2 Wafalme 14
1 Katika mwaka wa pili wa utawala wa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli, Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Yehoadani, kutoka Yerusalemu.
3 Akatenda yaliyo mema machoni pa Mwenyezi Mungu, lakini sio kama Daudi baba yake alivyokuwa amefanya. Katika kila kitu alifuata mfano wa Yoashi baba yake.
4 Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
5 Baada ya ufalme kuimarika mkononi mwake, aliwaua maafisa waliomuua mfalme baba yake.
6 Hata hivyo, hakuwaua wana wa wale wauaji, sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Torati ya Musa, ambako Mwenyezi Mungu aliamuru, “Baba hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto kwa ajili ya baba zao. Kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe.”
7 Ndiye aliwashinda Waedomu elfu kumi katika Bonde la Chumvi, na akauteka Sela katika vita, naye akauita Yoktheeli, jina ambalo mji huo unalo hadi leo.
8 Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi, mwana wa Yehu, mfalme wa Israeli, akisema, “Njoo, tukabiliane uso kwa uso.”
9 Lakini Yehoashi mfalme wa Israeli akamjibu Amazia mfalme wa Yuda: “Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma ujumbe kwa mwerezi uliokuwa Lebanoni, ‘Mtoe binti yako aolewe na mwanangu.’ Kisha mnyama wa mwituni aliyekuwa Lebanoni akaja na kuukanyaga ule mbaruti.
10 Hakika umeishinda Edomu, na sasa unajivuna. Jisifu katika ushindi wako, lakini kaa nyumbani mwako! Kwa nini unachokoza na kujiletea anguko lako mwenyewe na la Yuda pia?”
11 Hata hivyo, Amazia hakusikia, hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia. Yeye na Amazia mfalme wa Yuda wakakutana uso kwa uso huko Beth-Shemeshi katika Yuda.
12 Yuda ikashindwa na Israeli, na kila mtu akakimbilia nyumbani mwake.
13 Yehoashi mfalme wa Israeli akamteka Amazia mfalme wa Yuda, mwana wa Yoashi, mwana wa Ahazia, huko Beth-Shemeshi. Kisha Yehoashi akaenda Yerusalemu na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu kuanzia Lango la Efraimu hadi Lango la Pembeni, sehemu yenye urefu wa kama dhiraa mia nne.
14 Akachukua dhahabu yote na fedha na vyombo vyote vilivyopatikana ndani ya Hekalu la Mwenyezi Mungu na katika hazina zote za jumba la mfalme. Akachukua pia mateka na akarudi Samaria.
15 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Yehoashi, aliyoyafanya na mafanikio yake, pamoja na vita vyake dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
16 Yehoashi akalala na baba zake, akazikwa Samaria na wafalme wa Israeli. Naye Yeroboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
17 Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda aliishi miaka kumi na tano baada ya kifo cha Yehoashi mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.
18 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Amazia, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
19 Wakapanga njama dhidi ya Amazia huko Yerusalemu, naye akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatilie huko Lakishi, nao wakamuua huko.
20 Akarudishwa kwa farasi, akazikwa huko Yerusalemu pamoja na baba zake katika Mji wa Daudi.
21 Kisha watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, na kumfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
22 Ndiye aliijenga upya Elathi na kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala na baba zake.
23 Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Amazia mwana wa Yoashi mfalme wa Yuda, Yeroboamu mwana wa Yehoashi mfalme wa Israeli alianza kutawala huko Samaria, naye akatawala kwa miaka arobaini na moja.
24 Akafanya maovu machoni pa Mwenyezi Mungu, na hakuacha dhambi hata moja ya Yeroboamu mwana wa Nebati, ambazo alikuwa amesababisha Israeli kuzitenda.
25 Ndiye alirudishia mipaka ya Israeli kuanzia Lebo-Hamathi hadi Bahari ya Araba, sawasawa na neno la Mwenyezi Mungu, Mungu wa Israeli, lililosemwa kupitia mtumishi wake Yona mwana wa Amitai, nabii kutoka Gath-Heferi.
26 Mwenyezi Mungu alikuwa ameona jinsi kila mmoja katika Israeli, awe mtumwa au aliye huru, alivyoteseka kwa uchungu; hapakuwa na yeyote wa kuwasaidia.
27 Kwa kuwa Mwenyezi Mungu alikuwa hajasema kuwa atafuta jina la Israeli chini ya mbingu, akawaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi.
28 Kuhusu matukio mengine ya utawala wa Yeroboamu, yote aliyoyafanya na mafanikio yake ya kijeshi, ikiwa ni pamoja na jinsi alivyorudisha Dameski na Hamathi kwa Israeli, ambayo ilikuwa mali ya Yuda, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
29 Yeroboamu akalala na baba zake, wafalme wa Israeli. Naye Zekaria mwanawe akawa mfalme baada yake.
Cross-references
165
- 12Ki 13:10, 2Ch 25:1–4, 1Ch 3:12, 2Ki 14:15
- 32Ch 25:2–3, 1Pe 1:18, 2Ch 25:14–16, 2Ki 12:2, Zec 1:4–6, Jer 16:19, 1Ki 11:4, 2Ch 24:17
- 42Ki 12:3, 2Ki 16:4, 2Ki 15:4, 2Ki 15:35
- 52Ch 25:3–4, 2Ki 12:20–21, Num 35:33, Gen 9:6, Exo 21:12–14
- 6Deu 24:16, Ezk 18:20, Ezk 18:4, Jer 31:30
- 72Sa 8:13, 1Ch 18:12, Jos 15:38, Psa 60:1, 2Ch 25:11–12, Isa 16:1, 2Ki 8:20–22
- 82Ch 25:17–24, 2Sa 2:14–17, 2Ki 14:11, Pro 25:8, Pro 17:14, Pro 20:18, Pro 13:10, Pro 18:6
- 9Jdg 9:8–15, Hos 9:6, 1Ki 4:33, 1Sa 13:6, 2Ch 33:11, 2Sa 12:1–4, Sng 2:2, 2Ch 25:10–13
- 10Deu 8:14, 2Ch 26:16, 2Ch 32:25, Pro 16:18, Pro 3:30, Pro 20:3, Pro 15:18, Jas 4:6
- 11Jos 19:38, 1Sa 6:9–19, 2Ch 25:16, Jos 21:16, 2Ch 25:20, Jos 15:10
- 122Sa 18:17, 1Sa 4:10, 1Ki 22:36
- 13Neh 8:16, Zec 14:10, Jer 31:38, Neh 12:39, Luk 14:11, Pro 16:18, Job 40:11–12, Pro 29:23
- 141Ki 7:51, 1Ki 14:26, 2Ki 18:23, 1Ki 15:18, 2Ki 12:18, 2Ki 24:13, 2Ki 25:15
- 152Ki 13:12–13, 2Ki 10:34–35, 1Ki 14:19–20
- 162Sa 7:12, Amo 7:10–11, Amo 1:1, 1Ki 1:21, Hos 1:1, 2Ki 13:13, 2Ki 13:9
- 172Ch 25:25–28, 2Ki 13:10, 2Ki 14:23, 2Ki 14:1–2
- 181Ki 11:41, 2Ki 13:8, 2Ki 13:12, 1Ki 14:29
- 19Jos 10:31, Mic 1:13, 2Ki 21:23, 2Ki 12:20–21, 2Ki 15:14, 2Ki 18:14, 2Ki 15:30, 2Ki 18:17
- 202Ki 9:28, 2Ch 33:20, 2Ch 26:23, 1Ki 2:10, 2Ki 8:24, 1Ki 11:43, 2Ki 12:21, 2Ch 21:20
- 21Mat 1:8–9, 2Ki 15:13, 1Ch 3:12, 2Ki 21:24, 2Ch 26:1
- 222Ki 16:6, 1Ki 9:26, Deu 2:8, 2Ch 8:17, 2Ch 26:2
- 23Hos 1:1, Amo 1:1, Amo 7:9–11, 2Ki 14:27
- 24Deu 9:18, Gen 38:7, 1Ki 12:28–31, 2Ki 13:2, 2Ki 13:11, 2Ki 13:6, 2Ki 21:6, 1Ki 21:25
- 25Deu 3:17, 1Ki 8:65, Jon 1:1, Jos 19:13, Mat 12:39–40, Num 13:21, Ezk 47:16–18, 2Ki 13:25
- 26Deu 32:36, 2Ki 13:4, Exo 3:7, Exo 3:9, Jdg 10:16, Psa 106:43–45, Isa 63:9, 1Ki 14:10
- 272Ki 13:23, 2Ki 13:5, Hos 1:6–7, Rev 3:5, Deu 29:20, Deu 25:19, Exo 32:32–33, Rom 11:2–12
- 281Ki 11:24, 1Ch 18:5–6, 2Sa 8:6, 2Ch 8:3–4
- 292Ki 15:8
Topics in this chapter
38
Amaziah, Ambassadors, Ambition, Amittai, Beth-Shemesh, Citizens, Conspiracy, Damascus, Edomites, Ephraim, Gath-Hepher, God, Hamath, Heart, Homicide, Hostage, Israel, Prophecies Concerning, Jehoaddan, Jehoash, Jeroboam, Jerusalem, Joktheel, Jonah, Lachish, Massacre, Parables, Pride, Prophecy, Regicide, Rulers, Salt, Sarcasm, Sela, Syria, Temple, Thistle, Uzziah, Zachariah