Yohana 11
1 Basi mtu mmoja, jina lake Lazaro, alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania, kijiji cha Mariamu na Martha dada yake.
2 (Huyu Mariamu, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye alimpaka Bwana Isa mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake.)
3 Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Isa kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”
4 Lakini Isa aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti, bali ni wa kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.”
5 Isa aliwapenda Martha, Mariamu na Lazaro ndugu yao.
6 Hata hivyo, baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, alikawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.
7 Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Yudea.”
8 Wanafunzi wake wakamwambia, “Mwalimu, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”
9 Isa akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wanaotembea mchana hawawezi kujikwaa, kwa maana wanaona kwa nuru ya ulimwengu huu.
10 Lakini wale wanaotembea usiku hujikwaa kwa sababu hawana nuru ndani yao.”
11 Baada ya kusema haya, Isa akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”
12 Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.”
13 Hata hivyo, Isa alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.
14 Kwa hiyo Isa akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa.
15 Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwako huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”
16 Tomaso (aliyeitwa Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”
17 Isa alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne.
18 Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu, umbali wa yamkini maili mbili,
19 na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Mariamu kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao.
20 Martha aliposikia kwamba Isa anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Mariamu alibaki nyumbani.
21 Martha akamwambia Isa, “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.
22 Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”
23 Isa akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”
24 Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”
25 Isa akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi;
26 na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?”
27 Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Al-Masihi, Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”
28 Baada ya kusema haya, Martha alienda akamwita Mariamu dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.”
29 Mariamu aliposikia hivyo, akaondoka upesi, akaenda hadi alipokuwa Isa.
30 Isa alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha.
31 Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Mariamu nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani kwamba alikuwa anaenda kule kaburini kulilia huko.
32 Mariamu alipofika mahali pale Isa alipokuwa, alipiga magoti miguuni pake na kusema, “Bwana, kama ungekuwa hapa, ndugu yangu hangekufa.”
33 Isa alipomwona Mariamu akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Isa alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana.
34 Akauliza, “Mmemweka wapi?” Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”
35 Isa akalia machozi.
36 Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”
37 Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”
38 Isa akafika penye kaburi akiwa amefadhaika sana kwa mara nyingine. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe liliwekwa kwenye ingilio lake.
39 Isa akasema, “Liondoeni jiwe.” Martha dada yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”
40 Isa akamwambia, “Sikukuambia kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”
41 Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Isa akainua macho yake juu, akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia.
42 Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya watu hawa waliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”
43 Baada ya kusema haya, Isa akapaza sauti yake, akaita, “Lazaro, njoo huku!”
44 Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake. Isa akawaambia, “Mfungueni; mwacheni aende zake.”
45 Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Mariamu walipoona yale Isa aliyoyatenda, wakamwamini.
46 Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Isa aliyoyafanya.
47 Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa Baraza la Wayahudi. Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi.
48 Tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”
49 Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, aliyekuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote!
50 Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”
51 Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe, bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Isa angekufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi;
52 wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja.
53 Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Isa.
54 Kwa hiyo Isa akawa hatembei tena hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.
55 Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu ili wakajitakase kabla ya Pasaka.
56 Watu wakawa wanamtafuta Isa, nao waliposimama kwenye ua la Hekalu, waliulizana, “Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu?”
57 Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Isa aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.
Querverweise
370
- 1Luk 10:38–42, Jhn 12:17, Jhn 11:11, Jhn 12:9, 2Ki 20:1–12, Mat 21:17, Jhn 11:5–6, Act 9:37
- 2Jhn 12:3, Mat 26:6–7, Mrk 14:3, Luk 7:37–38
- 3Jhn 11:5, Rev 3:19, Heb 12:6–7, Jhn 13:23, Psa 16:3, Jhn 11:11, Gen 22:2, 2Ti 4:20
- 4Jhn 11:40, Jhn 9:3, 1Pe 4:14, Jhn 5:23, Jhn 17:5, 1Pe 4:11, Jhn 13:31–32, Mrk 5:39–42
- 5Jhn 15:9–13, Jhn 17:26, Jhn 11:36, Jhn 16:27, Jhn 11:8
- 6Isa 30:18, Isa 55:8–9, Gen 42:24, Gen 22:14, Gen 43:29–31, Mat 15:22–28, Gen 44:1–5, Gen 45:1–5
- 7Act 20:22–24, Luk 9:51, Act 15:36, Jhn 10:40–42
- 8Jhn 10:31, Jhn 8:59, Act 21:12–13, Mat 16:21–23, Jhn 10:39, Act 20:24, Psa 11:1–3, Mat 23:7
- 9Jhn 9:4, Jhn 12:35, Jer 31:9, Luk 13:31–33, Pro 3:23
- 10Pro 4:18–19, 1Jn 2:10–11, Jer 13:16, Jer 20:11, Ecc 2:14, Psa 27:2
- 11Dan 12:2, Jhn 11:13, Jhn 11:43–44, Mat 27:52, 1Th 5:10, 1Co 15:51, Eph 5:14, Mrk 5:39
- 13Mat 9:24
- 14Jhn 16:25, Jhn 16:29, Jhn 10:24
- 152Ti 2:10, Jhn 14:10–11, Jhn 11:4, 1Jn 5:13, Jhn 11:35–36, Isa 54:15, 2Co 4:15, Isa 65:8
- 16Jhn 13:37, Mat 10:3, Mrk 3:18, Luk 6:15, Mat 26:35, Jhn 14:5, Jhn 21:2, Jhn 20:24–29
- 17Jhn 11:39, Hos 6:2, Act 2:27–31, Jhn 2:19
- 18Luk 24:13, Jhn 11:1, Rev 14:20, Rev 21:16, Jhn 6:19
- 19Job 2:11, Jhn 11:31, 1Th 5:11, 2Co 1:4, Job 42:11, 1Th 4:18, Rom 12:15, Lam 2:13
- 201Th 4:17, Luk 10:38–42, Mat 25:1, Jhn 11:30, Act 10:25, Mat 25:6, Act 28:15
- 21Jhn 11:32, Mat 9:18, 1Ki 17:18, Jhn 11:37, Luk 7:6–10, Luk 8:49–55, Jhn 4:47–49, Psa 78:19
- 22Jhn 9:31, Jhn 11:41–42, Mrk 9:23, Mat 28:18, Heb 11:17–19, Jhn 5:22–27, Jhn 3:35, Psa 2:8
- 23Jhn 11:43–44
- 24Dan 12:2–3, Act 24:15, Jhn 5:28–29, Isa 26:19, Act 17:31–32, Hos 13:14, Luk 14:14, Psa 17:15
- 251Th 4:14, Jhn 3:36, 1Jn 5:11–12, Jhn 1:4, Rom 8:10–11, Jhn 5:21, Isa 26:19, Rom 8:2
- 26Jhn 10:28, Jhn 5:24, Rom 8:13, 1Jn 5:10–12, Jhn 8:51–53, Jhn 6:54–58, Jhn 6:50–51, Jhn 3:15–18
- 27Mat 16:16, Jhn 6:14, Jhn 6:69, Mal 3:1, 1Jn 5:1, 1Jn 5:20, Luk 2:11, 1Ti 1:15–16
- 28Jhn 13:13, 1Th 4:17–18, Jhn 11:20, Jhn 20:16, Mrk 10:49, Jhn 1:45, Mat 26:18, Mrk 14:14
- 29Psa 27:8, Pro 15:23, Sng 3:1–4, Psa 119:59–60, Pro 27:17
- 30Jhn 11:20
- 31Jhn 11:19, 2Sa 12:16–18, Gen 37:35, 1Co 2:15
- 32Jhn 11:21, Luk 17:16, Luk 5:8, Luk 8:41, Rev 5:14, Rev 22:8, Rev 5:8, Jhn 11:37
- 33Jhn 11:38, Jhn 12:27, Rom 12:15, Mrk 3:5, Gen 43:30–31, Heb 5:7–8, Gen 45:1–5, Mrk 14:33–35
- 34Mat 28:6, Mrk 16:6, Jhn 20:2, Mrk 15:47, Jhn 1:39
- 35Luk 19:41, Heb 4:15, Jhn 11:33, Isa 53:3, Psa 119:136, Jer 13:17, Job 30:25, Heb 2:16–17
- 36Jhn 11:3, 1Jn 4:9–10, Rev 1:5, 1Jn 3:1, Eph 5:2, Eph 5:25, Jhn 14:21–23, 2Co 8:8–9
- 37Jhn 9:6–7, Psa 78:19–20, Luk 23:39, Jhn 11:32, Mat 27:40–42, Luk 23:35, Mrk 15:32, Jhn 11:21
- 38Jhn 11:33, Luk 24:2, Mat 27:60, Isa 22:16, Gen 23:19, Mrk 15:46, Mrk 8:12, Jhn 20:1
- 39Jhn 11:17, Psa 49:7, Mrk 16:3, Gen 3:19, Php 3:21, Gen 23:4
- 40Jhn 11:4, Jhn 11:23–26, Rom 4:17–25, Psa 63:2, Jhn 1:14, 2Co 3:18, Psa 90:16, 2Co 4:6
- 41Mat 11:25, Jhn 17:1, Psa 123:1, Luk 10:21, Php 4:6, Jhn 12:28–30, Luk 18:13
- 42Jhn 3:17, Jhn 17:21, Heb 7:25, 1Jn 4:14, Mat 26:53, 1Jn 4:9–10, Jhn 11:22, Jhn 17:25
- 43Act 9:40, 2Ki 4:33–36, Act 9:34, Luk 7:14–15, 1Ki 17:21–22, Act 3:6, Mrk 4:41, Act 3:12
- 44Jhn 5:25, Jhn 20:7, Jhn 11:25–26, Php 3:21, Jhn 5:21, Luk 7:15, Gen 1:3, Act 20:9–12
- 45Jhn 11:19, Jhn 2:23, Jhn 10:41, Jhn 12:9–11, Jhn 11:31, Jhn 12:17–19, Jhn 7:31, Jhn 12:42
- 46Luk 16:30–31, Jhn 9:13, Act 5:25, Jhn 5:15–16, Jhn 12:37
- 47Mat 26:3, Act 4:16–17, Jhn 12:19, Jhn 11:57, Act 4:5–6, Jhn 2:11, Mat 5:22, Act 5:21
- 481Th 2:15–16, Mat 27:25, Zec 14:1–2, Dan 9:26–27, Mat 23:35–38, Act 5:28, Zec 13:7–8, Luk 11:52
- 49Jhn 18:13–14, Jhn 11:51, Mat 26:3, Pro 26:12, Luk 3:2, Act 4:6, 1Co 1:20, 1Co 2:6
- 50Jhn 18:14, Luk 24:46, Jhn 19:12, Rom 3:8, Jhn 11:48
- 512Co 5:21, Dan 9:26, Gal 4:4–5, 1Sa 23:9, Exo 28:30, Mat 20:28, Gal 3:13, Num 22:28
- 52Jhn 10:16, Isa 49:6, 1Jn 2:2, 1Pe 1:1, Eph 1:9–10, Rev 5:9, Rom 9:25–26, Eph 2:14–22
- 53Act 9:23, Act 5:33, Mat 26:59, Psa 31:13, Psa 113:2, Psa 109:4–5, Psa 2:2, Jhn 12:10
- 54Jhn 7:1, 2Ch 13:19, Jhn 7:4, Jhn 4:1–3, Jhn 7:10, Jhn 18:20, Jhn 10:40, Jhn 7:13
- 552Ch 30:17–20, Heb 9:13–14, Jhn 2:13, Jhn 6:4, Gen 35:2, Jhn 12:1, Exo 19:10, 1Sa 16:5
- 56Jhn 7:11, Jhn 11:7–8
- 57Psa 109:4, Jhn 8:59, Jhn 9:22, Jhn 10:39, Jhn 5:16–18
Themen in diesem Kapitel
52
Adoption, Afflictions and Adversities, Anointing, Apostles, Atonement, Bethany, Burial, Caiaphas, Cave, Condolence, Courage, Darkness, Day, Dead (People), Death, Decision, Didymus (Twin), Envy, Ephraim, Faith, Family, Friendship, Furlong, Hours, Immortality, Israel, Prophecies Concerning, Jesus, the Christ, Kindness, Lazarus, Life, Love, Martha, Mary, Minister, Christian, Miracles, Ophrah, Persecution, Prayer, Priest, Prudence, Purification, Rabbi, Readings, Select, Resurrection, Salvation, Sleep, Sorrow, Suffering, Thankfulness, Thomas, Weeping, Women