Yohana 14
1 Isa akawaambia, “Msifadhaike mioyoni mwenu. Mnamwamini Mungu, mniamini pia.
2 Nyumbani mwa Baba yangu kuna makao mengi. Kama sivyo, ningewaambia. Naenda kuwaandalia makao.
3 Nami nikienda na kuwaandalia makao, nitarudi tena na kuwachukua mkae pamoja nami, ili mahali nilipo nanyi mpate kuwepo.
4 Ninyi mnajua njia ya kufika ninakoenda.”
5 Tomaso akamwambia, “Bwana, sisi hatujui unakoenda, tutaijuaje njia?”
6 Isa akawaambia, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kupitia kwangu.
7 Kama mngenijua mimi, mngemjua na Baba pia. Tangu sasa mnamjua Baba yangu, tena mmemwona.”
8 Filipo akamwambia, “Bwana, tuoneshe Baba, na hiyo itatutosha.”
9 Isa akamjibu, “Filipo, nimekaa nanyi muda huu wote hata usinijue? Mtu yeyote aliyeniona mimi amemwona Baba. Sasa wawezaje kusema, ‘Tuoneshe Baba’?
10 Je, huamini ya kuwa mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambia siyasemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba akaaye ndani yangu ndiye atendaye hizi kazi.
11 Nisadiki mimi kwamba niko ndani ya Baba, na Baba yuko ndani yangu; la sivyo, niaminini kwa sababu ya zile kazi nizitendazo.
12 Amin, amin nawaambia, yeyote anayeniamini mimi, kazi ninazozifanya naye atazifanya. Naam, na atazifanya kazi kubwa kuliko hizi, kwa sababu mimi ninaenda kwa Baba.
13 Nanyi mkiomba lolote kwa Jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba apate kutukuzwa katika Mwana.
14 Mkiniomba lolote kwa Jina langu, nitalifanya.
15 “Kama mnanipenda, mtazishika amri zangu.
16 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine akae nanyi milele.
17 Huyo ndiye Roho wa kweli ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa sababu haumwoni wala haumjui. Ninyi mnamjua kwa kuwa yuko pamoja nanyi, naye anakaa ndani yenu.
18 Sitawaacha ninyi yatima; nitakuja kwenu.
19 Bado kitambo kidogo na ulimwengu hautaniona tena, ila ninyi mtaniona. Kwa kuwa mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.
20 Wakati huo mtajua ya kuwa mimi niko ndani ya Baba, na ninyi mko ndani yangu, na mimi niko ndani yenu.
21 Yeyote mwenye amri zangu na kuzishika ndiye anipendaye. Naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.”
22 Ndipo Yuda (siyo Iskariote) akamwambia, “Bwana, itakuwaje kwamba utajidhihirisha kwetu na si kwa ulimwengu?”
23 Isa akamjibu, “Mtu yeyote akinipenda atalishika neno langu na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake na kufanya makao yetu kwake.
24 Mtu yeyote asiyenipenda hayashiki maneno yangu, na maneno niliyowapa si yangu bali ni ya Baba aliyenituma.
25 “Nimewaambia mambo haya yote wakati bado niko pamoja nanyi.
26 Lakini huyo Msaidizi, yaani huyo Roho Mtakatifu wa Mungu, ambaye Baba atamtuma kwenu kwa Jina langu, atawafundisha mambo yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
27 Amani nawaachia; amani yangu nawapa. Amani hii ninayowapa si kama ile ulimwengu unatoa. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiogope.
28 “Mlisikia nikisema, ‘Ninaenda zangu, lakini nitarudi tena.’ Kama kweli mngenipenda, mngefurahi kwa kuwa naenda kwa Baba, kwani Baba ni mkuu kuliko mimi.
29 Nimewaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini.
30 Sitasema nanyi zaidi, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu anakuja, naye hana kitu kwangu,
31 lakini ulimwengu upate kujua kuwa ninampenda Baba, nami hufanya vile Baba alivyoniamuru. “Haya inukeni; twendeni zetu.
Querverweise
232
- 1Isa 26:3, Jhn 16:22–23, Isa 12:2–3, 2Co 12:9–10, Jhn 14:27–28, Jhn 6:40, Psa 42:5–6, Jhn 12:44
- 22Co 5:1, Jhn 13:36, Heb 13:14, Rev 21:2, Heb 11:10, Rev 3:12, Heb 11:14–16, Jhn 12:25–26
- 31Th 4:16–17, Jhn 12:26, 2Ti 2:12, Act 1:11, Heb 9:28, Rom 8:17, Jhn 14:28, Jhn 14:18–23
- 4Jhn 10:9, Jhn 16:28, Jhn 3:16–17, Jhn 6:40, Jhn 3:36, Jhn 12:26, Jhn 6:68–69, Jhn 13:3
- 5Jhn 11:16, Mrk 9:19, Jhn 20:25–28, Luk 24:25, Jhn 15:12, Mrk 8:17–18, Heb 5:11–12
- 6Act 4:12, Jhn 10:9, Eph 2:18, Jhn 11:25–26, Jhn 1:4, 1Jn 5:20, Jhn 1:14, 1Jn 5:11–12
- 7Col 1:15–17, Jhn 8:19, Luk 10:22, Jhn 17:8, Jhn 17:6, Jhn 17:26, Jhn 17:21, Jhn 14:9–10
- 8Exo 33:18–23, Rev 22:3–5, Jhn 1:43–46, Psa 17:15, Jhn 16:25, Jhn 6:5–7, Mat 5:8, Jhn 12:21–22
- 9Col 1:15, Jhn 12:45, Jhn 14:7, Heb 1:3, Jhn 10:30, Jhn 1:14, Php 2:6, Jhn 14:20
- 10Jhn 5:19, Jhn 10:38, Jhn 10:30, Act 10:38, Jhn 8:28, Jhn 12:49, Col 2:9, Jhn 6:38–40
- 11Jhn 10:38, Jhn 5:36, Jhn 10:25, Jhn 14:10, Heb 2:4, Act 2:22, Mat 11:4–5, Jhn 10:32
- 12Mat 21:21, Mrk 16:17, Luk 10:17–19, Act 16:18, Act 19:12, Act 9:34, Act 3:6–8, Act 8:7
- 13Jhn 15:7, Mrk 11:24, Mat 7:7, Mat 21:22, 1Jn 5:14, Jhn 16:23, Jhn 14:14, Jhn 15:16
- 151Jn 2:3–5, 1Jn 5:2–3, Jhn 14:21–24, 2Jn 1:6, Jhn 15:10–14, 1Jn 4:19–20, 2Co 5:14–15, 1Pe 1:8
- 16Jhn 14:26, Jhn 15:26, Jhn 16:7–15, Rom 15:13, Rom 8:26–27, Gal 5:22, Rom 14:17, Act 9:31
- 17Ezk 36:27, Jhn 16:13, 1Jn 2:27, Jhn 15:26, 1Jn 4:6, 1Co 2:14, 1Co 3:16, 2Ti 1:14
- 18Jhn 14:3, Psa 23:4, Mat 18:20, Jhn 14:16, Jhn 14:27–28, Mat 28:20, Jhn 16:33, Heb 2:18
- 19Jhn 16:16, Jhn 6:56–58, Jhn 7:33, Heb 7:25, Col 3:3–4, Jhn 11:25, Jhn 16:22, 1Co 15:45
- 20Jhn 15:5–7, Gal 2:20, Jhn 17:21–23, Jhn 17:26, Jhn 14:10, 1Jn 4:12, Jhn 10:38, Rom 8:1
- 21Jhn 14:15, 1Jn 5:3, 1Jn 2:5, 2Jn 1:6, Jhn 15:9–10, Jhn 16:27, Deu 11:13, Luk 11:28
- 22Act 1:13, Luk 6:16, Mat 10:3, Act 10:40–41, Jhn 6:60, Jhn 3:4, Jhn 3:9, Mrk 3:18
- 23Jhn 14:21, Jhn 14:15, Rev 3:20–21, 1Jn 4:15–16, 1Jn 2:24, 1Jn 4:4, 2Co 6:16, Jhn 10:30
- 24Jhn 7:16, Jhn 14:10, Jhn 8:42, Jhn 5:19, Jhn 3:34, Jhn 14:21–23, 1Jn 3:16–20, Mat 25:41–46
- 25Jhn 17:6–8, Jhn 13:19, Jhn 16:1–4, Jhn 16:12, Jhn 14:29, Jhn 15:11
- 26Jhn 15:26, Jhn 14:16, 1Co 2:10–13, 1Jn 2:27, Jhn 16:7, 1Jn 2:20, Eph 1:17, Rom 15:13
- 27Php 4:7, Jhn 16:33, Isa 41:10, 2Th 3:16, Col 3:15, 2Ti 1:7, Rom 15:13, Num 6:26
- 28Jhn 10:29–30, 1Co 15:24–28, 1Co 11:3, Heb 1:2–3, Heb 2:9–15, Php 2:6–11, Jhn 13:16, Jhn 20:17
- 29Jhn 13:19, Jhn 16:4–31, Mat 24:24–25
- 301Jn 5:19, 1Jn 4:4, Jhn 12:31, Eph 6:12, Rev 12:9, Eph 2:2, 1Pe 2:22, 2Co 4:4
- 31Jhn 12:49, Jhn 10:18, Jhn 4:34, Luk 12:50, Php 2:8, Heb 5:7–8, Psa 40:8, Jhn 15:9
Themen in diesem Kapitel
41
Afflictions and Adversities, Apostles, Blindness, Chiding, Church, Commandments, Communion, Contingencies, Depravity of Man, Doubting, Duty, Faith, Fellowship, God, Heaven, Holy Spirit, House, Immortality, Jesus, the Christ, Judas (Jude), Life, Love, Mansion, Miracles, Obedience, Peace, Persecution, Philip, Prayer, Resurrection, Righteous, Righteousness, Satan, Spirituality, Thomas, Trinity, Trouble, Truth, Unbelief, Way, Wisdom