1 Samweli 19
1 Sauli akamwambia mwanawe Yonathani na watumishi wake wote wamuue Daudi. Lakini Yonathani mwana wa Sauli alimpenda sana Daudi.
2 Yonathani akamwonya Daudi, akisema, “Baba yangu Sauli anatafuta nafasi ya kukuua. Ujilinde kesho asubuhi, nenda mahali pa siri na ukae huko.
3 Nitatoka na kukaa na baba yangu shambani mahali uliko. Nitazungumza naye juu yako, nami nitakueleza nitakachogundua.”
4 Yonathani akanena mema kuhusu Daudi kwa Sauli baba yake na kumwambia, “Mfalme asitende mabaya kwa mtumishi wake Daudi; hajakukosea, aliyoyafanya yamekuwa ya faida sana kwako.
5 Alihatarisha maisha yake alipomuua yule Mfilisti. Mwenyezi Mungu akajipatia ushindi mkubwa kwa ajili ya Israeli wote, nawe uliuona na ukafurahi. Kwa nini basi utende mabaya kwa mtu asiye na hatia kama Daudi kwa kumuua bila sababu?”
6 Sauli akamsikiliza Yonathani na kuapa hivi: “Hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo, Daudi hatauawa.”
7 Basi Yonathani akamwita Daudi na kumweleza mazungumzo yote. Akamleta kwa Sauli, naye Daudi akawa pamoja na Sauli kama kwanza.
8 Vita vilitokea tena, naye Daudi akatoka na kupigana na Wafilisti. Akawapiga kwa nguvu nyingi hata wakakimbia mbele yake.
9 Lakini roho mbaya iliyoachiwa nafasi na Mwenyezi Mungu ikaja juu ya Sauli alipokuwa ameketi katika nyumba yake akiwa na mkuki mkononi mwake. Daudi alipokuwa anampigia kinubi,
10 Sauli akajaribu kumchomea Daudi ukutani kwa huo mkuki wake, lakini Daudi akauhepa huo mkuki wa Sauli ukakita ukutani. Usiku ule ule Daudi akakimbia na kuokoka.
11 Sauli akatuma watu nyumbani mwa Daudi wailinde hiyo nyumba na kumuua asubuhi. Lakini Mikali, mkewe Daudi, akamwonya akisema, “Usipokimbia kuokoa maisha yako usiku huu, kesho utauawa.”
12 Basi Mikali akamteremsha Daudi kupitia dirishani, naye akakimbia na kuokoka.
13 Kisha Mikali akachukua kinyago, akakilaza kitandani, akakifunika kwa vazi na kukiwekea singa za mbuzi kichwani.
14 Sauli alipotuma watu kumkamata Daudi, Mikali akasema, “Yeye ni mgonjwa.”
15 Kisha Sauli akatuma watu tena kumwona Daudi naye akawaambia, “Mleteni kwangu juu ya kitanda chake ili nipate kumuua.”
16 Lakini wale watu walipoingia, kumbe ni kinyago tu kilichokuwa kitandani, na kwenye kichwa kulikuwa na singa za mbuzi.
17 Sauli akamwambia Mikali, “Kwa nini umenidanganya mimi hivi na kumwacha adui yangu aende zake ili apate kuokoka?” Mikali akamwambia, “Yeye aliniambia, ‘Niache niende zangu. Kwa nini nikuue?’ ”
18 Daudi alipokuwa amekimbia na kuokoka, alimwendea Samweli huko Rama na kumwambia yale yote Sauli alimfanyia. Ndipo Daudi na Samweli wakaenda Nayothi kukaa huko.
19 Habari zikamfikia Sauli kusema: “Daudi yuko Nayothi huko Rama.”
20 Basi Sauli akatuma watu kumkamata Daudi, lakini walipoona kundi la manabii wakitoa unabii, wakiwa pamoja na Samweli akiwa amesimama hapo kama kiongozi wao, Roho wa Mungu akaja juu ya watu wa Sauli, nao pia wakatoa unabii.
21 Sauli akaelezwa hilo, naye akapeleka watu wengine zaidi, nao wakatoa unabii pia. Sauli akatuma watu mara ya tatu, nao pia wakatoa unabii.
22 Mwishowe, yeye mwenyewe akaondoka kwenda Rama na kwenda hadi kwenye kile kisima kikubwa kilichoko huko Seku. Naye akauliza, “Wako wapi Samweli na Daudi?” Wakasema, “Wako Nayothi huko Rama.”
23 Hivyo Sauli akaenda Nayothi huko Rama. Lakini Roho wa Mungu akaja juu yake hata yeye, akawa anatembea huku anatoa unabii hadi akafika Nayothi.
24 Akavua majoho yake na pia akatoa unabii mbele ya Samweli. Akalala hali hiyo ule mchana kutwa na usiku kucha. Hii ndiyo sababu watu husema, “Je, Sauli pia yumo miongoni mwa manabii?”
Cross-references
118
- 11Sa 18:1, 1Sa 18:9
- 2Pro 17:17, Act 9:24, Act 23:16, 1Jn 3:12–14, Psa 16:3, 1Sa 18:1–3, 1Sa 20:2, Jhn 15:17–19
- 31Sa 20:9, 1Sa 20:13
- 4Jer 18:20, Pro 31:8–9, Gen 42:22, 1Sa 20:32, Pro 17:13, 1Sa 22:14, Psa 109:4–5, Psa 35:12
- 51Ch 11:14, 1Sa 11:13, Jdg 9:17, Mat 27:4, 1Sa 20:32, Act 20:24, 1Sa 28:21, Psa 119:109
- 6Pro 26:24–25, Jer 5:2, 1Sa 19:10–11, Psa 15:4, 1Sa 14:39, 1Sa 28:10
- 71Sa 18:13, 1Sa 16:21, 1Sa 18:2, 1Sa 18:10, Gen 31:2, Isa 30:33, 1Ch 11:2, Exo 4:10
- 8Psa 27:3, Psa 18:32–50
- 91Sa 16:14, 1Sa 18:10–11, 1Sa 16:16
- 101Sa 20:33, 1Sa 18:11, Pro 21:30, Psa 34:19, Psa 124:7, Luk 4:30, 2Pe 2:20–22, Psa 18:17
- 11Psa 59:1–17, Jdg 16:2
- 12Jos 2:15, Act 9:24–25, 2Co 11:32–33, Psa 34:19
- 13Gen 31:19, Jdg 18:14, Jdg 18:17, Jdg 17:5, Hos 3:4
- 14Jos 2:5, 2Sa 16:17–19, 2Sa 17:20
- 15Psa 37:12, Job 31:31, Pro 27:3–4, 1Sa 19:6, Rom 3:15
- 172Sa 2:22, 2Sa 17:20, Mat 2:16, 1Sa 19:14, 1Ki 21:20, 1Sa 22:17, 1Sa 28:12, Exo 1:17–19
- 181Sa 7:17, 1Sa 28:3, Jas 5:16, 1Sa 15:34, Psa 116:11
- 191Sa 23:19, Pro 29:12, 1Sa 22:9–10, 1Sa 26:1
- 20Jol 2:28, 1Sa 10:5–6, Jhn 7:32, 1Co 14:24–25, 1Sa 10:10, 1Sa 19:11, 1Co 14:3, 1Sa 19:14
- 212Ki 1:9–13, Jol 2:28, Pro 27:22, Jer 13:23
- 23Pro 16:9, 1Sa 10:10, Num 24:2, 1Sa 19:20, 1Co 13:2, Pro 21:1, Num 23:5, Mat 7:22
- 242Sa 6:20, Isa 20:2, 1Sa 10:10–12, Mic 1:8, 2Sa 6:14, Num 24:4, Act 9:21