Ayubu 42
1 Ndipo Ayubu akamjibu Mwenyezi Mungu:
2 “Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
3 Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema mambo nisiyoyaelewa, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
4 “Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
5 Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
6 Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
7 Baada ya Mwenyezi Mungu kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira nawe na rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kunihusu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
8 Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu atawaombea, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
9 Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Mwenyezi Mungu alivyowaambia; naye Mwenyezi Mungu akayakubali maombi ya Ayubu.
10 Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Mwenyezi Mungu akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
11 Ndipo ndugu zake na dada zake wote, na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni wakaja, wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Mwenyezi Mungu aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
12 Mwenyezi Mungu akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda jike elfu moja.
13 Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
14 Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia, na wa tatu Keren-Hapuki.
15 Katika nchi ile yote hakukuwa wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
16 Baada ya hili Ayubu akaishi miaka mia moja na arobaini; akawaona wanawe, na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
17 Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyeshiba siku.
Querverweise
103
- 2Mat 19:26, Mrk 10:27, Gen 18:14, Heb 4:12–13, Jer 32:17, Isa 46:10, Eph 1:11, Pro 19:21
- 3Psa 131:1, Psa 139:6, Job 38:2, Psa 40:5, Pro 30:2–4
- 4Job 40:7, Job 38:3, Gen 18:30–32, Gen 18:27
- 5Eph 1:17–18, Rom 10:17, Jhn 12:45, Jhn 12:41, Isa 6:1, Isa 6:5, Job 26:14, Job 4:12
- 6Ezr 9:6, Jas 4:7–10, 1Ti 1:13–16, Job 40:3–4, Dan 9:3, Job 30:19, Ezk 36:31, Job 2:8
- 7Job 11:5–6, Job 32:2–3, Job 32:5, Psa 51:4, Job 4:1, Job 2:11, Job 8:1
- 8Num 23:1, Jas 5:16, Psa 103:10, Job 22:30, 1Ch 15:26, Gen 20:17, Ezk 14:14, Mat 3:17
- 9Heb 11:8, Act 9:6, Act 10:33, Mat 7:24, Jhn 2:5, Ecc 9:7, Job 22:27, Pro 3:11–12
- 10Deu 30:3, Job 8:6–7, Pro 22:4, Isa 40:2, Isa 61:7, Psa 14:7, Psa 126:1, Act 7:50
- 11Job 19:13–14, Job 2:11, Pro 16:7, Gen 24:22, Heb 12:12, Rom 12:15, Gen 37:35, Gen 24:53
- 12Job 8:7, Ecc 7:8, Pro 10:22, Gen 24:35, Psa 144:13–15, Job 1:3, Gen 26:12–14, Deu 8:16
- 13Job 1:2, Isa 49:20, Psa 127:3, Psa 107:41
- 15Num 27:7, Psa 144:12, Jos 18:4, Act 7:20, Jos 15:18–19
- 16Pro 17:6, Gen 50:23, Psa 128:6, Gen 25:7, Gen 47:28, Gen 50:26, Jos 24:29, Gen 35:28
- 17Gen 25:8, Job 5:26, Gen 15:15, Psa 91:16, Deu 6:2, Pro 3:16
Themen in diesem Kapitel
23
Ashes, Blessing, Dust, Eliphaz, Faith, God, Humility, Inheritance, Intercession, Jemima, Job, Keren-Happuch, Kezia, Longevity, Love, Old Age, Prayer, Repentance, Sin, Uncharitableness, Wisdom, Women, Zophar