Yohana 12
1 Siku sita kabla ya Pasaka, Isa alienda Bethania, makao ya Lazaro, aliyekuwa amemfufua kutoka kwa wafu.
2 Wakaandaa karamu kwa heshima ya Isa. Martha akawahudumia, wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Isa.
3 Kisha Mariamu akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Isa na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
4 Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wanafunzi wa Isa, ambaye baadaye angemsaliti Isa, akasema,
5 “Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari mia tatu, na fedha hizo wakapewa maskini?”
6 Yuda hakusema hivi kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi; ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha, na akawa akiiba zile fedha.
7 Isa akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
9 Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Isa alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Isa, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Isa alikuwa amemfufua.
10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakapanga njama ya kumuua Lazaro pia,
11 kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake, Wayahudi wengi walikuwa wanamfuata Isa na kumwamini.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa wa watu waliokuwa wamekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Isa angekuja Yerusalemu.
13 Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Mwenyezi Mungu!” “Amebarikiwa mfalme wa Israeli!”
14 Isa akamkuta mwana-punda, akampanda, kama ilivyoandikwa,
15 “Usiogope, ewe Binti Sayuni; tazama, mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
16 Wanafunzi wake Isa mwanzoni hawakuelewa mambo haya. Lakini Isa alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
17 Wale waliokuwepo Isa alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu waliendelea kushuhudia.
18 Na kwa sababu walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu, umati wa watu wakaenda kumlaki.
19 Hivyo Mafarisayo walipoona hayo, wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
20 Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wameenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
21 Hawa wakaenda kwa Filipo, aliyekuwa raia wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Isa.”
22 Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Isa.
23 Isa akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
24 Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa, huzaa mbegu nyingi.
25 Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele.
26 Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii’? Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, ikasema, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
29 Umati ule wa watu waliokuwa mahali pale waliisikia ile sauti, nao wakasema hiyo ilikuwa sauti ya radi; wengine wakasema malaika ameongea naye.
30 Isa akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
31 Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
32 Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
33 Isa aliyasema haya akionesha ni kifo gani atakachokufa.
34 Umati ule wa watu wakapaza sauti, wakasema, “Tumesikia kutoka Torati kwamba Al-Masihi adumu milele; hivyo wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?”
35 Ndipo Isa akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingali pamoja nanyi. Nendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakoenda.
36 Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Isa aliondoka, akajificha wasimwone.
37 Hata baada ya Isa kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
38 Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Mwenyezi Mungu, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Mwenyezi Mungu umefunuliwa kwa nani?”
39 Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
40 “Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
41 Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Isa na kunena habari zake.
42 Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
43 Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zinazotoka kwa Mungu.
44 Isa akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali pia yeye aliyenituma.
45 Yeyote anionaye mimi amemwona yeye aliyenituma.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
47 “Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
48 Yuko anayehukumu yule anayenikataa mimi na kuyakataa maneno yangu; yale maneno niliyoyasema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
49 Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
50 Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.”
Querverweise
357
- 1Mrk 14:3–8, Jhn 11:1, Luk 24:50, Jhn 11:55, Mat 21:17, Jhn 11:44, Mat 26:6–11, Mrk 11:11
- 2Luk 22:27, Rev 3:20, Luk 10:38–42, Jhn 12:9–10, Mrk 14:3, Jhn 11:43–44, Mat 26:6, Luk 12:37
- 3Mrk 14:3–9, Jhn 11:2, Luk 10:38–39, Mat 26:6–13, Luk 7:37–38, Jhn 11:32, Jhn 11:28, Luk 7:46
- 4Mat 10:4, Jhn 18:2–5, Jhn 13:2, 1Sa 17:28–29, Ecc 4:4, Luk 6:16, Jhn 13:26, Jhn 6:70–71
- 5Luk 12:33, Luk 18:22, Mat 26:8–9, Mrk 14:4–5, Luk 6:41, Mal 1:10–13, Exo 5:17, Jhn 6:7
- 6Jhn 13:29, Psa 50:16–20, Jas 2:6, Jas 2:2, 2Ki 5:20–27, Gal 2:10, 1Co 6:10, Pro 29:7
- 7Mat 26:12, Mrk 14:6, Mat 27:57–60, Mat 26:10, Jhn 19:38–42, Psa 109:31, Mrk 15:42–47, Zec 3:2
- 8Deu 15:11, Mrk 14:7, Mat 26:11, Jhn 12:35, Jhn 13:33, Jhn 8:21, Act 1:9–11, Jhn 16:5–7
- 9Act 4:14, Act 3:10–11, Jhn 11:43–45
- 10Luk 16:31, Gen 4:4–10, Mat 2:16, Jhn 11:47–53, Dan 5:21–23, Exo 10:3, Job 40:8–9, Mat 2:3–8
- 11Jhn 11:45, Jhn 12:18, Jas 3:14–16, Act 13:45, Jhn 11:48, Jhn 7:31, Jhn 15:18–25
- 12Mrk 11:7–10, Mat 21:4–9, Luk 19:35–38, Jhn 11:55–56
- 13Psa 118:25–26, Rev 15:3, Luk 19:35–38, Mat 21:9–11, Rev 7:9, Mrk 11:8–10, Psa 72:17–19, Hos 3:5
- 14Zec 9:9, Mat 21:1–7, Mrk 11:1–7, Luk 19:29–35
- 15Zec 9:9, Isa 62:11, Zep 3:16–17, Isa 35:4–5, 2Sa 16:2
- 16Jhn 2:22, Jhn 14:26, Jhn 7:39, Act 2:36, Jhn 12:23, Luk 18:34, Act 3:13, Luk 24:45
- 171Jn 5:9–12, Rev 1:2, Jhn 19:35, Act 1:22, Act 5:32, Jhn 12:9, Jhn 1:34, Psa 145:6–7
- 18Jhn 12:11
- 19Act 17:6, Psa 22:27, Act 4:16–17, 1Jn 2:2, Isa 27:6, Jhn 3:26, Jhn 17:21, Act 5:27–28
- 20Jhn 7:35, Act 17:4, Isa 11:10, Mrk 7:26, 1Ki 8:41–43, Act 8:27, Gal 2:3, Isa 60:2–14
- 21Mat 2:2, Luk 19:2–4, Jhn 6:40, Jhn 14:8–9, Mat 15:22–28, Jhn 1:36–39, Jhn 1:43–47, Mat 11:21
- 22Jhn 1:40–41, Luk 9:49–50, Mrk 10:13–14, Jhn 6:8, Mat 10:5
- 23Jhn 13:31–32, Jhn 17:1–5, Mrk 14:41, Isa 49:5–6, Isa 60:9, 1Pe 2:9–10, Isa 55:5, Isa 53:10–12
- 241Co 15:36–38, Isa 53:10–12, Heb 2:9–10, Jhn 12:32–33, Psa 72:16, Rev 7:9–17, Psa 22:22–31, Psa 22:15
- 25Mat 10:39, Luk 9:23–24, Mrk 8:35, Luk 17:33, Mat 16:25, Luk 14:26, Mat 19:29, Rev 12:11
- 26Col 3:24, 1Sa 2:30, Gal 1:10, Jhn 17:24, Jhn 10:27, 1Jn 5:3, Rom 1:1, 1Th 4:17–18
- 27Jhn 12:23, Isa 38:15, Heb 5:7, Jhn 13:21, Mat 26:42, Mrk 14:33–36, Mat 26:38–39, Psa 88:3
- 28Jhn 13:31–32, Mat 26:42, Jhn 11:40–44, Rev 5:9–14, Mat 17:5, Mat 3:17, Isa 49:3–7, Php 1:6–11
- 29Job 37:2–5, Rev 14:2, Rev 6:1, Exo 20:18, Exo 19:16, Job 40:9, Ezk 10:5, Rev 18:1–2
- 30Jhn 11:42, 2Co 8:9, Jhn 11:15, Jhn 5:34
- 312Co 4:4, 1Jn 3:8, 1Jn 5:19, Jhn 14:30, Eph 6:12, Heb 2:14, Col 2:15, Rev 20:2–3
- 32Jhn 8:28, Jhn 3:14, 1Pe 2:24, 1Jn 2:2, Jhn 1:7, Heb 2:9, Gal 3:13, 1Ti 2:6
- 33Jhn 18:32, Jhn 21:19
- 34Ezk 37:24–25, Isa 9:7, Dan 7:14, Psa 110:4, Dan 7:27, Dan 2:44, 2Sa 7:13, Jhn 3:14–16
- 35Jhn 12:46, Jhn 16:16, Eph 5:8, 1Jn 1:6–7, Jhn 8:12, Jhn 11:10, Jer 13:16–17, Jhn 12:36
- 36Eph 5:8, 1Th 5:5, Jhn 8:59, Jhn 1:7, Luk 16:8, Act 13:47–48, Isa 60:1, Mat 21:17
- 37Luk 16:31, Jhn 1:11, Jhn 15:24, Mat 11:20, Jhn 11:42
- 38Isa 53:1, Rom 10:16, Rom 10:20, 1Co 1:24, 2Co 4:3–6, 2Co 3:14–18, Mat 16:17, Gal 1:16
- 39Jhn 10:38, Isa 6:9–10, Jhn 5:44, 2Pe 2:14, Jhn 6:44, Isa 44:18–20
- 40Isa 6:10, Mat 13:13–15, Luk 8:10, Mrk 4:12, Isa 57:18–19, Hos 6:1, Jos 11:20, Isa 29:10
- 41Isa 6:1–5, Jhn 1:14, Isa 6:9–10, 2Co 4:6, Jhn 5:39, Jhn 1:18, Jhn 14:9, Heb 1:3
- 42Jhn 7:13, Isa 51:7, Jhn 9:22, Pro 29:25, Mat 10:32, Jhn 19:38, Isa 66:5, Jhn 11:45
- 43Jhn 5:44, Mat 23:5–7, Jhn 5:41, Luk 16:15, 2Co 10:18, 1Th 2:6, Luk 19:17, 1Sa 2:30
- 44Mat 10:40, Jhn 5:24, Jhn 13:20, Mrk 9:37, Jhn 7:28, 1Pe 1:21, Pro 8:1, Isa 55:1–3
- 45Jhn 14:9–10, 2Co 4:6, Col 1:15, Jhn 12:41, Heb 1:3, Jhn 15:24, 1Jn 5:20
- 46Jhn 8:12, Psa 36:9, Isa 42:7, Jhn 9:5, Jhn 12:35–36, Act 26:18, Jhn 3:19, Jhn 1:4–5
- 47Jhn 3:17, Jhn 8:15–16, Jhn 12:48, 1Ti 1:15–16, 1Jn 4:14, Luk 19:10, Mat 20:28, Jhn 5:45
- 48Luk 10:16, Heb 9:27–28, Rom 2:16, 2Th 1:8, Jhn 11:24, Jhn 3:17–20, Heb 12:25, Heb 10:29–31
- 49Jhn 14:10, Jhn 8:26, Jhn 5:30, Jhn 17:8, Deu 18:18, Jhn 14:31, Jhn 15:15, Jhn 8:42
- 50Jhn 17:3, Jhn 6:68, 1Jn 5:20, Jhn 6:63, 1Jn 2:25, 1Jn 5:11–13, 1Jn 3:23–24, Jhn 20:31
Parallelstellen
2
- The Triumphal EntryMat 21:1–11, Mrk 11:1–11, Luk 19:28–40, Jhn 12:12–19
- The Anointing at BethanyMat 26:6–13, Mrk 14:3–9, Jhn 12:1–8
Themen in diesem Kapitel
77
Andrew, Anointing, Apostles, Ass (Donkey), Bethany, Bethsaida, Blindness, Colt, Confession, Corn, Covetousness, Cowardice, Curiosity, Deacon, Deafness, Desire, Dishonesty, Faith, Feasts, God, Gospel, Greece, Heart, Heaven, Hosanna, Hospitality, Hypocrisy, Indecision, Israel, Prophecies Concerning, Jerusalem, Jesus, the Christ, Judas (Jude), Judgment, Law, Lazarus, Life, Light, Love, Martha, Martyrdom, Mary, Minister, Christian, Miracles, Obedience, Ointment, Opinion, Public, Palm Tree, Paradox, Parsimony (Stinginess), Persecution, Philip, Poor, Pound, Prayer, Presumption, Prophecy, Prudence, Quotations and Allusions, Responsibility, Righteous, Salvation, Satan, Self-Denial, Simon, Sin, Spikenard, Synagogue, Theft and Thieves, Unbelief, Voice, Wheat, Wicked (People), Wisdom, Word of God, Words, Worldliness, Zion