Yohana 17
1 Baada ya Isa kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Mtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa.
3 Nao uzima wa milele ndio huu: wakujue wewe uliye Mungu wa pekee wa kweli, na Isa Al-Masihi uliyemtuma.
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujaumbwa.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
8 kwa kuwa maneno yale uliyonipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
9 Ninawaombea wao. Siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
10 Wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia, kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
17 Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndilo kweli.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao,
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako. Wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiwe uliyenituma mimi.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
23 Mimi ndani yao na wewe ndani yangu: ili wawe wamekamilika katika umoja, na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao, nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao, na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
Querverweise
200
- 1Jhn 13:31–32, Php 2:9–11, Jhn 17:4–5, Jhn 12:23, Jhn 12:27–28, Act 3:13, Jhn 7:39, 1Pe 1:21
- 2Jhn 10:28–29, Jhn 6:39, Dan 7:14, Jhn 6:37, Mat 28:18, Jhn 17:24, Heb 2:8–9, Jhn 17:9
- 31Jn 5:20, 1Jn 5:11–12, Jer 9:23–24, Jhn 3:17, Jhn 17:25, Hos 6:3, Jhn 14:9–10, Heb 8:11–12
- 4Jhn 4:34, Act 20:24, 2Ti 4:7, Jhn 14:31, Jhn 19:30, Jhn 15:10, Jhn 13:31–32, Jhn 12:28
- 5Jhn 1:1–3, Col 1:15–17, Jhn 10:30, 1Pe 1:20, Php 2:6, Heb 1:3, Rev 5:9–14, Heb 1:10
- 6Jhn 17:26, 1Jn 5:20, Jhn 14:21–24, Jhn 17:24, Jhn 10:27–29, Jhn 6:37, Exo 34:5–7, Jhn 17:2
- 7Jhn 7:16–17, Jhn 16:15, Jhn 8:28, Jhn 17:10, Jhn 10:29–30, Jhn 14:7–10, Jhn 12:49–50, Jhn 14:20
- 8Jhn 17:14, Jhn 15:15, Jhn 16:30, 1Th 2:13, Jhn 16:27, Jhn 8:42, Jhn 17:21, Jhn 12:49
- 9Heb 9:24, Jhn 17:2, Jhn 17:6, Luk 22:32, 1Jn 2:1–2, Jhn 17:20, 1Jn 5:19, Jhn 14:16
- 10Jhn 10:30, 1Pe 2:9, Rev 5:8–14, 2Th 1:10, 1Co 3:21–23, Jhn 16:14–15, Col 1:15–19, Col 2:9
- 11Mat 6:9, Pro 18:10, Jhn 17:12–18, Heb 9:24, Jhn 10:29–30, Jhn 17:21–22, Eph 4:4, Php 2:9
- 12Psa 109:6–19, Jhn 10:27–28, Jhn 18:9, Jhn 13:18, Jhn 6:37, Act 1:16–20, Jhn 6:70–71, Jhn 6:39–40
- 13Heb 12:2, Gal 5:22, Jhn 15:11, Jhn 3:29, Jhn 16:22–24, 1Jn 1:4, Jhn 13:3, Psa 43:4
- 14Jhn 17:16, Jhn 15:18–21, 1Jn 5:19–20, Jhn 8:23, 1Jn 4:5–6, Jhn 7:7, Pro 29:27, Mat 10:24–25
- 15Psa 121:7, 1Jn 5:18, Mat 6:13, 2Th 3:3, Gal 1:4, 1Ch 4:10, Luk 11:4, Isa 38:18–19
- 16Jhn 17:14
- 17Jhn 15:3, Psa 119:160, Eph 5:26, 1Pe 1:22–23, Jhn 17:19, Jhn 8:32, Jas 1:21, 2Th 2:13
- 18Jhn 20:21, 2Co 5:20, Jhn 17:3, Mat 10:5, Eph 3:7, Jhn 4:38, Isa 61:1–3, Mat 23:34
- 19Tit 2:14, Heb 2:11, Jhn 17:17, Heb 10:5–10, 1Co 1:2, 1Th 4:7, 2Ti 2:10, 2Co 4:15
- 20Jhn 17:6–11, Act 2:41, Act 4:4, Rom 15:18–19, Eph 4:11, Rom 16:26, 2Ti 1:2
- 211Co 12:12, Col 3:11–14, Jhn 17:11, 1Co 12:25–27, Php 1:27, Jhn 13:35, Jhn 10:30, Jhn 17:22–23
- 222Co 3:18, Jhn 14:20, Jhn 1:16, Eph 2:20, Mrk 16:17–20, 2Co 5:20, 1Jn 3:24, 2Co 6:1
- 23Jhn 17:21, Jhn 16:27, 1Jn 3:1, Jhn 13:35, 1Jn 4:12–16, Col 3:14, Jhn 17:26, 1Jn 1:3
- 24Jhn 12:26, Jhn 17:5, Jhn 14:3, 2Co 4:6, 1Jn 3:2, Gen 45:13, Mat 25:21, 2Co 3:18
- 25Jhn 17:11, Jhn 7:29, Jhn 17:8, Jhn 16:27, Jhn 15:21, Heb 8:11, 2Co 4:4, Jhn 10:15
- 26Jhn 17:23, Jhn 17:6, Jhn 15:9, 1Jn 4:13–14, Jhn 14:20, Heb 2:12, Jhn 15:15, Psa 22:22
Themen in diesem Kapitel
37
Blessing, Blindness, Church, Communion, Earth, Election, Fellowship, Gifts From God, Glorifying God, Glory, God, Gospel, Grace of God, Hatred, Heaven, Holiness, Immortality, Jesus, the Christ, Joy, Judas (Jude), Life, Love, Minister, Christian, Obedience, Persecution, Power, Prayer, Predestination, Regeneration, Reprobacy, Righteous, Salvation, Sanctification, Truth, Wicked (People), Wisdom, Word of God