhn 12:35, Mat 5:14, Job 33:28, Jhn 1:4–9, Psa 18:28, Jhn 3:19
- 13Jhn 5:31–47
- 14Jhn 13:3, Jhn 16:28, Jhn 14:10, Jhn 8:42, Rev 3:14, Jhn 17:8, Num 12:3, Jhn 7:27–29
- 151Sa 16:7, Jhn 12:47, Jhn 3:17, Jhn 7:24, Rom 2:1, Jhn 18:36, Amo 5:7, 1Co 4:3–5
- 16Jhn 8:29, Act 17:31, Isa 32:1–2, 1Sa 16:7, Jhn 16:32, Jhn 5:22–30, Jer 23:5–6, Psa 72:1–2
- 17Deu 19:15, Deu 17:6, Heb 10:28, Mat 18:16, Gal 3:24, 2Co 13:1, Rev 11:3, Gal 4:21
- 18Jhn 8:38, Jhn 8:58, Rev 1:17–18, Heb 2:4, Jhn 8:25, Jhn 10:11, 1Jn 5:6–12, Jhn 14:6
- 19Jhn 8:54–55, Jhn 16:3, Jhn 14:6–9, 2Co 4:4–6, Jhn 7:28, 1Co 15:34, Mat 11:25, Jhn 1:10
- 20Jhn 7:30, Jhn 7:8, Mrk 12:41, Jhn 7:44, Mat 27:6, Mrk 12:43, 1Ch 9:26, Jhn 11:9–10
- 21Jhn 7:34, Jhn 8:24, 1Co 15:17–18, Jhn 13:33, Ezk 3:18–19, Job 20:11, Luk 16:22–26, Jhn 12:33
- 22Jhn 8:52, Psa 22:6, Jhn 8:48, Heb 13:13, Jhn 10:20, Psa 31:18, Psa 123:4, Jhn 7:35
- 23Jhn 3:31, 1Jn 2:15–16, Jhn 17:16, Jhn 17:14, 1Jn 4:5–6, 1Jn 5:19–20, Psa 17:4, Jas 4:4
- 24Jhn 3:36, Mrk 16:16, Jhn 3:18, Heb 10:26–29, Heb 12:25, Pro 8:36, Jhn 4:26, Heb 2:3
- 25Jhn 5:17–29, Jhn 8:12, Luk 22:67, Jhn 1:22, Jhn 19:9, Jhn 10:24, Jhn 1:19
- 26Jhn 15:15, Jhn 8:40, Jhn 12:47–50, Jhn 7:28, Jhn 17:8, Heb 5:11–12, Jhn 7:16, Jhn 16:12
- 27Isa 6:9, Isa 59:10, Isa 42:18–20, Jhn 8:43, 2Co 4:3–4, Rom 11:7–10, Jhn 8:47
- 28Jhn 5:19, Jhn 5:30, Jhn 6:38, Jhn 12:49–50, Jhn 3:14, 1Th 2:15–16, Jhn 12:32–34, Jhn 8:24
- 29Jhn 6:38, Jhn 16:32, Jhn 15:10, Jhn 5:30, Jhn 4:34, Isa 42:1, Jhn 8:16, Jhn 14:10–11
- 30Jhn 7:31, Jhn 2:23, Jhn 10:42, Jhn 6:14, Jhn 11:45
- 312Jn 1:9, Jhn 15:4–9, 2Ti 3:14, 1Ti 4:16, Jas 1:25, Col 1:23, 1Sa 12:14, Jhn 6:66–71
- 32Rom 8:2, Jhn 8:36, Jhn 17:17, 1Pe 2:16, Jhn 14:6, Rom 6:22, Rom 6:14–18, Isa 61:1
- 33Mat 3:9, Jhn 8:39, Neh 5:4–8, Neh 9:27–28, Gen 15:13, Jhn 8:37, Ezr 9:9, Jhn 19:25
- 34Rom 6:16, 2Pe 2:19, Pro 5:22, 1Jn 3:8–10, Rom 6:12, Rom 6:6, Tit 3:3, Rom 6:19–20
- 35Gal 4:4–7, Luk 15:31, Gen 21:10, Rom 8:15–17, Gal 4:30–31, Ezk 46:17, Heb 3:5–6, Jhn 14:19–20
- 362Co 3:17, Gal 5:1, Rom 8:2, Jhn 8:31–32, Luk 4:18, Zec 9:11–12, Isa 61:1, Isa 49:24–25
- 37Jhn 8:45–47, 1Co 2:14, Rom 9:7, Jhn 7:1, Jhn 8:59, Jhn 8:43, Act 13:26, Jhn 12:39–43
- 38Jhn 5:19, Jhn 8:44, Jhn 8:41, Jhn 5:30, Jhn 12:49–50, Jhn 14:24, Jhn 3:32, Jhn 14:10
- 39Gal 3:7, Jhn 8:37, Rom 9:7, Rom 2:28–29, Mat 3:9, Mat 5:45, Gal 3:29, Rom 4:12
- 40Jhn 8:26, Gal 4:29, Gal 4:16, Rev 12:12–13, Psa 37:32, Rev 12:17, Jhn 8:37–38, Psa 37:12
- 41Isa 64:8, Jhn 8:44, Jhn 8:38, Isa 63:16, Mal 2:11, Deu 32:6, Deu 14:1, Exo 4:22
- 42Jhn 12:49, Jhn 14:10, Jhn 17:8, Jhn 17:25, Jhn 15:23–24, Mal 1:6, Jhn 1:14, 1Jn 5:1–2
- 43Rom 8:7–8, Jhn 12:39–40, Jhn 7:17, Jhn 5:43, Pro 28:5, Jhn 6:60, Act 7:51, Jer 6:10
- 44Act 13:10, 1Jn 3:12, 1Jn 3:8–10, 2Co 11:3, Rev 12:9, Jhn 8:38, Rev 20:7–10, Jhn 8:41
- 452Ti 4:3–4, Jhn 3:19–20, Jhn 18:37, Jhn 7:7, 2Th 2:10, Gal 4:16
- 46Heb 4:15, Jhn 16:8, 2Co 5:21, Jhn 8:7, Jhn 14:30, Mrk 11:31, 1Pe 2:22, Mat 21:25
- 47Jhn 10:26–27, 2Jn 1:9, Jhn 18:37, 1Jn 3:10, Jhn 6:45–46, Jhn 8:37, Jhn 8:45, 1Jn 4:1–6
- 48Jhn 7:20, Jhn 8:52, Mat 10:25, Jhn 10:20, Mat 12:24, Jhn 4:9, Jas 2:19, Mat 10:5
- 491Pe 2:23, Jhn 8:29, Isa 49:3, Jhn 13:31–32, Jhn 11:4, Jhn 14:13, Pro 26:4–5, Mat 3:15–17
- 50Jhn 5:41, Jhn 8:54, Jhn 7:18, Jhn 5:20–23, Jhn 12:47–48, Jhn 5:45
- 51Jhn 11:25–26, Jhn 5:24, Jhn 3:15–16, Jhn 15:20, Jhn 6:50, Luk 2:26, Heb 11:5, Psa 89:48
- 52Heb 2:9, Jhn 9:24, Jhn 8:48, Jhn 8:51, Zec 1:5–6, Heb 11:13
- 53Jhn 4:12, Isa 9:6, Heb 7:1–7, Rom 9:5, Jhn 10:29–30, Jhn 19:7, Jhn 8:58, Jhn 5:18
- 54Pro 25:27, Jhn 8:50, 2Pe 1:17, Jhn 16:14–15, Psa 110:1–4, 2Co 10:18, Jhn 7:18, Act 3:13
- 55Jhn 8:19, Jhn 7:28–29, Jhn 8:44, Rev 3:9, Jhn 8:51, Mat 11:27, Jhn 15:21, 1Jn 5:10
- 56Heb 11:13, Gen 22:18, Gal 3:7–9, Jhn 8:39, Mat 13:17, Luk 10:24, 1Pe 1:10–12, Heb 11:39
- 58Exo 3:14, Col 1:17, Jhn 17:5, Jhn 1:1–2, Isa 44:6, Jhn 17:24, Heb 13:8, Rev 1:8
- 59Jhn 11:8, Jhn 10:30–33, Jhn 10:39–40, Lev 24:16, Luk 4:29–30, Jhn 12:36, Act 8:39–40, Jhn 11:54
Themen in diesem Kapitel
50
Abraham, Adultery, Blindness, Church, Conscience, Conviction, Darkness, Decision, Demons, Depravity of Man, Faith, Falsehood, God, Gospel, Hades, Hypocrisy, Instruction, Jesus, the Christ, Law, Liars, Liberty, Light, Love, Lust, Malice, Obedience, Persecution, Perseverance, Regeneration, Reproof, Righteous, Righteousness, Satan, Scribe (S), Self-Condemnation, Self-Delusion, Self-Righteousness, Servant, Sin, Slander, Temple, Treasure-Houses, Truth, Unbelief, Uncharitableness, Wicked (People), Wisdom, Witness, Women, Word of God